Elections 2010 Kama hali ndio hii, basi Dr. Slaa asubiri kuapishwa tu

Kimewakaaaaaaaaaa!!! Hadanganyiki mtu tena. Ila bado nawashangaa watu wengine. Mtu hata nyuma ya mabati huna unaishi kijijini. Hlserikali haijawahi kukuwezesha hata kidogo JK anakuja na kundi lake la kina michuzi wapo kwenye mahelikopta wewe unapanua limdomo lako unaimba NAMBAR WAI +Eeeeeeeeeee nambARI 1 ..PUMBAFU KABISA WEWE.HAINA AKILI WEWE KABISA , WW NI SAWA NA MFU...
Read my status please!!
 
Jamani hii kitu mwanzo nilidhani ni utani. Leo nimeongea na kaka yangu aliyekwenda kata moja ya Chabutwa. Alipofika pale alikuta jamaa mmoja amebandika picha kubwa sana ya Kikwete ukutani. Kaka yangu bila wasiwasi akaanza kumwambia jamaa juu ya UFISADI wa EPA na Richmond ulivyofanyika na kuwa hela za Richmond zilimnufaisha Lowassa na EPA ndiyo zilimuingiza Ikulu.

Walienda leo, ameshangaa kukuta jamaa AMELICHANA kabisa hilo picha na kuliondoa ukutani. Analaani saana kuwa alikuwa MJINGA kwa kiasi kikubwa namna ile. ANa hasira sana na CCM nzima ingawa kwa miaka kadhaa, baba yake alikuwa Mwenyekiti wa CCM.

Bahati mbaya saana Operation Sangara haikufika Sikonge na hata Uchaguzi huu Slaa hafiki Sikonge. Kama angelifika, ingelibadili saana mawazo ya watu. Tusiwadharau watu wa Vijijini maana kama wakiambiwa na mtu vizuri, wataelewa tu kuwa USANII Tanzania ni mwingi na kuwa wameibiwa sana na wataendelea kuibiwa saaana.

Hapa kijijini kwetu kwa sasa karibu kila sehemu kuna mavitabu, makaratasi na kila aina za takataka za Kikwete, CCM na Mbunge. Ila watu taratibu wameanza kufunguka macho. Nina imani hata kama Slaa atashindwa, basi atumie muda mwingi kutembelea wanachama vijijini ambako Chadema hawajaingia na kujenga zaidi Chadema huko kwenye Mashina.

Acha watumie hela nyingi ila sisi zetu ni kampeni za Kifamilia na kijirani zaidi. Tutaelimishana hadi kieleweke.
 
Tusibweteke kabisa! na hizi wiki tano zilizobaki bado kuna kazi kubwa mbele yetu ya kukiondoa chama filisi cha mafisadi madarakani. Hivyo inabidi kuhakikisha tunafanya kampeni za nguvu sana katika kila kona ya nchi yetu na kuhakikisha tunazilinda kura zetu ili kuhakikisha hakuna wizi wowote utakaofanywa na chama filisi cha mafisadi katika zoezi la kuhesabu kura.
 
Mimi kwetu ni karatu vijijini, ikubukwe mwaka 2005, watu wengi walimchagua Slaa kuwa mbunge wao lakini kwa Urais walimchagua Kikwete. Lakini juzi juzi nilienda huko vijijini nikiwa na nia ya kuwashawishi pia wale conservatives wabadili nia.
Cha kushangaza kabla mimi sijaanza kuwaeleza habari ya umuhimu wa kuchagua chadema, wao ndio walikuwa wa kwanza kunishawishi kwanza,

Ndipo nikajua kuwa sasa basi!
 


Kadri CCM wanavyozidi kupiga kampeni, ndivyo wanazidi kuipipigia debe kambi ya upinzani. Ndio, watu wanaenda kwenye mikutano ya kampeni ya CCM - KUWAZOMEA - lakini kwenye mikutano ya upinzani WANASHANGILI!

Hivi CCM haijagundua hili? Au sasa ndio wanafanya maandalizi ya kuchakachua kura, washinde kwa kishindo?
 
Nahisi kupona ugonjwa nisioujua very soon
Post of the year to me.
Nimetamani kucheka nikaanza kulia ghafla.

Mwaka huu chama changu CCM lazima kile makapi maana kimedanganya na kufanya madudu vya kutosha.
TUKIANGUSHE kwenye KURA
 

Huyo kausoma Mwongozo wa Kanisa vizuri. Teh teh teh!
 
ccm wachakachua jf presidential poll.wanavote 4vote per dk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…