Kama Kiswahili ndio lugha ya Taifa, Serikali ihakikishe kinatumika katika nyanja zote muhimu ikiwemo Elimu

Kama Kiswahili ndio lugha ya Taifa, Serikali ihakikishe kinatumika katika nyanja zote muhimu ikiwemo Elimu

Joined
Dec 26, 2021
Posts
33
Reaction score
23
Kiswahili na Kiingereza, ni lugha mbili ambazo zipo kwenye mitaala ya elimu yetu nchini, lakini asilimia zaidi ya 80 ya watanzania hawajui lugha zote mbili Kwa ufasaha.

Au hata lugha Moja tu kwa ufasaha na usahihi.

Ni kwa sababu ya uwepo wa lugha mbili ambazo, hupokezana na huingiliana kwenye mitaala ya elimu.

Shule ya msingi utatumia Kiswahili, Secondary na chuo utatumia Kiingereza.

Kama tumeweza kutumia lugha ya kiswahili, kwenye elimu ya shule ya msingi tumeshindwa nini ngazi ya sekondari na chuo?

Mtanzania akiwa na wazo, hawezi kulipeleka katika lugha ya kiswahili na kiingereza pia, ni kwa sababu hazijui lugha zote Kwa ufasaha.

Mkanganyiko huu wa Lugha ni moja wa kikwazo, Cha maendeleo ya uchumi wa taifa letu.

Lugha yetu ya taifa, ni kiswahili. Lakini Kiswahili hakifanywi vile ambavyo inabidi ifanywe lugha ya taifa iwe.

Serikali imeshindwa kuzuia swala Hilo na kama sio kuzuia, basi imeshindwa kuzipatia kipaumbele lugha zote mbili kwa wakati mmoja.

Kama serikali imeifanya kiswahili kuwa lugha ya taifa, basi inabidi ihakikishe yafuatayo.

1. Kiswahili kitumike ngazi zote za Elimu za elimu nchini Chekechea Hadi ngazi ya chuo kikuu, na kusiwe na Muingiliano wa lugha ya kiingereza.

2. Serikali ihakikishe matumizi ya lugha ya kiswahili kwa ufasaha, lugha ya kiswahili itumike kwa upana katika kutekeleza majukumu yake.
Leo unakuta tangazo la au nyaraka ya serikali Kwa kiingereza. Serikali imeshindwa kuwa mfano Kwa wananchi wake katika matumizi ya lugha ya kiswahili.

3.Bila ubabaishaji serikali ikazanie lugha ya kiswahili, iwe lazima kujifunza Kwa Kila mgheni ajae nchini.

4.Mitandao ya kijamii, vyombo vya habari na vifaa vya mawasiliano, vyote Kwa ulazima wa kisheria vitumie lugha ya kiswahili TU.

Pili kama serikali imeamua lugha zote mbili zitumike, basi inabidi ihakikishe haya.

1: Lugha zote mbili zipewe kipaumbele kuanzia ngazi ya utoaji elimu, jamii na hadi serikalini.

Na kiujumla serikali imeshindwa kupanua na kutengeneza fursa za ajira kupitia Kiswahili.

Kupitia balozi zetu zilizopo mataifa mbali mbali duniani, serikali ingeweza kuandaa programu za kufundisha kiswahili, walimu wangeajiriwa watanzania.

Viongozi katika serikali zetu, wanashindwa kuwa innovative na creative, wamakalia kutuahidi haki zetu au majukumu ya serikali.

Ahadi za kampeni ni nitajenga Barbara, nitajenga shule kiundani hayo ni majukumu ambayo serikali imeshindwa kutekeleza.

Ni ngumu kusikia ahadi za ubunifu, ambazo zitamkwamua mtanzania.

Viongozi wangeweza kubuni programu ya kukuza lugha ya kiswahili na kuifundisha, wapo watu wengi wanataka kujifunza kiswahili hawajui wapi pa kuanzia.

Kama tumeamua tuwe taifa la lugha malaya, yani tuwe na lugha mbili basi zote zipewe kipaumbele.

Mtanzania ashindwe akatae yeye kujifunza lugha zote mbili, Kwa Sasa serikali ndio imeshindwa kumjengea mazingira ya kujifunza lugha zote mbili.
 
Mara mitahara mara elimi mara kiswahili ( ufasaha ni Kiswahili). Hakika mtoa mada umethibitisha wewe ni mmojawapo wa Watanzania ambao hamna uelewa wa lugha zote mbili za Kiswahili na Kiingereza.

Kujitenga na Kiingereza ni ujinga wa hali ya juu. Hatutakiwi kukiacha bali tatizo hatuna Waalimu na miundombinu mizuri ( mitaala, vifaa, vitabu ) katika ufundishaji wa Lugha ya Kiingereza.

