Kama kwa haya tunayoyaona Rais Magufuli mbali na taratibu, pia anavunja katiba waziwazi vipi kwa tusiyoruhusiwa kuona

Kama kwa haya tunayoyaona Rais Magufuli mbali na taratibu, pia anavunja katiba waziwazi vipi kwa tusiyoruhusiwa kuona

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Kwa haya machache tunayoyaona, Rais wetu anavunja taratibu na kanuni waziwazi, vipi kwa tusiyoruhusiwa kuona? Tutazame haya machache:

1. Nafasi 10 alizopewa kuteua wabunge alivunja katiba tukapiga kelele mmoja akajiuzulu kisha kupewa ubalozi. Hata hivyo kujiuzulu kwa huyo mmoja hakukumoondolea hadhi ya kulipwa mafao kama mbunge.

2. Uteuzi wa Jaji mkuu alienda kinyume cha taratibu za kimahakama, akateua kaimu Jaji mkuu. Sijuia alikuwa anataka atimiziwe kwanza matakwa yapi ndipo amthibitishe? Nadhani alifanikiwa. Sasa tunaona hukumu zikiamuliwa na DPP lakini kwa kivuli cha Rais.

3. Kwenye uteuzi wa CAG mpya amevunja tena katiba waziwazi na hata hivyo ameshindwa kabisa kutafsiri neno "Shall" kisheria ambalo limo kama muongozo wa utendaji wa CAG katika kanuni zinazoongoza ofisi hiyo. Hata hivyo tunamkumbusha Rais aelewe kuwa kanuni zinazoongoza ofisi yoyote ile ya umma zimetokana na muongozo mama sheria iliyopitishwa na bunge kwa kuzingatia katiba. Kanuni hazijawahi kuwa juu ya katiba hata siku moja.

4. Kwenye manunuzi makubwa na utekelezaji wa miradi mbali mbali mikubwa ame by-pass muongozo wa bunge na ndiyo maana havikaguliwi. Huu ni ufisadi wa aina yake.

Tunamkumbusha Rais kuwa aliapa kuilinda katiba. Hakuzungumza tu pale uwanja wa Uhuru, aliapa!
 
Kibaya zaidi hakuna wa kumzuia kikatiba, si ndani ya chama chake ama serikalini. Kote amepata utiifu uliopitiliza kutokana na hofu na woga juu tabia, hulka na aina ya uongozi wake. Hakuna tena wa kujaribu kumfunga paka kengere.

Wazee wastaafu walitafuta upenyo wa kuja na waraka, lkn wazee wenzao ambao ilikuwa ni kete muhimu kwa mustakabali wa taifa letu waliwakana mchana kweupe. Only "wishes" sasa ipo kupitia jitahada za Mh. Membe, endapo 'those wishes will mature and live up" ndipo ambapo utakapo tambua unafiki uliopo ndani ya CCM.
 
Wananchi wanataka maendeleo na ujenzi wa nchi.
Ikiwemo hiyo miradi tekelezwa,mlitaka iletwe bungeni ili muipinge na kutucheleweshea maendeleo?

Wananchi hawali wala demokrasia sio hitaji lao la msingi,bali hili ni lenu wanasiasa maana huko mdio shambani kwenu.

Mtapiga zomali sana lakini mwisho wa siku wananci tunawaona na tutawaadhibu kwenye debe la kura 2020.
#Tuko na JPM 2020[emoji1241][emoji818]
 
Wananchi wanataka maendeleo na ujenzi wa nchi.
Ikiwemo hiyo miradi tekelezwa,mlitaka iletwe bungeni ili muipinge na kutucheleweshea maendeleo?

Wananchi hawali wala demokrasia sio hitaji lao la msingi,bali hili ni lenu wanasiasa maana huko mdio shambani kwenu.

Mtapiga zomali sana lakini mwisho wa siku wananci tunawaona na tutawaadhibu kwenye debe la kura 2020.
#Tuko na JPM 2020[emoji1241][emoji818]
Tunahitaji maendeleo zaidi kuliko uhai wetu na afya zetu. Hivyo diuo muhimu kwetu, tukiona barabara nzuri mgonjwa anapona hata kama hanabhela ya matibabu.
Minimum wage ni laki 2 sasa umelazwa muhimbili unatakiwa laki 5 hawaku discharge mpaka kulipa deni.
Kwa ufupi mshahara hulingani na hali ya maisha na hicho ndiyo kitu muhimu wananchi wananchohitaji.
Huwezi kununua nyumba ya kisiasa na gari watoto hawana ada wala chakula ukasema hayo ni maendeleo huo unaitwa uwendawazimu.
 
