Kama demokrasia imerudishwa nchini, kulikoni ACT- Wazalendo kuzuiwa Maandamano?

Kama demokrasia imerudishwa nchini, kulikoni ACT- Wazalendo kuzuiwa Maandamano?

voicer

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2020
Posts
5,545
Reaction score
11,935
Kwamba Mheshimiwa Rais anapongezwa kwa kuifungua Demokrasia nchini. Lakini maandamano ya kupinga Ufisadi, Ubadhirifu na hujuma zilizotajwa na CAG yakipigwa marufuku?

Kwamba Serikali inayopinga ubadhirifu,ndio hiyohiyo inayozuia maandamano ya wananchi kuipongeza kwa kuyaibua hayo madudu kupitia ripoti ya CAG na kuyatangaza hadharani?

Hivi Demokrasia iliyofunguliwa ni ipi? Ya ushirikiano wa kulamba asali bila kupingana hadharani?

Ya kuitana kwenye tafrija na kujazana mapambio ya kusifiana?

Hivi ina maana mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, naye hajasikia kwamba maandamano ya ACT yamezuiwa na Polisi?

Na kama alisikia na kukaa kimya kwa jambo nyeti kama hilo,ni nini tafsiri yake?

Tukisema hakuna jipya ndani ya utawala huu,dhidi ya wafujaji wa mali za umma!

Bado mtaendelea kutuita Sukuma Gang?

Haya bhana, mi napita tu!

InCollage_20221210_215633674.jpg
 
Hii nchi ina wenge sana.

mamlaka zina unafiki mkubwa sana

hao porisi wanatumika kisiasa afu badae wanataka huruma ya wananchi na hyo serekali juu ya kuongezewa maslahi.

wanafika mbali na kulialia JF hao hao migambo walinda amani.

HAKUNA DEMOKRASIA HAPA, NI ASALI NA ULAMBAJI BASI
 
Hii nchi ina wenge sana.

mamlaka zina unafiki mkubwa sana

hao porisi wanatumika kisiasa afu badae wanataka huruma ya wananchi na hyo serekali juu ya kuongezewa maslahi.

wanafika mbali na kulialia JF hao hao migambo walinda amani.

HAKUNA DEMOKRASIA HAPA, NI ASALI NA ULAMBAJI BASI
Na mimi ninadhani unafiki unaanzia kule ofisi kuu kabisa!

Maana haiingii akilini kwamba Polisi walizuia,bila kuwa na maelekezo toka juu.
 
Kwamba Mheshimiwa Rais anapongezwa kwa kuifungua Demokrasia nchini. Lakini maandamano ya kupinga Ufisadi, Ubadhirifu na hujuma zilizotajwa na CAG yakipigwa marufuku?

Kwamba Serikali inayopinga ubadhirifu,ndio hiyohiyo inayozuia maandamano ya wananchi kuipongeza kwa kuyaibua hayo madudu kupitia ripoti ya CAG na kuyatangaza hadharani?

Hivi Demokrasia iliyofunguliwa ni ipi? Ya ushirikiano wa kulamba asali bila kupingana hadharani?

Ya kuitana kwenye tafrija na kujazana mapambio ya kusifiana?

Hivi ina maana mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, naye hajasikia kwamba maandamano ya ACT yamezuiwa na Polisi?

Na kama alisikia na kukaa kimya kwa jambo nyeti kama hilo,ni nini tafsiri yake?

Tukisema hakuna jipya ndani ya utawala huu,dhidi ya wafujaji wa mali za umma!

Bado mtaendelea kutuita Sukuma Gang?

Haya bhana, mi napita tu!

View attachment 2594790
NIlipowaambia uhuru bandia sikuwa nimekosea.

Tuendelee na drama
 
Ila yameleta nafuu nchini,jana spika kasema siku sita za majumuisho ndio wataijadili,mwanzo alisema mtu ajadili kivyake vyake lakini itajadiliwa bunge la November.

Hii ni dhahiri kuwa yale maandamano yakamfanya spika na katibu wa bunge kutafuta kifungu cha kusema siku sita za hili bunge.
 
Yazuiwe tu, wengine wata take advantage humo humo...
 
Back
Top Bottom