Ningekuwa wewe ningeshauri maboresho zaidi katika sifa za Waalimu wanaofundisha Kiingereza tangu Shule za Msingi, pili kuhakikisha kunapatikana vitabu vya kutosha kwa Waalimu na Wanafunzi katika ngazi zote za elimu inakofundishwa lugha hiyo lakini tatu approaches ( mbinu) za ufundishaji ambazo ziwe zinahamasisha ( zina encourage) kuongea badala ya mitihani ya kuandika pekee.

Tukiwa na madarasa ambayo mwanafunzi atalazimika kuongea mara kwa mara yatajenga kujiamini na kuongeza uwezo wa kuandika, kusoma na kuongea Kiingereza kwa ufasaha
 
Lugha ya kiswahili ni lugha ya KIMASIKINI.
Dunia ya Sasa bila kiingereza ni wazi utapata tabu sana huu ndo ukweli mchungu
 
Ajabu hata Kiswahili chenyewe hukijui. Eti mitahara! Neno sahihi ni mitaala.
Ni kweli sikijui Kwa maana nimeandaliwa kwenye mfumo wa elimu wa lugha mbili, sijui kuandika Kwa kiswahili najua kuandika Kwa kiingereza.

Nilikuwa namaanisha Syllabus, hapo umenielewa?
 
Kiswahili ni lugha ya kufundishia shule za msingi lakini wengi wenye kipato na wasomi na wenye madaraka hawasomeshi watoto wao huko.

Wanaoanzisha shule binafsi wanatumia kiingereza kama lugha ya kufundishia.

Hata watanzania maskini wangependa watoto wao wasome kwa kiingereza.

Serikali ilazimeshe watu? Huoni kwamba watu wanataka kiingereza na sio serikali pekee?

Hata ikipitishwa sheria bado watu watawahamishia watoto wao nchi jirani kwenye hicho kiingereza.
Tusiilaumu serikali.
 
Kijifunza kiswahili kama lugha ya taaluma ni kuukaribisha umaskini ndani mwako.
 
Lugha ya kiswahili ni lugha ya KIMASIKINI.
Dunia ya Sasa bila kiingereza ni wazi utapata tabu sana huu ndo ukweli mchungu
umesema kweli kabisa, ila wazee wanataka eti watoto wa leo wajifunze kiswahili sijui wana nia gani?
 
Kiswahili tungekiacha cha kuongelea nyumbani ,shuleni tutumie kizungu
 
Lugha bila kuwa na elimu yako na teknolojia yako utafika.mbali utakuwa kituko tu

Utatafsri History. Kuwa historia,Geography unatafsiri jiografia,physics utatafsiri fizikia,Engineer utatafsiri injinia nk

Vizuri uachie tu watu wasome kwa kingereza tu
.Nilishashauri humu kuwa shule zote ziwe English medium tu

Walimu wa English medium schools mbona wamesoma Vyuo vyetu hivi hivi vyetu vya ualimu
 
Kiswahili kitumike nyanja zote isipokuwa kwenye Science and Technology tutumie English
 
Aliyeandika mitahara sio mimi lakini,Mimi nimemnukuu tu ila naona karekebisha tayari.
Aliyeandika mitahara sio mimi lakini,Mimi nimemnukuu tu ila naona karekebisha tayari.
Chamakh amechangia vizuri sana hii hoja. Kwa ufupi amesema:

a) Sifa za waalimu wanaofundisha Kiingereza ziboreshwe

b) Pawepo na vitabu vya kutosha kwa waalimu na wanafunzi

c) Mbinu za kufundisha Kiingereza zijumuishe kuhamasisha wanafunzi kuongea Kiingereza

Mfano hai ni mimi mwenyewe. Nimeanza shule 1959 kijijini na tukaanza kufundishwa Kiingereza darasa la 3 mwka 1961 (wakati tunapata uhuru). Nilipomaliza darasa la 4 1962 nikafanya mtihani na kuchaguliwa kwenda darasa la 5 shule nyingine (Full Primary School) kwa kuwa shule ya awali ilikuwa inaishia darasa la 4 (Lower Primary School).

Lugha ya kufundishia iliendelea kuwa Kiswahili. Tulipoingia darasa la 7 mwaka 1965 lugha ya kufundishia ikageuka kuwa Kiingereza hadi tulipoaliza darasa la 8 mwaka 1966. Wakati tunaanza kutumia Kiingereza kama lugha ya kujifunza tayari tulikuwa tumepata uelewa wa kutosha wa kuweza kuongea na kunadika Kiingereza kwa ufasaha.

