Kama hauna mambo mengi, daka Mitsubishi i-MIEV electric car, hafu sahau gharama za mafuta!

Kama hauna mambo mengi, daka Mitsubishi i-MIEV electric car, hafu sahau gharama za mafuta!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Wadau wa JF Garage.

Kuna chuma, EV kutoka kampuni la Kijapan Mitsubishi inaenda kwa jina Mitsubishi i-MIEV (Mitsubishi innovative Electric Vehicle).
IMG_6639.jpeg

Hii unaweza kuipata BEforward kwa bei kati ya Mil 5 hadi 6 na kuendelea, na kodi zake (kwenye calculators ya TRA haipo) nimeulizia ni Tsh Mil 3.5 tu. Kwa makadirio bei jumla ni Mil 9-10.
IMG_6637.jpeg

Ni kagari flani kana design ya kipekee kama mitoko ya Madonna, na ukipita mahala lazima watu wageuze shingo. Ila muonekano ni subjective, kila mtu ana mapendeleo yake. Tuje kwenye specifications.
IMG_6636.jpeg

Kama tulivyosema ni EV yenye range ya 160 kilometa, kutoka kwenye battery ya 16kWh inayoisukuma motor yenye 47 kW (63hp). Ina port mbili za kuchaji, ya kawaida AC Level 1 ambayo inataka 15A na 110-240V unaweza chajia ata nyumbani na Fast charger DC.
IMG_6638.jpeg

Ni hatch yenye milango minne, design yake kidogo ina utata especially kwenye matair, ya mbele na nyuma hayafanani size, hii tuwaachie mainjinia wa Mitsubishi na badala ya spare tyre wanakupa compressor ya 12v utayoiplug kwenye cigarette lighter.

Maisha ni kujilipua.
 
Ogopa sana kumiliki kitu kipya cha kwanza nchini kwako,tena nchi zisizo na teknolojia ya kutosha kama hii yetu
Mi Niko tofauti hapo mkuu Huwa napenda vitu unique iwe ni innovation/version au brand MPYA
Nime experience mara nyingi Huwa ni konki!
Na wakiuza Huwa wanafungua mlango w information kwa watumiaJi wa kwanza kukosoa au kure commend

Vinginevyo toleo linalofuata Huwa ni quality refused make hapo ndo Huwa wanatafuta pesa yao irudi kwanza Huwa ni introduction na kutest market
 
Wadau wa JF Garage.

Kuna chuma, EV kutoka kampuni la Kijapan Mitsubishi inaenda kwa jina Mitsubishi i-MIEV (Mitsubishi innovative Electric Vehicle).
View attachment 3028060
Hii unaweza kuipata BEforward kwa bei kati ya Mil 5 hadi 6 na kuendelea, na kodi zake (kwenye calculators ya TRA haipo) nimeulizia ni Tsh Mil 3.5 tu. Kwa makadirio bei jumla ni Mil 9-10.
View attachment 3028061
Ni kagari flani kana design ya kipekee kama mitoko ya Madonna, na ukipita mahala lazima watu wageuze shingo. Ila muonekano ni subjective, kila mtu ana mapendeleo yake. Tuje kwenye specifications.
View attachment 3028062
Kama tulivyosema ni EV yenye range ya 160 kilometa, kutoka kwenye battery ya 16kWh inayoisukuma motor yenye 47 kW (63hp). Ina port mbili za kuchaji, ya kawaida AC Level 1 ambayo inataka 15A na 110-240V unaweza chajia ata nyumbani na Fast charger DC.
View attachment 3028063
Ni hatch yenye milango minne, design yake kidogo ina utata especially kwenye matair, ya mbele na nyuma hayafanani size, hii tuwaachie mainjinia wa Mitsubishi na badala ya spare tyre wanakupa compressor ya 12v utayoiplug kwenye cigarette lighter.

Maisha ni kujilipua.
Dr WA uchumi toka Iramba ataweka Kodi zaidi kwenye huo huo umeme unaochajia
 
Inatumia muda gani kuchaji kufikia full charge?

With full charge inatembea kilomita ngapi?
 
Juzi Kwa mara ya Kwanza nimeiona BYD pale kamata kwenye yard ya be forward alafu ilikuwa ni IT inaenda Congo....Kwa Tanzania tulivyokuwa waoga itachukua miaka mingi kumiliki gari za UMEME
 
Kucharge haya magari yanatumia Unit ngapi za umeme?.....
Swali zuri.

Ila itategemea na size ya battery (inayopimwa kwa kWh).

Mfano: gari kama Tesla lenye battery size ya 54 kWh, utatumia unit za umeme 54 kujaza kutoka 0-100% full charge.

Kwa bei ya leo June, unit izo ni kama Tsh 19,000/= (kwa unit 1 Tsh 357/=)

Kwa lugha nyingine iyo bei unapata mafuta petrol lita Lita 6 na nusu hivi.

Tukija kwenye range, Tesla ikiwa full charge itakupeleka 420 Km.

Mafuta Lita 6.5 yatatupeleka wapi? Kwa ku-assume gari letu lina consumption ya 20km/L (ambapo ni gari gani inafikia hapa, ata IST haifiki) inamaana tutafika 130 km tu.
 
Back
Top Bottom