Kagera Sugar vs Simba SC

Kagera Sugar vs Simba SC

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Team zipo kwenye maandalizi. Kagera Sugar wamejipanga vizuri kuweza jipigia Simba hii mbovu ambayo kila atakaye anajipigia. Kagera wametamba kuwa ushindi kwao ni lazima. Yaani wakimkosa kosa sana Simba basi ni draw.

Simba inaingia uwanjani ikiwa na woga siku zote inapopambana na Kagera huwa nyasi zinawaka moto na wakijitahidi sana hasa Kagera akiwa nyumbani huwa ni sare.

Hivyo tutegemee match yenye ushindani mkubwa sana kutokana na ukweli kuwa team ya Kagera imekuwa ikipata ushauri mzuri kutoka Yanga. Na wameshapewa mbinu za kuifunga Simba kutokana na ukweli wa Simba mwaka huu kagawa points 6 kwa Yanga.

Msikae mbali. Tupate matangazo ya wadhamini kwanza. Wakati huu Juma Mgunda akinywa Uji na wachezaji wake wakinywa chai ya hudhurungi na andazi moja moja isipokuwa namwona Kibu Denis yeye ameshika pande la muhogo wa kuchemsha.

Mchana umefika

Wachezaji wa Simba wanajikusanya wapo waliokuwa wamelala chini ya miti hapa Lodge walipofikia, na wengine nimewaona wanacheza karata. Kuna ambao walitoka mida flani kwenda mjini angalau kupata chochote kitu.

Sasa wamerudi naona wanapewa kila mtu chips kavu na kachumbari nyingi. Kila mmoja amekadhiwa Mo Energy ashushie huku wakisubiria match hapo baadaye.

Msitoke ndugu wapenzi wa mpira.
 
Simba hatapoteza mechi hata Moja kwa zilizobaki
Hii huwa ni kawaida kwake hata msimu uliopita ilikuwa hivyo na lengo huwa ni kuamsha hali ya mashabiki kuelekea Simba day
 
Team zipo kwenye maandalizi. Kagera Sugar wamejipanga vizuri kuweza jipigia Simba hii mbovu ambayo kila atakaye anajipigia. Kagera wametamba kuwa ushindi kwao ni lazima. Yaani wakimkosa kosa sana Simba basi ni draw.

Simba inaingia uwanjani ikiwa na woga siku zote inapopambana na Kagera huwa nyasi zinawaka moto na wakijitahidi sana hasa Kagera akiwa nyumbani huwa ni sare.

Hivyo tutegemee match yenye ushindani mkubwa sana kutokana na ukweli kuwa team ya Kagera imekuwa ikipata ushauri mzuri kutoka Yanga. Na wameshapewa mbinu za kuifunga Simba kutokana na ukweli wa Simba mwaka huu kagawa points 6 kwa Yanga.

Msikae mbali. Tupate matangazo ya wadhamini kwanza. Wakati huu Juma Mgunda akinywa Uji na wachezaji wake wakinywa chai ya hudhurungi na andazi moja moja isipokuwa namwona Kibu Denis yeye ameshika pande la muhogo wa kuchemsha.
Haina ushindani hivi Kagera nguvu za kucheza wanazitoa wapi, wamesafiri kwa basi kutoka Dar kwenda Bukoba usiku wa trh 8 baada ya mechi na yanga na wamefika jana, na leo wacheze na Simba.
 
Simba hatapoteza mechi hata Moja kwa zilizobaki
Hii huwa ni kawaida kwake hata msimu uliopita ilikuwa hivyo na lengo huwa ni kuamsha hali ya mashabiki kuelekea Simba day
Kwa kama sio kuelekea simba day huwa wanapoteza kusudi au kuzidiwa
 
Unfortunately hadi nyuzi zenu mnasusia kuchangia
 
Simba hatapoteza mechi hata Moja kwa zilizobaki
Hii huwa ni kawaida kwake hata msimu uliopita ilikuwa hivyo na lengo huwa ni kuamsha hali ya mashabiki kuelekea Simba day
Hii kagera sugar imekamilika usiichukulie powa
 
Back
Top Bottom