Kama bunge liliwahi kumwajibisha Waziri Mkuu kwa ufisadi wa Richmond kwanini lishindwe hawa waliotajwa na report ya CAG?

Sir robby

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2022
Posts
2,396
Reaction score
4,080
Wadau naamini Bado mnakumbuka SAKATA la RICHMOND lilivyomwondoa MADARAKANI aliyekuwa WAZIRI MKUU Mh.EDWARD LOWASSA kutokana na Tuhuma za Ufisadi wa Kampuni ya RICHMOND.

Juzi CAG Wakati anakabidhi Report yake kwa Mh.RAIS ametaja Madudu mengi yakionyesha UPOTEVU wa MABILIONI ya FEDHA za UMMA.

Ninaamini kama lile BUNGE liliweza Kuisimamia SERIKALI mpaka WAZIRI MKUU akajiuzulu pamoja na baadhi ya Mawaziri basi Tunataka na BUNGE hili liibane SERIKALI wahusika Wote waliotajwa na CAG WACHUKULIWE Hatua za KISHERIA ikuwa ni pamoja na Kushtakiwa na KURUDISHA FEDHA walizotuibia.

WATANZANIA tutalishangaa sana BUNGE kama LITASHINDWA kuwashughulikia Watendaji wote Waliotajwa na CAG.Baadhi ya MADUDU yaliyotajwa YANATIA KINYAA kuyasikia Utadhani NCHI haina VIONGOZI wala VYOMBO vya KUSIMAMIA Fedha za UMMA.


Soma

 
Sio bunge hili la wamama

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Again, the report raises audit queries, not proven corruption!

Nchi hii ina shida sana ya uelewa 😏

Kamati za bunge ndio zitachuja pumba na mchele, kisha maazimio yatapitishwa kuielekeza serikali ichukue hatua.

Kinyume ja hapo ni kuwaonea watu.
 
Shida CAG hajataja jina la mtu ni mpaka Uchunguzi ufanyike.
 
Tumekubaliana .hili nalo mawaziri wakalitazame
 
Mwigulu kasema pesa zote kubwa idhini ilitoka Kwa mkuu Wa nchi Sasa nani anapaswa kuwajibika
 
Watu bado hawajamuelewa Mwigulu Nchemba masikini...

Sasa sijui ni kwamba ni wajingaa!??
 
Upo sahihi, kuna watu hawajui taratibu za audit queries na zinavyo shughulikiwa.
Baadhi wanadhani ripoti ya CAG ndio alfa na Omega wakati si kweli, kwani tuhuma hutakiwa kujibiwa kabla hatua kuchukuliwa
 
Kamati za bunge ndio zenye jukumu la kufanya uchunguzi. Alichofanya CAG no kuonesha ubadhirifu na bunge Ienye kazi ya kumbainisha mbadhirifu. Kwa bunge hili la upande mmoja, lenye kujikomba komba, lenye vilaza wasiojua nini maana ya kuwa muwakilishi wa wananchi sidhani kama kutakalofanyika.
Ulishawahi kuona wapi duniani bunge linafanya kikao cha kumpongeza rais kutimiza majukumu yake? Ni Tanzania tu, hakika we are laughing stock in the world
 
Hakuna namna waongeze tozo kufidia upotevu, kumbuka hili ni bunge la chama kimoja na kanuni moja ya kutoumbuana.
 
Kwa aina ya watu waliopo Bungeni, unaamini wana uwezo wa kuchambua report ya CAG?
 
Lile lilikuwa Bunge, sasa hivi kuna kusanyiko la vilaza waliowekwa hapo na yule mwovu aliyeko motoni kwa ajili ya kumuandalia utawala usiokuwa na ukomo.

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Usilinganishe bunge la sitta na hili bunge la machawa. Hakuna kitu Hapo. Spika mwenyewe kadai Rais hana ulazima wa kusikiliza ushauri wa bunge.
 
Tangu lini wabunge haramu wakapinga ufisadi?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…