Malik Obama, kaka yake Barrack Obama, ameikashifu Kenya kwa anachokiita unafiki - Malik anadai kuwa, Kenya inatawaliwa na kabila moja, Kikuyu - Analinganisha hilo kwa kupewa jina barabara ya Forest jijini Nairobi kuwa Prof. Wangari Maathai - Pia amedai kuwa nyingi ya sekta nchini zina wasimamizi wengi kutoka jamii ya Wakikuyu
Kaka yake aliyekuwa Rais wa Marekani Barrack Obama, Malik Obama, ameichana Kenya na watu wake kwa anachokiita ni unafiki na kutawaliwa na jamii moja. Kwenye ujumbe wake wa Tweeter, Malik anadai kuwa, nchi inatawaliwa na kabila moja na kabila hilo ni jamii ya Wakikuyu.
Ametoa mfano wa barabara ya Forest jijini Nairobi ambayo ilipewa jina la Prof. Wangari Maathai kwa heshima ya Mshindi huyo wa Tuzo la Amani la Nobel mwendazake Wangari Maathai.
Malik Obama (Kulia) anasema Kenya inatawaliwa na kabila moja Picha: BBC
Maathai hadi kifo chake alikuwa mpiganiaji wa uhuru na mtu aliyejali sana hifadhi za mazingira. Kwenye ujumbe wake, Malik anaendelea kusema, sekta zote muhimu Kenya zinaongozwa na watu kutoka kabila la Wakikuyu. Hii ni pamoja na Fedha, kawi, miundombinu na usalama. Madai yake yanajiri huku joto la kisiasa nchini likiendelea kuwa lisiloelezeaka kufuatia chaguzi za Agosti 8 na Oktoba 26.
Malik ameichana Kenya kwa kuwa taifa lenye unafiki mkubwa Picha: BBC
Rais Uhuru Kenyatta alichaguliwa na kuapishwa huku Upinzani National Super Alliance (NASA) ukilalamika na kutangaza kutomtambua Rais. Kinara Mkuu wa NASA Raila Odinga ametaja kuwa, ataapishwa Desemba 12, 2017, wiki tatu baada ya Uhuru kuapishwa
Kenya inatawaliwa na kabila moja tu na sio vizuri, asema kakake Barack Obama | TANZANIA CLASSIC
Kaka yake aliyekuwa Rais wa Marekani Barrack Obama, Malik Obama, ameichana Kenya na watu wake kwa anachokiita ni unafiki na kutawaliwa na jamii moja. Kwenye ujumbe wake wa Tweeter, Malik anadai kuwa, nchi inatawaliwa na kabila moja na kabila hilo ni jamii ya Wakikuyu.
Ametoa mfano wa barabara ya Forest jijini Nairobi ambayo ilipewa jina la Prof. Wangari Maathai kwa heshima ya Mshindi huyo wa Tuzo la Amani la Nobel mwendazake Wangari Maathai.
Malik Obama (Kulia) anasema Kenya inatawaliwa na kabila moja Picha: BBC
Maathai hadi kifo chake alikuwa mpiganiaji wa uhuru na mtu aliyejali sana hifadhi za mazingira. Kwenye ujumbe wake, Malik anaendelea kusema, sekta zote muhimu Kenya zinaongozwa na watu kutoka kabila la Wakikuyu. Hii ni pamoja na Fedha, kawi, miundombinu na usalama. Madai yake yanajiri huku joto la kisiasa nchini likiendelea kuwa lisiloelezeaka kufuatia chaguzi za Agosti 8 na Oktoba 26.
Malik ameichana Kenya kwa kuwa taifa lenye unafiki mkubwa Picha: BBC
Rais Uhuru Kenyatta alichaguliwa na kuapishwa huku Upinzani National Super Alliance (NASA) ukilalamika na kutangaza kutomtambua Rais. Kinara Mkuu wa NASA Raila Odinga ametaja kuwa, ataapishwa Desemba 12, 2017, wiki tatu baada ya Uhuru kuapishwa
Kenya inatawaliwa na kabila moja tu na sio vizuri, asema kakake Barack Obama | TANZANIA CLASSIC