KERO Kagera: Ukosefu wa vyoo bora Shule ya msingi Mugana A unahatarisha usalama wa afya za wanafunzi

KERO Kagera: Ukosefu wa vyoo bora Shule ya msingi Mugana A unahatarisha usalama wa afya za wanafunzi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Jovinus Mujuni

New Member
Joined
Dec 18, 2024
Posts
2
Reaction score
2
Jamani hivi suala la kujengea wanafunzi vyoo ni jukumu la nani? maana Kuna shule moja wilaya ya Missenyi mkoani Kagerainaitwa Mugana A kwakweli hali ya vyoo sio salama kwa watoto wale kwani vimechakaa mno na havikidhi mahitaji yao kwani wataambulia kupata magonjwa.

Hivyo wahusika tunaomba hili suala muweze kulitilia maanani maana hizo ni afya za watoto wetu, kwanza vyoo havina miundombinu ya maji na suala hili limekuwa kero ya muda mrefu.

Hivyo kupitia jukwaa hili naomba wahusika muweze kulivaa hili na kuweza kuwasaidia watoto hawa kupata vyoo safi na vya kisasa.
Screenshot 2025-01-10 12.42.15 PM.png

Screenshot 2025-01-10 12.40.15 PM.png

Screenshot 2025-01-10 12.39.34 PM.png
 
Back
Top Bottom