Kama kipengele cha kuwabeba polisi kingepitishwa kada zingine nasi tungefanya yetu

Kama kipengele cha kuwabeba polisi kingepitishwa kada zingine nasi tungefanya yetu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Kwanza niipongeze serikali Kwa kufuta huo mswada wa kutaka kuwabeba polisi ati wasishtakiwe wakiwa kwenye majukumu Yao.
Ingekuwa muswada wa hovyo kuwahi kutokea.

Sisi waalimu nasi tungepeleka muswada bungeni kuwa tusishtakiwe tuwapo kwenye majukumu yetu, tukiwapa adhabu wanafunzi, Kama mnavyojua waalimu Kama Mimi tunapiga bakora mpaka mtoto anazimia Kama sio kufa Kabisa. Ni vile sheria zinatuzuia kufanya hivyo.

Hasira za mishahara kidunchu tungezihamishia Kwa watoto, hasira za kutopandishiwa mishahara na madaraja tungezihamishia kwenye michongo na matako ya wanafunzi. Ni bahati tuu sheria zinatukataza.

sisi madaktari nasi tungepeleka muswada kuwa tusishtakiwe iwapo itatokea uzembe WA bahati mbaya au Makusudi tunapowahudumia wagonjwa. Mbona watoto wenye utindio wa ubongo wangeongezeka nakuambia, hakuna cha uzembe wala nini, tungefanya kusudi kabisa.

sisi tume ya uchaguzi tungeiomba serikali ituwekee sheria zitakazotulinda katika majukumu yetu, hatutaki kushtakiwa, hata Kama tukimpa ushindi asiyemshindi,

Kada zingine nazo zingedai sheria zakuwalinda wawapo katika majukumu Yao hata kama wamefanya uhalifu wa makusudi kabisa.

Na mwisho tungekuwa na taifa la kulindana.

Natamani hata kina Spika, Rais na wengineo ambao wanakinga ziondolewe ili wote tuwe Sawa chini ya sheria.

Tupendane!
 
Kumbe haya mambo ya kuwekeana kinga bado yanaendelea, kwamba polisi sasa wajifanyie wanavyotaka ikiwemo kuua kwa makusudi kama kule Mtwara na wasishtakiwe? Aisee nchi ya danganyika imeshakuwa ngumu hii.
 
Kumbe haya mambo ya kuwekeana kinga bado yanaendelea, kwamba polisi sasa wajifanyie wanavyotaka ikiwemo kuua kwa makusudi kama kule Mtwara na wasishtakiwe? aisee nchi ya danganyika imeshakuwa ngumu hii.
Wapo Kwenye majukumu yao
 
Mtoa hoja kumbe wewe ni mwalimu!wewe pia ni sehemu ya tatizo nchi yetu imejikuta imo,wewe ndiye unayebeba kura haramu,unayehesabu kura haramu and i got no sympathy with teachers hapa nchini;mnapiga kelele muda huu come elections time mnalambishwa pipi na kusahau kila kitu, vipi shemeji (President JK)aliwalipa malimbikizo yenu?,na for your informations a SMART teacher hatumiii kabisa corporal punishments!(hii adhabu na mengineyo ndio iliyosabisha principal wa Mkwawa CNE afe na alikufa kifo kibaya na hopes anaungua hadi leo,sometime kwenye maisha haya tunakua pushed to far na washenzi fulani).
 
Sheria za namna hii zilikuwa zikipendwa sana na yule hayati wa Chato
 
Mtoa hoja kumbe wewe ni mwalimu!wewe pia ni sehemu ya tatizo nchi yetu imejikuta imo,wewe ndiye unayebeba kura haramu,unayehesabu kura haramu and i got no sympathy with teachers hapa nchini;mnapiga kelele muda huu come elections time mnalambishwa pipi na kusahau kila kitu,vipi shemeji (President JK)aliwalipa malimbikizo yenu?,na for your informations a SMART teacher hatumiii kabisa corporal punishments!(hii adhabu na mengineyo ndio iliyosabisha principal wa Mkwawa CNE afe na alikufa kifo kibaya na hopes anaungua hadi leo,sometime kwenye maisha haya tunakua pushed to far na washenzi fulani).

Tunawapigia Kura waliotupatia Uhuru wa bendera, siku wakija watakaotupigania uhuru wa kiuchumi tutawapa nao Kura.

Sio mtupe maneno matupu
 
Napendekeza aliyehusika kuandaa hicho kipengele awajibishwe. Ilikuwa ni matusi kwenye akili za watanzania.
 
Back
Top Bottom