Hii iliwezekana kutokana na sababu alizoziainisha Chamakh. Kwa mfano hatukuruhusiwa kuongea lugha yoyote isipokuwa Kiingereza kwa muda wote tunapokuwa shuleni. Hii ilitujengea kujiamini kwa kuwa wakati huo hata tulikuwa tunafanya midahalo kwa Kiingereza. Pia tulikuwa na vitabu vya kutosha vya hadithi ambavyo tulihimizwa kuvisoma.

Ajabu ni kwamba waalimu wetu ambao walikuwa na uwezo wa kufundisha Kiingereza vizuri hakuna hata mmoja ambaye alikwa na elimu ya sekondari. Wote walikuwa wamemaliza darasa la 8 halafu wakaenda mafunzo ya ualimu. Kwa hiyo tulipoingia sekondari mwaka 1967 hatukuwa na tatizo la lugha kama walilo nalo vijana wa sasa.

Tuliendela vizuri hadi chuo kikuu. Je ni wapi tulipojikwaa? Jibu ni kwamba ilifika wakati tukapuuza kuzingatia vigezo alivyovitoa Chamakh. Rai yangu siku zote kuhusu mjadala huu ni kwamba sisi kama taifa la Tanzania tunaweza kuamua kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia SI kwa sababu vijana wetu wetu wanashindwa kuelewa Kiingereza lakini kwa sababu lugha ya Kiswahili inajitosheleza kufundishia lakini wakati huo huo vijana wetu wakiwa na uwezo wa kujifunza na kuelewa lugha zingine za kigeni kama ilivyo katika nchi kadhaa.
 
Kiswahili na Kiingereza, ni lugha mbili ambazo zipo kwenye mitaala ya elimu yetu nchini, lakini asilimia zaidi ya 80 ya watanzania hawajui lugha zote mbili Kwa ufasaha.

Au hata lugha Moja tu kwa ufasaha na usahihi.

Ni kwa sababu ya uwepo wa lugha mbili ambazo, hupokezana na huingiliana kwenye mitaala ya elimu.

Shule ya msingi utatumia Kiswahili, Secondary na chuo utatumia Kiingereza.

Kama tumeweza kutumia lugha ya kiswahili, kwenye elimu ya shule ya msingi tumeshindwa nini ngazi ya sekondari na chuo?

Mtanzania akiwa na wazo, hawezi kulipeleka katika lugha ya kiswahili na kiingereza pia, ni kwa sababu hazijui lugha zote Kwa ufasaha.

Mkanganyiko huu wa Lugha ni moja wa kikwazo, Cha maendeleo ya uchumi wa taifa letu.

Lugha yetu ya taifa, ni kiswahili. Lakini Kiswahili hakifanywi vile ambavyo inabidi ifanywe lugha ya taifa iwe.

Serikali imeshindwa kuzuia swala Hilo na kama sio kuzuia, basi imeshindwa kuzipatia kipaumbele lugha zote mbili kwa wakati mmoja.

Kama serikali imeifanya kiswahili kuwa lugha ya taifa, basi inabidi ihakikishe yafuatayo.

1. Kiswahili kitumike ngazi zote za Elimu za elimu nchini Chekechea Hadi ngazi ya chuo kikuu, na kusiwe na Muingiliano wa lugha ya kiingereza.

2. Serikali ihakikishe matumizi ya lugha ya kiswahili kwa ufasaha, lugha ya kiswahili itumike kwa upana katika kutekeleza majukumu yake.
Leo unakuta tangazo la au nyaraka ya serikali Kwa kiingereza. Serikali imeshindwa kuwa mfano Kwa wananchi wake katika matumizi ya lugha ya kiswahili.

3.Bila ubabaishaji serikali ikazanie lugha ya kiswahili, iwe lazima kujifunza Kwa Kila mgheni ajae nchini.

4.Mitandao ya kijamii, vyombo vya habari na vifaa vya mawasiliano, vyote Kwa ulazima wa kisheria vitumie lugha ya kiswahili TU.

Pili kama serikali imeamua lugha zote mbili zitumike, basi inabidi ihakikishe haya.

1: Lugha zote mbili zipewe kipaumbele kuanzia ngazi ya utoaji elimu, jamii na hadi serikalini.

Na kiujumla serikali imeshindwa kupanua na kutengeneza fursa za ajira kupitia Kiswahili.

Kupitia balozi zetu zilizopo mataifa mbali mbali duniani, serikali ingeweza kuandaa programu za kufundisha kiswahili, walimu wangeajiriwa watanzania.

Viongozi katika serikali zetu, wanashindwa kuwa innovative na creative, wamakalia kutuahidi haki zetu au majukumu ya serikali.

Ahadi za kampeni ni nitajenga Barbara, nitajenga shule kiundani hayo ni majukumu ambayo serikali imeshindwa kutekeleza.

