Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KALAMU YA IRVING WALLACE ''THE MAN'' INAPOGEUKA JINAMIZI
Huyu Irving Wallace alikuwa akiandika riwaya ambazo zina mengi ya ukweli kiasi unaweza ukachukua ''plot'' ya kitabu chake ukabandika katika matukio ya kweli.
Toka juzi Irving Wallace na kitabu chake, ''The Man,'' amekuwa akinitaabisha akili yangu na kunitoa raha.
Katika, ''The Man,'' serikali ya Marekani ghafa inajikuta inakabiliwa na kile walichokiona kuwa ni ''janga,'' pale Rais na Makamu wake wote wamekufa katika ajali.
Haraka inaangaliwa katiba inasemaje ikiwa Rais kafa nani anashika madaraka?
Makamu wa Rais.
Imetokea na Makamu wa Rais na yeye kafa vilevile?
Speaker of the House.
Na yeye katangulia mbele ya haki katika wakati huo huo wa wenzake?
President Pro Tempore of the Senate.
Huyo ndiye anaefuatia kushika nafasi ya urais.
Hapa Irving Wallace anaanza vurugu zake sasa usikiweke kitabu chini.
Huyu President Pro Tempore of the Senate ni Mtu Mweusi jina lake Douglas Dilman.
Rais wa United States Mtu Mweusi, Douglas Dilman!
Huyu Negro ndiye atutawale sisi Wazungu?
Haiwezekani hata kidogo.
Plot ya kitabu ni 1950s Mwamerika Mweusi si chochote.
Huyu Negro ndiye atawazwe kuwa Rais wa United States?
Wanajiuliza na wanatambua kuwa katiba ndivyo isemavyo na wao Watu Weupe ndiyo waliyoipitisha katiba hiyo wakiamini kuwa Mungu hawezi kuwaua hao wote kwa wakati mmoja.
Hata kama wakifa hizo nafasi zote zilikuwa mali na miliki ya Watu Weupe.
Huyu Mswahili atatokea wapi hadi ashike nafasi hiyo?
Huyu Irving Wallace kila kitabu chake kinamwambia mwenzake, sogea huko nipishe mimi.
Huyu Irving Wallace alikuwa akiandika riwaya ambazo zina mengi ya ukweli kiasi unaweza ukachukua ''plot'' ya kitabu chake ukabandika katika matukio ya kweli.
Toka juzi Irving Wallace na kitabu chake, ''The Man,'' amekuwa akinitaabisha akili yangu na kunitoa raha.
Katika, ''The Man,'' serikali ya Marekani ghafa inajikuta inakabiliwa na kile walichokiona kuwa ni ''janga,'' pale Rais na Makamu wake wote wamekufa katika ajali.
Haraka inaangaliwa katiba inasemaje ikiwa Rais kafa nani anashika madaraka?
Makamu wa Rais.
Imetokea na Makamu wa Rais na yeye kafa vilevile?
Speaker of the House.
Na yeye katangulia mbele ya haki katika wakati huo huo wa wenzake?
President Pro Tempore of the Senate.
Huyo ndiye anaefuatia kushika nafasi ya urais.
Hapa Irving Wallace anaanza vurugu zake sasa usikiweke kitabu chini.
Huyu President Pro Tempore of the Senate ni Mtu Mweusi jina lake Douglas Dilman.
Rais wa United States Mtu Mweusi, Douglas Dilman!
Huyu Negro ndiye atutawale sisi Wazungu?
Haiwezekani hata kidogo.
Plot ya kitabu ni 1950s Mwamerika Mweusi si chochote.
Huyu Negro ndiye atawazwe kuwa Rais wa United States?
Wanajiuliza na wanatambua kuwa katiba ndivyo isemavyo na wao Watu Weupe ndiyo waliyoipitisha katiba hiyo wakiamini kuwa Mungu hawezi kuwaua hao wote kwa wakati mmoja.
Hata kama wakifa hizo nafasi zote zilikuwa mali na miliki ya Watu Weupe.
Huyu Mswahili atatokea wapi hadi ashike nafasi hiyo?
Huyu Irving Wallace kila kitabu chake kinamwambia mwenzake, sogea huko nipishe mimi.