Kama kuna anaemtaka huyu mwanamke amchukue jamani

Kama kuna anaemtaka huyu mwanamke amchukue jamani

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Nilitembelea nchi ya Botswana miaka ya 2008, nilikutana na jumuia ya wa-Tanzania na kama mnavyojua tukikutana nje ya nyumbani ukute mtu anaongea Kiswahili mnajiona kama mmetoka familia moja.

Jumamamosi moja kama hii kuna kaka wa ki-Tanzania alifanya barbecue na kutualika wabongo wenzake. Mmoja katika walikuwa alikuja na mtoto wa ki-Tswana, tulicheza enzi hizo mac mugs wa king Kiba na nyota yako ya TID pamoja na nakshi nakshi mrembo.

Katikati ya raha yule aliyekuja na mtoto wa ki-Tswana rafiki zake walimstua mbona hapokei simu wakati mke wake alikuwa njiani akirudi kutoka mapumzikoni bongo?

Pombe zote zilimwisha yule kaka akaanza kumnadi mtoto wa watua, kama kuna anaemtaka Huyu mwanamke amchukue Mimi ninaondoka.

Nilijifunza huku kutoka na foreigner huku, unanadiwa pasi kufahamu.
 
Ngoja na mimi nianze uchokozi wa kushika nafasi za watu. Ila kunadiwa ni moja ya matunda ya uzinzi na kupenda sana bata wenye matope.
 
dedicate rara ya tekno

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Back
Top Bottom