Me ni mwabafunzi wa chuo nina ndoto ya kua mkulima mkubwa wa mpunga lakin sifaham inahitajik mtaji kias gani tafadhar naomb nisaidiwe
Naweza nikajibu kama ifuatavyo kulingana na eneo la bonde la Usangu kuanzia Ilongo mpaka Igawa ( kusahihishwa ni ruksa).
Kulima kwa powertiller- Tsh 50000
Kuvuruga (kuchanganya tope)- Tsh 50000
Mbegu inategemeana na msimu- mfano mwaka huu ilikuwa ni Tsh 36000, kwa wastani wa debe za mpunga kwa heka kama unapanda randomly bila kamba na kama unapanda kwa kutumia kamba ni kiasi kama cha nusu debe tu (10 litres).
Kupanda ilikuwa inaanzia Tsh 80000-Tsh 12000 inategemeana na muda wa kupanda kama ni mwezi wa 12, 1, 2 au wa tatu.
Mbolea kwa DAP ni Tsh 70000( kwa bei ya ruzuku) na kawaida ilikuwa Tsh 110000 hivi.
Kujazia matuta ya kukinga maji ni Tsh 20000 kwa heka kama matuta yalikuwapo, ila kama hayakuwepo ni kuyapanga upya ni Tsh 40000.
Kusawazisha heka ni Tsh 20000 kama mvurugaji alivuruga vibaya, ila inaweza kushuka au kupanda kutegemeana na mvurugaji.
Dawa ya kuua magugu andaa kama Tsh 35000 hivi.
Palizi andaa kuanzia Tsh 30000, inategemeana na magugu kama yalikufa kwa kiwango kikubwa ila haiwezi kupungua hiyo bei na inaweza kuongezeka.
Dawa ya wadudu na mpigaji andaa Tsh 20000.
Kuvuna kwa kombaini andaa Tsh 150000 kwa heka.
Mifuko ya kuvunia andaa kama Tsh 30000 .
Wakukusanya vipeto andaa kama 30000 ya makuli, ila inaweza kupungua na pia kupanda kutegemeana na uwepo wa maji shambani.
Kuanika andaa kama 6000 .
Kushona na kuchekecha ni kama andaa 18000+ 30000 ya mifuko.
Usafiri kutoka shambani mpaka mbeya mjini Sido andaa kama 2500-3500 kwa njia ya ilongo na kutoka igawa huko ubaruku andaa kama 4000-5000 kwa kiroba kimoja.
Pakia shusha 1200 kwa kila kiroba.
Zingatia ; bei hizo za baaada ya uvunaji hutegemea na mavuno yapo kiasi gani uliypopata. Na hii ni eneo tajwa la bonde la Usangu.
Naruhusu marekebisho