Ni ngumu kusikia ahadi za ubunifu, ambazo zitamkwamua mtanzania.

Viongozi wangeweza kubuni programu ya kukuza lugha ya kiswahili na kuifundisha, wapo watu wengi wanataka kujifunza kiswahili hawajui wapi pa kuanzia.

Kama tumeamua tuwe taifa la lugha malaya, yani tuwe na lugha mbili basi zote zipewe kipaumbele.

Mtanzania ashindwe akatae yeye kujifunza lugha zote mbili, Kwa Sasa serikali ndio imeshindwa kumjengea mazingira ya kujifunza lugha zote mbili.
Zaidi ya lugha 2,000 huzungumzwa barani Afrika, Kiingereza ikiwa miongoni mwa lugha hizi na kuzungumzwa katika mataifa 25 ya Afrika
Orodha imetolewa ya nchi zinazomumunya Kiingereza kwa ustadi, Kenya ikioshwa na mataifa kadhaa ikiwemo Uganda na Nigeria
Je, Kenya inashikilia nafasi ya ngapi katika kutafuna Kiingereza Afrika? Na ni nani nambari moja? Soma upate uhondo
Zaidi ya lugha elfu mbili huzungumzwa barani Afrika; ukuaji wa lugha na utofauti ukichangia katika kuimarisha mazungumzo miongoni mwa raia wa mataifa mbalimbali ya Bara Afrika.

Orodha ya Mataifa Kumi Bora Yanayotafuna Kiingereza Kizuri Barani Afrika, Uganda Nambari Moja
Uganda ndilo taifa linaloongoza kwa kutafuna Kiingereza kizuri barani Afrika.
Ijapokuwa lugha nyingi hutumika katika mafunzo ya shule ya msingi Afrika, kuna mataifa 25 kati ya 54 ambako lugha ya Kiingereza inatumika kwa masuala rasmi na kibiashara.

Mataifa mengi yanayotumia Kiingereza ni zile zilikuwa chini ya wakoloni kutoka Uingereza isipokuwa Rwanda na Eritrea.

Hii hapa ni orodha ya mataifa kumi bora katika kuzungumza Mataifa 10 Afrika yanayokeketa Kiingereza bora kwa mujibu wa shirika la utafiti la CCJK.

10. Rwanda
Ni moja kati ya mataifa madogo zaidi barani Afrika ikiwa na idadi ya watu milioni 13 na asilimia 0.2 pekee ndio inayozungumza Kiingereza. Kinyarwanda ndiyo lugha inazungumzwa kwa sana na vilevile ni lugha ya taifa.

9. Ghana
Taifa hili la Magharibi mwa Afrika linachukua nafasi ya 9 kwenye orodha hii. Ghana hutumia Kiingereza kama lugha rasmi ya taifa. Ghana ina takriban lugha zingine 11.

8. Malawi
Malawi ina idadi ya watu milioni 19 na licha ya kuwa Kiingereza ndiyo lugha rasmi ni asilimia 26 pekee ya raia wake wanaotumia lugha hii. Chichewa ndiyo lugha ya taifa na asimilia 57 huzungumza lugha hii.

7. Zimbabwe
Ikiwa na idadi ya watu milioni 14.8, nchi hii inashikilia nafasi ya saba katika orodha ya mataifa yanayozungumza Kiingereza kizuri.

6. Botswana
Taifa jingine ambalo halina ufuo wa bahari, likipatikana kusini kwa Afrika. Kiingereza ndiyo lugha rasmi licha ya nchi hii kuwa na watu wengi wanaozungumza lugha ya Setswana.

5. Zambia
Zambia ina zaidi ya lugha na lahaja 70. Hata hivyo, Kiingereza ndiyo lugha rasmi kwa biashara na masuala mengine.

4. Kenya
Taifa hili la Afrika Mashariki limeorodheshwa la nne katika ubora wa kumumunya Kiingereza. Kenya ni nyumba kwa makabila mbalimbali yanayozungumz alugha zao lakini lugha rasmi ni Kiingereza.
3.Nigeria ni taifa la tatu Afrika katika kuzungumza Kiingereza kizuri. Taifa hili lina watu milioni 206 na kati yao, milioni 79 wanapiga Kiingereza.

2. Afrika Kusini
Afrika Kusini inashikilia nafasi ya pili kwenye ubora ikiwa na raia milioni 4.8 wanaozungumza Kiingereza kama lugha yao ya kwanza.
1. Uganda inachukua nafasi ya kwanza kwenye orodha ya mataifa ya Afrika yanayozungumza Kiingereza kizuri. Nchi hii imetumia Kiingereza kama lugha ya taifa tangu kupata uhuru miaka ya sitini.
 
Back
Top Bottom