Kama hii tweet ni kweli basi Air Tanzania ni ya kuhurumiwa

Wewe unafikiri biashara ni mteremka wa kupata kila siku? Haya kwenye biashara ni ya kawaida sana.
JIWE alishatangaza kuwa SERIKALI haipati HASARA.

- CHA MUHIMU NI SIFA TU KWA JIWE.

#ViWonder
 
Iko kazi. Ndege inayobeba zaidi ya watu 100 iende na watu 6. Biashara ya ndege ni changamoto kubwa.
 
Mm nliwahi kusafiri na basi toka dar hadi iringa tulikuwa abiria hatuzidi 20 kwenye basi la watu 60, so haya mambo ni ya kawaida kila kona.

Shida ya mleta mada yeye ni kuokoteza kila aina ya takataka na kuila
Ndege siyo kama basi. Inabidi walipie uwanja, mafuta, wahudumu, vyakula na usafi kwenye ndege ambavyo vinafanywa na viwanja wanakotua. Hesabu ni kiasi gani wanapoteza?
Tusiwe tunaongea kisiasa, tuongee kiuchumi. Kwenda Uganda kutoka Dar hailipi sababu wafanyabiashara wengi hawachukui mzigo kule na ujue hakuna shughuli zaidi na watu wenye uhusiano na uganda wapo kanda ya Ziwa. Wangetumia ndege ndogo ya kubeba abiria hata hamsini au less than that kama tunavyotumia Auric sababu ile haipati hasara.
 
Wasipoangalia hli shirika litarudi lilikotoka mapema sana..

Kiongozi wa hii nchi hana tofauti na baba anaechukua pesa na kwenda kununua suti na vitu vya dhamani ili tu washkaji zake wamuone anazo wakati nyumbani watoto wanashindia uji wa chumvi..ujinga ujinga tu!
 
Kwa sababu ya hiyo tweet?
Wewe mbona hujaelewa? Kwa sababu ya kuleta hasara kutokana na kutokuwa na business plan ya brand new long range aircraft (Greamliner) pamaja na raisi kujitahidi kuwanunulia hiyo ndege kwa cash maana mwanzoni walikuwa wanasingizia hawana ndege!!!!!!!!!!!! It is business time siyo muda wote ni wa porojo za kisiasa mkuu
 
Msihofu, siku hiyo nilikuwa nimekodi hiyo ndege kwenda Kampala, nikaruhusu abiria watano tu wapande.

Hili suala la kuanzisha route bila kutafakari demand au ushindani wa hiyo route niliongelea humu, watu wa Lumumba wakasema eti mie sio mzalendo. Hata hizi route za China na Mumbai nina wasiwasi nazo.

Nilisema wazi, ATC wasifikiri ni watanzania tu watapanda hizi ndege kwa kuwa ni wazalendo, na kwamba hata kama ni Watanzania sio wengi wa kutosha. Wasidhani abiria wengine watapanda hizi ndege kwa kuwa wanampenda Magufuli hata wakaacha kupanda ndege za mashirika ambayo wao ni wanachama wa frequent flyer programme

Nilipendekeza wajaribu mikakati ya kuvutia, promotion - eidha kushusha nauli sana (economy of scale) au ku-package nauli na kitu kingine, hasa mwanzoni mwa route - mfano fly to Entebe with Air Tanzania and stay one night free at Nile Hotel (Kampala). Hapo hata mie na my wife wangu tutaenda Kampala kutembea!

Kwa mfano route ya Kampala, hivi wameangalia nauli ya Dar -Kampala inatofautiana vipi na nauli ya KQ ya Dar-Nairobi-Kampala au Rwandair ya Dar-KIgali-Kampala? Hizi nauli hazipangwi kizalendo bwana, lazima zipangwe kimkakati. La sivyo ATCL watapata tabu sana na hizo ndege, na Magufuli is watching them, haelewi haambiliki!
 
Simpendi kabisa Magufuli mnafiki na katili anayejifanya mcha Mungu,natamani kuona akitoweka Duniani haraka hana faida kwa lolote lile hasara tupu
 
Hahaha makonda hawajazi ndege?! Inabidi ndege zingine zifukuzwe waipishe airtanzania.
 
Hii inaonesha jinsi wanavyojali wateja. Mashirika mengine huwa yanahairisha safar
 
Jamaa kila siku yeye ni kutafuta na kufurahia mapungufu tu.
Yapo mengi yanajionyesha menyewe wala sio ya kutafuta,,,by the way mbona husem wanavyo buy airtime daily kufanya show za uznduzi?.. Nyingi zikiwa na lengo LA kuchomekeaaa ya moyoni?.../
 
Mtu nina Gold yangu ya Emirate halafu niende kuanza moja kwenye ndege nisiyojua nitakula chakula gani au kupewa kinywaji gani? Mazoea yana tabu. Sipotezi Gold yangu bure.
 
Mtu nina Gold yangu ya Emirate halafu niende kuanza moja kwenye ndege nisiyojua nitakula chakula gani au kupewa kinywaji gani? Mazoea yana tabu. Sipotezi Gold yangu bure.
Haswaa! Halafu jiulize, hivi ukiwa stranded huko Mumbai kwa matatizo ambayo ni yao, ATC wana uwezo wa kukuweka hoteli kama airline zinavyofanya? Hoteli gani huko wanaijua ATC hadi wachukue abiria wao waliokwama? KIla hoteli itataka ATC walipe cash kwanza.Mwishowe abiria mtaombwa kwa ajili ya uzalendo na kumpenda Magufuli mjilipie hoteli hadi ndege itakapofanyiwa marekebisho! Kazi sasa kama wewe ni Mmalawi!
 
Sana sana wataomba ubalozi uwasaidie wawaweke kwenye guest za vichochoroni. Ukweli sijafika India ila nimekaa sehemu zote zinazoizunguka. Watu tumezoea kuweka 5 stars and 4 na kulala una kula ukikamua kulala Airport. Pale Dubai ukienda ile ya Gold, Silver na Platinum unamzidi aliyelala hotelini. Halafu uniambie haya ya kuletwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…