Hua wanakauli yao ya kijinga sana eti "KATIBA SIO NENO LA MUNGU, WALA KATIBA SIO BIBLIA AU QURAN".

Ila wasubiri wakimaliza muda wao, ndio watakapojua maana ya "UPEPO WA KISULISULI", atakaeshika mpini akimwaga ujinga wote uliofanyika katika uongozi huu. Lazima BP iwahusu viongozi wengi wa utawala huu.
 
Kwa haya machache tunayoyaona, Rais wetu anavunja taratibu na kanuni waziwazi, vipi kwa tusiyoruhusiwa kuona? Tutazame haya machache:

1. Nafasi 10 alizopewa kuteua wabunge alivunja katiba tukapiga kelele mmoja akajiuzulu kisha kupewa ubalozi. Hata hivyo kujiuzulu kwa huyo mmoja hakukumoondolea hadhi ya kulipwa mafao kama mbunge.

2. Uteuzi wa Jaji mkuu alienda kinyume cha taratibu za kimahakama, akateua kaimu Jaji mkuu. Sijuia alikuwa anataka atimiziwe kwanza matakwa yapi ndipo amthibitishe? Nadhani alifanikiwa. Sasa tunaona hukumu zikiamuliwa na DPP lakini kwa kivuli cha Rais.

3. Kwenye uteuzi wa CAG mpya amevunja tena katiba waziwazi na hata hivyo ameshindwa kabisa kutafsiri neno "Shall" kisheria ambalo limo kama muongozo wa utendaji wa CAG katika kanuni zinazoongoza ofisi hiyo. Hata hivyo tunamkumbusha Rais aelewe kuwa kanuni zinazoongoza ofisi yoyote ile ya umma zimetokana na muongozo mama sheria iliyopitishwa na bunge kwa kuzingatia katiba. Kanuni hazijawahi kuwa juu ya katiba hata siku moja.

4. Kwenye manunuzi makubwa na utekelezaji wa miradi mbali mbali mikubwa ame by-pass muongozo wa bunge na ndiyo maana havikaguliwi. Huu ni ufisadi wa aina yake.

Tunamkumbusha Rais kuwa aliapa kuilinda katiba. Hakuzungumza tu pale uwanja wa Uhuru, aliapa!
Aliapa ndiyo kuilinda katiba lakini je, alikuwa ameshawahi japo kuisoma?? I am sure yeye alijua kwenye katiba kuna maneno tu kama CATARYST, MAENDEREO, OPPOSITE DIRECTION n.k hivyo basi aliapa kukilinda kitu asichokijua
 
Aliapa ndiyo kuilinda katiba lakini je, alikuwa ameshawahi japo kuisoma?? I am sure yeye alijua kwenye katiba kuna maneno tu kama CATARYST, MAENDEREO, OPPOSITE DIRECTION n.k hivyo basi aliapa kukilinda kitu asichokijua
Leo katuthibitishia kuwa yeye hana wa kumuongoza.
 
Hua wanakauli yao ya kijinga sana eti "KATIBA SIO NENO LA MUNGU, WALA KATIBA SIO BIBLIA AU QURAN".

Ila wasubiri wakimaliza muda wao, ndio watakapojua maana ya "UPEPO WA KISULISULI", atakaeshika mpini akimwaga ujinga wote uliofanyika katika uongozi huu. Lazima BP iwahusu viongozi wengi wa utawala huu.
Asante
 
1. Kuagiza bilion 40 zitoke hazina zikalipe wakulima wa korosho bila pesa hizo kutengwa kwenye bajeti au bila pesa kuidhinishwa na bunge

2. Uteuzi wa CAG mpya usiozingatia subsection 3 ya sheria

3. Kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na kufanya siasa kinyume cha katiba

Vyote hivyo ni uvunjifu wa sheria za nchi, lakini ah!
 
Huyu mtu anachokitafuta hakika ipo siku atakipata tu

Kiukweli ni mtu asiye na mapenzi mema na nchi hii hata kidogo ana lake jambo analolitengeneza hakuna kingine
Mwenye serikali yupo!!!.jpeg
 
Mjuaji mwingine huyu mleta mada. Kwa hiyo unaifahamu maana ya shall kuliko wanasheria wanaomzunguka rais?.
 
Back
Top Bottom