Kahama VS Njombe/Mafinga

Ziara ya Wahariri wa Vyombo vya Habari, kutembelea kiwanda cha Mipira ya Mikono cha MSD Idofi, kilichoko Makambako Mkoani Njombe.
 

MSD ILIVYOIBEBA AJENDA RAIS SAMIA KUPITIA KIWANDA CHA KUTENGENEZA GLOVES IDOFI


MICHUZI BLOG AT WEDNESDAY, JULY 03, 2024 MAKALA,

Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Makambaku

UKWELI ni kwamba Bohari ya Dawa (MSD) imedhamiria kuhakikisha inaendeleza mkakati wake wa kuzalisha bidhaa za afya ikiwemo mipira ya mikononi maarufu โ€˜glavesโ€™.

Ukiwa katika kiwanda chake cha kuzalisha glaves kilicopo eneo la Idofi Halmashauri ya Makambako mkoani Njombe utashuhudia kiwanda hicho ambacho ujenzi wake ulianza Oktoba 4, 2020 kikiendelea na uzalishaji ulioanza rasmi Februari mwaka huu na hadi sasa jozi milioni mbili za glaves zimeshatengenezwa.

Ni wazi MSD chini ya uongozi mahiri wa Mkurugenzi Mkuu wake Mavere Tukai imeamua kubeba kwa vitendo dhamira ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kiwanda cha Gloves Idofi kinazalisha mipira ya mkono na hatimaye kuokoa fedha ya serikali iliyokuwa ikitengwa kuagiza mipira hiyo nje ya nchi.

Akizungumza na wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari waliotembelea kiwanda hicho, Mhandisi Shiwa Mushi ambaye ni Kaimu Meneja Kiwanda cha Glovu MSD Idofi anaeleza hatua kwa hatua kuhusu sababu za kuanzishwa kwa kiwanda hicho na uzalishaji unaoendelea kwa sasa.

HISTORIA YA KIWANDA

Kwa mujibu wa Mhandisi Mushi, kiwanda hicho kinamilikiwa na MSD na kilianza kujengwa Oktoba 4, mwaka 2020 na dhumuni la kujengwa kwake ni kutokana na changamoto ya ugonjwa wa Uviko-19 mwaka 2019.

โ€œWakati wa janga la Korona miongoni mwa changaoto tulizozipata kama taasisi na nchi kwa ujumla ni uingizaji wa vifaa tiba nchini, kutokana na vizuizi na uagizaji wa dawa ilikuwa changamoto kubwa.

โ€œKwa hiyo nchi ikaona kuna haja pia kuanza kuanzisha viwanda vyake hasa kutokana na somo ambalo tumelipata na tukaona kiwanda cha aina ya glaves ni muhimu tukaanza nacho kwasababu tumekwenda kwenye changamoto ya upungufu wa vifaa tiba nchini.

โ€œNa ukiweza kuvaa glaves utaweza kuwahudumia wagonjwa hata kama ni wa Korona kwa usalama zaidi. Kwa hiyo tukaanza na kiwanda cha gloves ambacho kimejengwa Idofi, Makambako katika eneo lenye ukubwa wa ekari 38 na MSD inalimiki kisheria na ililitwaa kutoka kwa wananchi wa Idofi, tumewalipa na sasa eneo hili lina hati.โ€

MAJENGO YALIYOPO

Mhandisi Mushi anaeleza katika eneo hilo la kiwanda kuna majengo mengi yanayotoa picha ya kiwanda hicho na jengo hilo la kiwanda lina urefu wa mita 130 na upana mita 124 kwa maana kwamba ukiangalia mita za mraba 3,120.

Anasema katika hayo majengo lipo jengo la malighafi kwa ajili ya uzalishaji na majengo mawili mengine wamepanga yatakuwa kituo cha kiwanda cha gloves na wakiendelea na uzalishaji vizuri na kufanya biashara watajenga majengo mengine.

โ€œKwa upande wa kulia kwenye michoro yetu kuna majengo ambayo kwa sasa yapo kwa ajili ya uhifadhi wa bidhaa,โ€ anafafanua.

AINA MBILI ZA GLOVES

Pamoja na hayo anasema mikakati ya kiwanda ni kuzalisha aina mbili za glaves ambazo ni Surgical glove (zinatomika kuvaa kwenye upasuaji) na Examination glave (Glavu zinazovaliwa wakati wa uchunguzi wa awali).

KIMEBAKISHA SEHEMU MBILI

Akitoa maelezo zaidi ya kiwanda hicho, Mhandisi Mushi anasema kimebakisha sehemu mbili katika mkakati wa uzalishaji huku akifafanua kuwa kinakwenda kuzalisha pisi 20,000 ambazo ni sawa na pea 10,000 na hiyo ni kama kinazalisha katika hali yake ya kawaida.

