Kahama VS Njombe/Mafinga

Eneo ambalo tanroad wamelipa fidia kwaajili ya ujenzi wa one stop centre idofi makambako limeanzia mpakani mwa iringa na njombe
 

Attachments

  • IMG-20240520-WA0027.jpg
    35 KB · Views: 2
Mimi nadhani inatakiwa kutoboa na kujenga Barabara kuu kutoka Makambako directly Hadi Mlimba kama njia Mbadala ya ku bypass Ile escarpment ya Kitonga badala ya hiyo ya Tarura ambayo inaunga Makambako-Njombe-Songea Highway na Njombe-Mikumi-Kilosa-Handeni-Korogwe Highway.

Kama reli Imepita Barabara inashindikanaje? Na ikiwezekana ikapite Hadi Mgololo inaweza anzia hata hapo Nyigo sio lazima Makambako kabisa Bado italeta maana sana Kwa magari Yanayoenda Dar kutokea Mbeya kuchagua route ya Kupitia.
 
Upo sahihi na hili wazo na iman mbeleni watakuja kulitekeleza Kwa Sababu pale ni short cut mfano Kwa njia ya RELI makambako hadi mlimba ni km 163 ni sawa na makambako iringa ko hii Barabara itakuwa fupi mno ngoja wamalize kukifungua kipande Cha mlimba hadi mgololo hapo ndo watauona umuhimu wake
 
Barabara hizi nilizoziwekea rangi ya kijani ni muhimu sana kuzifungua huko mbele,maana tunazunguka zunguka sana bila sababu za msingi wakati hizo sio tuu ni shortcut ila zinafungua uchumi Mpya.

Hope Vijana wa kizazi hicho sometimes beyond 2030 watafikoria kuzifungua,sio Kila kitu lazima tuwafuate wakoloni πŸ‘‡πŸ‘‡

Mfano haiwezi Katavi na Tabora hazijaunganishwa na Iringa na Mikoa ya Mtwara wakati possibility zipo hakuna vikwazo vikubwa kama Ziwa ,milima inachimbuliwa vizuri tuu
 
Kabisa Yan kwa teknolojia ya Sasa milima sio kikwazo tena Cha msingi hiz njia za short cut wazifungue tu kurahisisha usafirishaji sio kuzungukazunguka hakuna tija kabisa na hii itasaidia kutoa misongamano isiyokuwa ya lazima alafu Kuna eneo hili kutoka makambako Rujewa hadi kuunganisha na road ya chunya tabora Halina vikwazo ni tambarare ya kutosha tena itakuwa short cut kwenda mikoa ya magharibi na Kanda ya ziwa
 
MRADI MKUBWA WA UMWAGILIAJI MKOA WA NJOMBE UNATEKELEZWA NDANI YA HALMASHAURI MBILI NJOMBE DC NA MAKAMBAKO TC WENYE UKUBWA EKARI ZAID YA 1000 KWELI MKOA UMEAMUA KULIENDELEZA HILI ENEO KIVIWANDA NA BIASHARA ZAIDI KUNA UBUNIFU WA KILA NAMNA πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amepiga marufuku wananchi wa Kijiji cha Itipingi kilichopo Kata ya Igongolo wilayani Njombe kutumia eneo la mradi wa umwagiliaji wenye thamani ya shilingi Bilioni 5.5 kama eneo la malisho ya mifugo.

Mhe. Mtaka ametoa kauli hiyo Julai 9, 2024 akiwa katika kijiji cha Itipingi kwaajili ya kushuhudia makabidhiano ya mradi wa umwagiliaji unaotekelezwa kwa awamu ya pili kati ya mkandarasi na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Mradi huo unaotarajiwa kuhudumia wananchi 417 kutoka kata mbili na Vijiji vitatu vya Itipingi, Kiumba na Malombwe umekabidhiwa mbele ya mkandarasi ili uanze kutekelezwa kwa awamu ya pili.
 

View: https://www.instagram.com/p/C9QVWcSs_SD/?igsh=MWl6NHJ6OGtyMnBidQ==
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…