Kama Lissu hajawahi kutengeneza faida kwenye maisha yake: Kwa mujibu wa Yesu atashindwa kuongoza Chadema

Kama Lissu hajawahi kutengeneza faida kwenye maisha yake: Kwa mujibu wa Yesu atashindwa kuongoza Chadema

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Luka 19:17
Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

Kuna uhusiano wa uwezo wa uongozi, na uwezo wa kuzalisha faida kwenye maisha ya kila siku. Mtu ambaye anauwezo wa kupewa elfu 10 ndani ya siku akakuletea 13000 ndiye anaqualify kuongoza kwa Mujibu wa Yesu.

Yule jamaa aliyezalisha zaidi alipoleta hesabu , Zawadi yake ilikuwa ni kutawala au kuwa kiongozi.

Lissu anaingia akiwa na sura ya umasikini lakini akiwa hana historia ya uzalishaji. Sijajua kupitia uanasheria wake umeweza kumfanya azalishe kiasi gani kama ushahidi wa uwezo wake wa kumonetize ujuzi wake ili Yesu amfanye mtawala bora hapo chadema.

Lakini kama ni hivihivi tu, atapata shida kuliko tunavyodhani. Nampenda na namuunga mkono ila hilo nalo alijue.

Viongozi wa kiafrika wenye poverty mentality wasioweza kuzalisha kwa ajili yao na kuwa na akiba kwa ajili ya kusaidia jamii ndio wanakuwa wezi wanapoingia madarakani. Wanajilimbikizia mali na kutengeneza magenge ya wizi serikalini na kwenye jamii maana wanaamini hawana uwezo wa kuzipata hizo kwa nguvu zao.

Ni hilo tu.

Mtumishi Matunduizi.
WWasalam
 
Tundu Lissu hana uwezo wa kuiongoza CHADEMA. Lissu ni wa kuongozwa na siyo kuongoza.
 
KIONGOZI GANI TAJIRI ALIINGIA MADARAKANI KM TAJIRI AWAMU ZOTE ZILIZOPITA?
 
Singida nyumbani kwao hajajenga nyumba, huwa anafikia gesti, nyumba ya Dar aliijenga baada ya kuiba fedha za Lawyers Environmental Action Team akiwa na Dk Nshala, na mwingine marehemu
 
Pepo la kubeti limemuharibu sana Lema, infact bado linamlemea na kumzonga mno, hafurukuti kiuchumi mbele ya muhindi 🐒
 
Hata siku Moja Wana harakati hawajawahi kufanikiwa kwenye uongozi.

🔹Kwa Sasa anadanganywa na watu wa club house na maria space ambao wengi ni masela nondo waliozamia ugaibuni wanaotaka siasa za ghasia

🔹 Wataanza ku dictate chama kutaka kile wanachofikiria wao ndio kitekelezwe

🔹Vikao halali vya chama vitagoma kuendeshwa kwa remote na watu ambao ni anonymous

🔹 Watalazimisha kuingia kwenye uchaguzi ili wapate FEDHA za ruzuku ( njaa Haina BAUNSA) hao ma dayaspora wataanza kumgeuka mbona ulisema no election no refomu no kampain?

🔹Wataanza kumshambulia, na kujitoa kuchangisha vidola viwili. Chama kitaishiwa FEDHA. Wenye njaa Kali zaidi watakimbilia nambari wani. Watabaki wachache wakiwa wanasigana. Mwisho wa taarifa ya habari inabaki historia. Mzee wa kunja ngumi anafuatwa na wazee wahafidhina ruuudi baba ruuudi baba but it is too late. Hakuna wa kuandamana saa hizi vijana wapo busy kutengeneza maisha na wanaogopa.migogoro na vyombo vya Dola maana mwisho wa siku MCHUMA JANGA HULA NA WAKWAO
 
Back
Top Bottom