Kagere ni chukizo, ana kera, anakwaza, anaudhi, anasumbua, mkatili, hafai na hana huruma akiwa mbele ya nyavu

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Wakati Simba wanamchukua tulisema babu, mzee hafai n.k lakini huyu jamaa ana sifa zote mbaya na za binadamu katili asiyefaa kuwahi tokea katika soka la Tanzania.

Sijajua zaidi niseme nini .. mengine semeni nyie ila mimi namchukia sana huyu jamaa.
 
Ilifaaa awe anakutana na Al Ahly,Casablanca,mazembe,Lakin kama alishindwa kutoboa ngome ya UD songo.......kwa hakika huyu ni kufikiria mara 2.Unategemea ashinde kufunga mechi na Alience,Ndanda,Singida,polisi,halafu mshahara mil 12?

Kipimo sahihi cha simba ilikuwa ni wahuni wa UD songo baasi.Ila hao Biashara aaah!atafunga sana.Shida ni UD songo baasi
 
Alikuwa wapi ujana wake wote? Mdogo wake Drogba baada ya kusumbua sana kesha staafu yeye bado anagombea namba na kina Mohd Rashidi!
 
Wakati Simba wanamchukua tulisema babu,mzee hafai n.k lakini huyu jamaa ana sifa zote mbaya na za binadamu katili asiyefaa kuwahi tokea katika soka la tanzania.

Sijajua zaidi niseme nini .. mengine semeni nyie.ila mimi namchukia sana huyu jamaa.
Yaani anakera sana, hasa katika kuvaa vikuku
 
Kagere hovyo kabisa mpaka acheze na Namungo, Ndanda, Njombe Mji ndio anafunga . Mechi muhimu na UD SONGO dakika 180 hakupiga hata shuti moja golini.
 
Hakuna kama Kagere Afrika ya Mashariki, amefunga goli 6 katika ligi ya Mabingwa Africa iliyoisha May mwaka huu akiwa mfungaji bora namba 2, baadhi ya timu alizozifunga mwaka huu ni pamoja na hiyo ulioitaja Al Ahly angalia pia angalia Unafahamu ya kwamba Mwaka huu Simba wame mboreshea mkataba wake ambao ulikuwa uishe Juni 2020 na sasa atakuwepo hadi Juni 2021? na huo mshahara wa milioni 12 kwa mwezi ulikuwa wa mkataba wa mwaka jana, sasa umeboreshwa.

Kushindwa kuifunga UD Songo siyo issue labda kama ni kilaza wa mambo ya kabumbu, Hao akina Messi, Ronaldo hufululiza hata mechi 7 bila kufunga itakuwa Kagere. Hata hivyo rekodi ya Kagere toka ajiunge na Simba Mwaka jana hakuna aliyeifikia ligi ya bongo miaka 10 iliyopita Magoli 23 ligi ya bara na sasa bado anaendelea tayari kafunga mechi magoli mechi 5 mfululizo
 
Ahaa.Ndo ujue sasa kakutana na wabovu wenzie akikutana na vigongo kama UD songo anapotea.Kwa sababu mechi ile alipotea hata hivyo kupotea mechi 2 sio sababu.Lakin kwa mimi najua Kagere kwa simba inaweza kuwa ndo bora wa muda wote ila kwa Yanga tuna watu kama Ben Mwalala,Bony Ambani,Jerry Tegete, hao ni baadhi ya mastraika bora zaidi kuwahi kutokea kwa ligi ya Bongo.
 
Kuna vibaka wanabisha huku matumbo yao yanaunguruma kwa kihoro. Mungu awalaze kwenye giza wale wote wasiomkubali MK 14!
 
Kagere hovyo kabisa mpaka acheze na Namungo, Ndanda, Njombe Mji ndio anafunga . Mechi muhimu na UD SONGO dakika 180 hakupiga hata shuti moja golini.
Umeiacha gogowazi hapo kwenye list..maana nao aliwatungua vilivyo..!
 
Mkuu straika bora ni late Masamaki Thomas
Anarekodi ya kufunga 25+ goals per msimu
 
Acha kufananisha Kagere na uchafu wakina Tegete
 
Idadi ya mgori yake sawa na points za Yanga. Msimu huu anaweza kutikisha magoli 50
 
Ingawa Mimi si shabiki wa Simba kiukweli jamaa anajua kufunga, hata takwimu hazidanganyi
 
Mbona hujasema shida ni yanga...naona ukikumbuka jinsi alivyowatoboa yanga unaweweseka mkuu
 
Kagere hovyo kabisa mpaka acheze na Namungo, Ndanda, Njombe Mji ndio anafunga . Mechi muhimu na UD SONGO dakika 180 hakupiga hata shuti moja golini.
Hapo kwenye namungo,ndanda,njombe mji,ongezea na yanga mkuu
 
Kwa hiyo yanga ni moja kati ya wabovu aliokutana nao???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…