Kama $400,000 zinazalisha 400 megawat- Rusumo Falls , je kwanini Serikali inakubali kutumia $2.9bn kuzalisha 2100 megawatts?

Hujaelewa wala hujajibu swali,
Anauliza kwa nini megawati 80 zinazalishiwa kwa $400m ambayo ni gharama ya juu sana na megawati 2100 kwa $2.9b ambayo ni chini sana, pasipo kujali nani analipa kiasi gani katika kuchangia.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu,
Siyo kila kila mradi unaweza kufanyiwa ulinganifu wa moja kwa moja na mwingine was aina hiyo.
Vitu kama mazingira, siasa, mahitaji ya wakati huo, nguvu za asili n.k hubadilisha gharama kwa kiwango cha kushangaza.
 
Kama ndivyo hivyo kwa nini ujenzi wa Rusumo umekuwa ghali zaidi?
Ilipaswa uzalishaji wa Rusomo uwe wa bei ya chini ukilinganisha na Rufiji!
Mkuu umeme WA maji huzalishwa kutegemea na height ya hilo dam, sasa Rusumo height tayari ipo yaani ni maporomoko wakati Rufiji maporomoko yatatengenezwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Google or find a video from youtube on different type of costs na jinsi zinavyokadiriwa.

Mfano inawezekana 'fixed costs' za kutengeneza basin, au ule ukuta wa kuporomosha maji azipishani sana ata kama kuna tofauti za volumes of flow and water current kitu ambacho kitapelekea gharama za awali zisipashane sana. Tofauti ikaja kwa kuwa Stieglers flow of current ya maji na volume zinazokuja ni kubwa zinaweza zalisha zaidi kushinda huko kwingine.

Kwa kifupi maswali mengine kabla atujauliza kwa sie mambumbu wa mambo ya engineering na aina ya miradi iliyopo walau tupate akili za engineers kwanza (mawazo, yao) kabla ya kuanza kulazimisha mambo.

Lakini kuna watu wao kazi yao kupinga tu kila kitu.
 
Kikisio chako ni sawa kwa Rufiji,hicho ndicho kiasi serikali inasema itatumia kujenga hilo bwawa,kwa nini kwa Rusumo imekuwa bei ya juu sana tofauti na kikisio hicho?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanzisha thread kwanza anatakiwa kujua mass production ni cheaper kuliko uzalishaji mdogo.
Au mfano Mdogo alinganishe bei ya coaster vs number ya abiria inayo chukua Na gharama Za uendeshaji dhidi ya bei ya bus kubwa vs number ya abiria inayo chukuwa Na gharama Za uendeshaji. Halafu aende toilet kujisaidia akalale
 
Factors ni nyingi
Rusumo ni mali ya nchi 3,Stiglers gourge ni mali ya Tanzania tu.
Rusumo ni mkopo toka Word Bank,wakati Bwawa la Rufiji ni pesa za serikali.
Wakandarasi ni Tofauti.
Waliofanya mapatano ya mikataba ni watu tofauti
Arab Contractor ni kampuni ya serikali ya Misri,mkataba wao upo nafuu kuna siasa ndani tofauti na Rusumo.
Fidia ni sawa sawa na hakuna kwenye eneo la bwawa la Rufiji.Wakati Rusumo kuna maeneo yalihitaji fidia.
 
Life span ya hiyo miradi ikoje?
 
Mkuu umeme WA maji huzalishwa kutegemea na height ya hilo dam, sasa Rusumo height tayari ipo yaani ni maporomoko wakati Rufiji maporomoko yatatengenezwa
We umeshafika hapo Rusumo au unaongela tu

Sent using Damu ya Yesu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…