ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
My Take
Wanasiasa wa Afrika yote Wanafanana,ni Bora Kila mtu alipata nafasi achukue chake mapema badala ya kukaza na kujifanya Mzalendo.
Kwa Afrika hapa,Kuwa Mzalendo ni kuchagua umaskini na ujinga.
=====
Gayton McKenzie, mwanasiasa wa upinzani ambaye safari yake ya maisha yalizungukwa na matukio kadha wa kadha kuanzia kuwa jambazi sugu hadi mmiliki wa klabu ya burudani yenye utata, sasa ameteuliwa kuwa waziri wa michezo, sanaa na utamaduni wa Afrika Kusini.
Rais Cyril Rampahosa alimteua Bw McKenzie - kiongozi wa Muungano wa Patriotic (PA) - kwenye wadhifa katika serikali ya vyama vingi ambayo aliitangaza Jumapili baada ya chama chake cha African National Congress (ANC) kupoteza wingi wake wa wabunge katika uchaguzi wa Mei 29.
Mtumiaji huyo mahiri wa mtandao wa X, (zamani Twitter), mwenye umri wa miaka 50, alifurahia uteuzi wake, akituma picha yake akiwa amevaa viatu vya soka, kwa ucheshi, aliandika: "Asanteni kwa umbe wenu wa heri, nitajibu hivi karibuni. Niko mbioni kujiandaa, nina kazi ya kufanya 🥅 ⚽️."
Kwa wandani wa Bw McKenzie, uteuzi wake ni ishara ya hivi punde ya jinsi alivyoshinda dhiki ili kupata mafanikio. Aliiba benki mara ya kwanza kabla ya kufikisha umri wa miaka 16, kisha akawa jambazi kamili. Alisema hayo alipokuwa akihojiwa na kituo cha redio, alikaa gerezani kwa miaka saba, na akaapa kubadilika baada ya kuachiliwa.
"Ningeweza kuwa na randi 12 mfukoni mwangu lakini nilikuwa na randi bilioni moja akilini mwangu. Na hilo ndilo watu hawaelewi - wanazingatia kile wanachokosa badala ya jinsi ya kupata kile wanachokosa," alisema katika mahojiano ya 2013 na shirika la utangazaji la SABC.
Alikua mzungumzaji wa kutia motisha anayelipwa sana, akachapisha vitabu kuhusu maisha yake, ikiwa ni pamoja na A Hustler's Bible, na kujitosa katika biashara mbalimbali - kutoka uchimbaji madini nchini Zimbabwe hadi vilabu vya burudani nchini Afrika Kusini - akiwa na Kenny Kunene, mwandani wake kutoka gerezani.
Bw Kunene alijipatia jina la utani la "Sushi King" baada ya kuomba kuandaliwa mlo wa sushi kwenye miili ya wanawake wakiwa wamevalia nguo ya ndani pekee kwenye tafrija ya kutimiza miaka 40 ya kuzaliwa kwenye klabu ya usiku ya Zar Lounge, jijini Johannesburg.
BBC Swahili
Wanasiasa wa Afrika yote Wanafanana,ni Bora Kila mtu alipata nafasi achukue chake mapema badala ya kukaza na kujifanya Mzalendo.
Kwa Afrika hapa,Kuwa Mzalendo ni kuchagua umaskini na ujinga.
=====
Gayton McKenzie, mwanasiasa wa upinzani ambaye safari yake ya maisha yalizungukwa na matukio kadha wa kadha kuanzia kuwa jambazi sugu hadi mmiliki wa klabu ya burudani yenye utata, sasa ameteuliwa kuwa waziri wa michezo, sanaa na utamaduni wa Afrika Kusini.
Rais Cyril Rampahosa alimteua Bw McKenzie - kiongozi wa Muungano wa Patriotic (PA) - kwenye wadhifa katika serikali ya vyama vingi ambayo aliitangaza Jumapili baada ya chama chake cha African National Congress (ANC) kupoteza wingi wake wa wabunge katika uchaguzi wa Mei 29.
Mtumiaji huyo mahiri wa mtandao wa X, (zamani Twitter), mwenye umri wa miaka 50, alifurahia uteuzi wake, akituma picha yake akiwa amevaa viatu vya soka, kwa ucheshi, aliandika: "Asanteni kwa umbe wenu wa heri, nitajibu hivi karibuni. Niko mbioni kujiandaa, nina kazi ya kufanya 🥅 ⚽️."
Kwa wandani wa Bw McKenzie, uteuzi wake ni ishara ya hivi punde ya jinsi alivyoshinda dhiki ili kupata mafanikio. Aliiba benki mara ya kwanza kabla ya kufikisha umri wa miaka 16, kisha akawa jambazi kamili. Alisema hayo alipokuwa akihojiwa na kituo cha redio, alikaa gerezani kwa miaka saba, na akaapa kubadilika baada ya kuachiliwa.
"Ningeweza kuwa na randi 12 mfukoni mwangu lakini nilikuwa na randi bilioni moja akilini mwangu. Na hilo ndilo watu hawaelewi - wanazingatia kile wanachokosa badala ya jinsi ya kupata kile wanachokosa," alisema katika mahojiano ya 2013 na shirika la utangazaji la SABC.
Alikua mzungumzaji wa kutia motisha anayelipwa sana, akachapisha vitabu kuhusu maisha yake, ikiwa ni pamoja na A Hustler's Bible, na kujitosa katika biashara mbalimbali - kutoka uchimbaji madini nchini Zimbabwe hadi vilabu vya burudani nchini Afrika Kusini - akiwa na Kenny Kunene, mwandani wake kutoka gerezani.
Bw Kunene alijipatia jina la utani la "Sushi King" baada ya kuomba kuandaliwa mlo wa sushi kwenye miili ya wanawake wakiwa wamevalia nguo ya ndani pekee kwenye tafrija ya kutimiza miaka 40 ya kuzaliwa kwenye klabu ya usiku ya Zar Lounge, jijini Johannesburg.
BBC Swahili