Kaka na Dada hawa...Mhh!

Hapo naona wazazi wa hao vijana wanampa mzigo Bibi katika kuwalea pamoja na kichanga chao hivyo wanamtesa bure bibi wa watu..
 
Hapo naona wazazi wa hao vijana wanampa mzigo Bibi katika kuwalea pamoja na kichanga chao hivyo wanamtesa bure bibi wa watu..
Sio jukumu la bibi wala wazazi ni jukum la wazazi wa kichanga. Wakaanzishe maisha yao hawajachelewa provided imani au jamii yao inaruhusu
 
Hao kweli ni ndugu, ila hawajatoka tumbo moja, ni mtoto wa dada mkubwa na dada mdogo, kwa mila za kiarabu hao ruhusa kabisa kuoana.Tatizo ni huko kuzini au kama mila zao haziruhusu. Kama sio waarabu hapo ndio kasheshe sasa. Mie nina rafiki yangu ni mwarabu hapa hapa bongo, kaolewa na kaka yake mtoto wa baba yake mkubwa. Baba zao ni tumbo moja.
Maji yamemwagika hivyo hayawezi kuzoleka, hivyo kuwasusa hao watoto haitasaidia kitu.Cha muhimu hao wazazi wawakalishe hao watoto na kuwaambia kwamba mlifanya kosa na kimila kwao haikubaliki, hivyo inabidi watengane. Hii inaweza kusaidia uwezekano wa hao watoto wao kutokuwa pamoja kimapenzi na hivyo kutoweza kuzaa mtoto mwingine.
 

Nyaralego,

1. Mbona ng'ombe, mbuzi wanazaliana tu..na je pia hii huwa kuleta recessive genes? Naomba mwanga na elimu kidogo!

2. Socially: sijui inakuwaje hata mtu unakuwa attracted na kulala na dada au kaka!

Wangepimwa akili!
 

Mbona Sheria on incest ipo jirani? Je ni kwanini haifanyi kazi- hilo ni tatizo la kijamii.Jamii huwa inaona vibaya au tuseme familia hujitahidi kuficha aibu hii na matokeo yake ndio vitendo kuendelea with impunity.
Ila ni aibu sana sijui inaanzaje hadi ndugu wa damu kuanza kutamaniana!
 
Ni kweli waarabu huwa wanaoana binamu na utamaduni huo unatekelezwa pia na waislamu walio wengi. Hata Bongo karibu waislamu wengi tu si tatizo kuoa binabu, ila kuzini hairuhusiwi. Kisichokubalika ni ndugu wa kutoka upande wa mama (kama walivyo hawa wawili). Kwa waarabu, waislamu na watu wengi wa pwani ya Tz, Kenya Zenji Comorro na kwengineko, unaruhusiwa kuoana na mtoto wa baba yako mdogo/mkubwa na pia watoto wa shangazi kwa mjomba. Lakini si kwa watoto wa mama mdogo/mkubwa. Sijui ni vigezo gani vilivyotumika mpaka ikaamulika hivyo. Sasa watu wengi kwa kupenda uzinzi, kwavile binamu huwa wanaruhusiwa kuoana, basi inakuwa pia si tatizo kubwa sana kuzini, wanazini tu ingawa kwa kujificha na wengine hata wanapata watoto kama walivyo watoto wengi tu wanaoitwa wa haramu. Lakini si laana kulingana na utamaduni wao. Ila wanaheshimu sana na kutofanya mzaha wowote wa kimapenzi kati ya mtoto wa mama mdogo na mkubwa.
 
Hapo naona wazazi wa hao vijana wanampa mzigo Bibi katika kuwalea pamoja na kichanga chao hivyo wanamtesa bure bibi wa watu..

Labda wanaona alizembea kuona kuwa kunamahusiano yasiyofaa kwa wajukuu zake maana alikuwa nao yeye. Ila sidhani kama kosa ni lake pekee, muhimu ni kuwa walilelewaje huko ktk familia zao.
Pili wazazi tumezoea kuwaruhusu watoto kwenda tu ovyo kukaa kwa ndugu bila kujua adhari za kukaa pamoja watoto wenye malezi tofauti, na hii inakuwa na influence sana kwa sababu mtoto anashindwa kufuata maadili aliyofundishwa kwa kuona mbona hawa ni dada na kaka au ndugu zangu hawawezi kuniambia kitu kibaya.
Nakweli incest ni ngumu kudhibitiwa kutokana na kufichwa na wahusika, lakini kwenye jamii zinazotembeleana au extended family zinatokea sana.
 
 

Mkuu nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani kwamba sheria si kiti sana. Wanaoua alibino sheria zipo lakini wanasongambele kama kawaida. swala hapa ni maadili ya jamii na kumuogopa Mungu. Kama watoto wangelelewa katika maadili mazuri ya dini hawawezi kufanya ufirauni huo. Hata hao wazee wanaokula mabinti zao ukifuatilia sana utakuta tatizo ni hilohilo
 
KWanza tunatakiwa tujue walijuana katika mazingira gani ni nini? kilitokea mpaka wakajikuta wamefanya mapenzi.
mimi namjua dada na kaka ambao wameshea baba wameoana bila kujijua ndoa kanisani na wana mtoto , wamejua ukubwani na wanaendelea na ndoa yao.
Wenye kosa ni wazazi kutowatambulisha watoto tangu wadogo.
na wazazi hata kama una watoto wengi nje uhakikishe wamejuana wote tangu wadogo uwakusanye hi ndo itazuia kutakana na kutamanian.
 
nadhani na wazazi wao pia walaumiwe kwa hii,Tabia njema uanzia kwa wazazi
 
True, Psychiatric evaluation!!!
 
kweli kabisa, kuna makabila hapa bongo mabinamu ruksa kuoana (aka kufinyangana). wengine wanasema "binamu nyama ya hamu".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…