โ€œNa kiwanda hiki ukifanya mahesabu kitaalamu inaonesha kwa mwaka kitazalisha jumla ya glaves jozi milioni 86.4, ambazo ni sawa na asilimia 86.34 ya mahitaji ya nchi.

โ€œKwa hali hii unaweza kuona kiwanda hiki ni kikubwa kwa kiasi gani, na sasa tumebaki na uzalishaji wa Examinationa glaves, ambapo katika kuzalisha kunahitajika malighafi.โ€
 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Makambako Keneth Haule amesema standi ya kisasa ya mabasi mjini Makambako itajengwa ilipo hivi sasa badala ya Kipagamo ambako awali walipendekeza ijengwe.

Haule ameyasema hayo wakati wa mkutano wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020-2025 kwa kipindi cha miaka mitatu ambayo imefanyika katika ukumbi wa Green City, ambapo amesema eneo liliopendekezwa ijengwe standi ya kisasa ni lilelile iliyopo standi ya sasa.

Mkurugenzi huyo amesema halmashauri itajenga soko la kisasa na kueleza kuwa mwezi wa nane mwaka huu watapokea mhandishi mshauri ambaye atakuja kutengeneza mpango kabambe (Master plan) wa mji wa mji wa Makambako pamoja na kuanza usanifu ujenzi wa standi na soko.

Aidha Haule amesema katika mwaka huu wa fedha Halmashauri imekusudia kujenga vituo vya kuegeshea magari makubwa maroli katika mitaa ya Mizani iringa road na Kahawa eneo ambalo linatumika kuoshea magari kwa sasa. Songea road
 
Mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika kujadili utekelezaji wa maazimio na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na wakuu wa nchi hizo mbili wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan iliyofanyika nchini China mwezi Novemba 2023.

Aidha, wameainisha maeneo mbalimbali ya kimkakati ambayo nchi hizo mbili zimedhamiria kuziendeleza na kuzisimamia kwa maenedeo ya watu wake. Maeneo hayo ni pamoja na kuanzisha na kuimarisha ushirikiano wa miji dada, kukuza ushirikiano wa biashara na uwekezaji, ujenzi wa miji ya kisasa, maendeleo ya viwanda, kilimo cha kisasa na uongezaji wa thamani ya mazao ya kilimo na mifugo na kuboresha mradi wa reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA).
 
VIWANDA VYA CHUMA NA MADINI YA CHUMA MKOA WA NJOMBE YANAENDA KUIBADILI TANZANIA WAWEKEZAJI WANAZIDI KUJA TU ๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Wajapani kufungua sehemu za kuunganisha, kutengeneza na kuuza magari nchini

Wafanyabiashara wa Kijapani wanatarajia kufungua sehemu za uunganishaji, utengeneza na uuzaji wa magari nchini ili kusaidia watanzania wenye uhitaji kuyapata kwa urahisi.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), Latifa Hamis katika Kongamamo la Kibiashara amablo limepewa jina la Siku ya Japan.

Latifa amesema hatua hiyo ya Wajapan kuja kuwekeza nchini Tanzania ni kutokana na kuona kuwa kuna idadi kubwa ya Watanzania wanayoyapenda na kununua magari yao.

Aidha amesema Kongamano hilo la Japan day limejumuisha wafanyabiashara wa Japan na wa Tanzania kukutana na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo fursa zilizopo Tanzania.

Amesema kupitia maonesho haya ya 48 ya Biashara ya Kimataifa ni wakati wa Watanzania kujitokeza kwa wingi kuona fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana kupitia maonesho hayo ambayo nchi ya Japan ni mojawapo wanaoshiriki katika banda la Karume.

Aidha amesema lengo lingine la mkutano huo ni kutafuta fursa za wafanyabiashara wa Japan kuwekeza nchini huku wafanyabiashara wa nchi hiyo wakionesha bidhaa mbalimbali kama kompyuta, simu na magari.

โ€œMkutano huo umehudhuriwa na kampuni tisa katika sekta mbalimbali kama uvuvi, afya, teknolojia, kilimo na usafirishaji ambazo zimekuwa zikionesha fursa za uwekezaji zilizopo,โ€ amesema.

Amesema mikutano hiyo itakuwa inafanyika katika kipindi chote cha maonesho huku wakizikutanisha nchi zilizoshiriki kuonesha fursa zilizopo.

Kwa upande wake Balozi wa Japan nchini, Yasushi Misawa amesema amevutiwa na maonesho hayo kwani yanawapa fursa ya kujifunza vitu vingi kutoka Tanzania.

โ€œWatanzania watajifunza kutoka kwetu na sisi tutajifunza kutoka kwao hivyo kuna vitu tunavyo na Tanzania havipo na vingine wanavyo na sisi hatuna,โ€™โ€™amesema

Amesema ushirikiano uliopo wa miaka mingi kati ya Tanzania na Japan unahitajika kuendelezwa na uimarisha wa uchumi wa nchi zetu.

Written by @janethjv255
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