Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Wakuu,
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Kagera imewaonya wagombea wa nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024, kutojihusisha na vitendo vya rushwa.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kagera, Ezekia Senkara, alisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo.
Soma pia: Msemaji Mkuu Wa Serikali: Serikali haifurahishwi na taarifa potofu katika kipindi hiki cha Uchaguzi. Watanzania fuateni sheria
Akitoa taarifa ya utendaji wa TAKUKURU kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2024, Senkara alieleza kuwa taasisi hiyo inaendelea kuhamasisha wananchi kupitia elimu ya kupambana na rushwa kuelekea uchaguzi.
Hadi sasa, hakuna mtu aliyekamatwa kwa kutoa au kupokea rushwa, wala kesi yoyote inayohusiana na rushwa kufikishwa mahakamani.
Source: Global TV Online
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Kagera imewaonya wagombea wa nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024, kutojihusisha na vitendo vya rushwa.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kagera, Ezekia Senkara, alisisitiza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo.
Soma pia: Msemaji Mkuu Wa Serikali: Serikali haifurahishwi na taarifa potofu katika kipindi hiki cha Uchaguzi. Watanzania fuateni sheria
Akitoa taarifa ya utendaji wa TAKUKURU kwa kipindi cha Julai hadi Septemba 2024, Senkara alieleza kuwa taasisi hiyo inaendelea kuhamasisha wananchi kupitia elimu ya kupambana na rushwa kuelekea uchaguzi.
Hadi sasa, hakuna mtu aliyekamatwa kwa kutoa au kupokea rushwa, wala kesi yoyote inayohusiana na rushwa kufikishwa mahakamani.
Source: Global TV Online