Kama mshahara ni chini ya Tsh 150,000/= kwa mwezi bora useme unatangaza nafasi za utumwa kuliko useme ni nafasi za kazi

Kama mshahara ni chini ya Tsh 150,000/= kwa mwezi bora useme unatangaza nafasi za utumwa kuliko useme ni nafasi za kazi

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Leo nimesikitika sana baada ya kusoma uzi wa jamaa anayetaka wahudumu wa mgahawani kwa mshahara wa Tsh 2000/= kwa siku kwa hoja kwamba watakula bure mgahawani. Watu wengi kwenye ule uzi wamempinga vikali mleta mada. Mimi pia niliandika comments za kupinga huo ujinga.

Ninawasihi waajiri binafsi watoe ujira ambao mtu anaweza hata kulipa nauli ya daladala na kubakiwa hata na Tsh 2000/= kila siku badala ya huu utumwa wanaoutangaza. Kama biashara yako haina mzunguko mzuri ni bora ukakomaa kivyako na familia yako hadi pale utakapoweza kuajiri mtu mwingine. Au akijitokeza mtu wa kujitolea ndo umlipe hizo posho kuliko kusema eti ni nafasi za kazi wakati ni utumwa mtupu.

Hata wafanyabiashara wakubwa wenye viwanda wanatuhumiwa kulipa mishahara ya chini ya Tsh 5000/= huku watu wakipigika hatari. Utetezi wao ni kwamba wakipandisha mishahara watashindwa kuendesha viwanda. Huu ni uongo mtupu. Hao matajiri ni wabinafsi wasio na utu. Kama kwenye net profit kwa mwaka tajiri anaweza kujinunulia V8 la anasa au kujijengea hekalu anawezaje kusema gharama za ku-run ni kubwa? Pia kusema kodi ni tatizo ninapinga. TRA wanachukua kodi baada ya kuangalia gharama zako za uendeshaji. Ina maana kiasi kidogo utachoongeza kama posho kwa wafanyakazi kitajumuishwa kwenye matumizi ya kampuni na kupelekwa TRA.

Watanzania tupendane na tuache kukandamizana. Kama sisi wa chini tunakandamizana kamwe hatuwezi kuwa kitu kimoja na kukataa ukandamizaji wa baadhi ya viongozi.
 
Hahahahah jamaa mzinguaji ni kama unapiga gitaa, kutibu hilo tatizo labda ugombee urais na unaweza ukapata na bado ukashindwa kutatua hilo tatizo.
Sijui viwanda vinapata wapi ujasiri wa kulipa watu elf 4 na mia tano mtu anayefanya kazi kuanzia saa 1 asubuhi hadi saa 2 usiku.
 
Kama ungekuwa na hiyo quality ya kulipwa 9Million usingeiomba hiyo kazi.Kutengeneza ajira Siyo jambo jepesi hata nchi ikitaka kuajiri lazima wajipange!

Tuboreshe mazingira ya biashara halafu mapato yakiwa mazuri automatically mishahara itapanda vinginevyo biashara zitafilisika
 
Leo nimesikitika sana baada ya kusoma uzi wa jamaa anayetaka wahudumu wa mgahawani kwa mshahara wa Tsh 2000/= kwa siku kwa hoja kwamba watakula bure mgahawani. Watu wengi kwenye ule uzi wamempinga vikali mleta mada. Mimi pia niliandika comments za kupinga huo ujinga.

Ninawasihi waajiri binafsi watoe ujira ambao mtu anaweza hata kulipa nauli ya daladala na kubakiwa hata na Tsh 2000/= kila siku badala ya huu utumwa wanaoutangaza. Kama biashara yako haina mzunguko mzuri ni bora ukakomaa kivyako na familia yako hadi pale utakapoweza kuajiri mtu mwingine. Au akijitokeza mtu wa kujitolea ndo umlipe hizo posho kuliko kusema eti ni nafasi za kazi wakati ni utumwa mtupu.

Hata wafanyabiashara wakubwa wenye viwanda wanatuhumiwa kulipa mishahara ya chini ya Tsh 5000/= huku watu wakipigika hatari. Utetezi wao ni kwamba wakipandisha mishahara watashindwa kuendesha viwanda. Huu ni uongo mtupu. Hao matajiri ni wabinafsi wasio na utu. Kama kwenye net profit kwa mwaka tajiri anaweza kujinunulia V8 la anasa au kujijengea hekalu anawezaje kusema gharama za ku-run ni kubwa? Pia kusema kodi ni tatizo ninapinga. TRA wanachukua kodi baada ya kuangalia gharama zako za uendeshaji. Ina maana kiasi kidogo utachoongeza kama posho kwa wafanyakazi kitajumuishwa kwenye matumizi ya kampuni na kupelekwa TRA.

Watanzania tupendane na tuache kukandamizana. Kama sisi wa chini tunakandamizana kamwe hatuwezi kuwa kitu kimoja na kukataa ukandamizaji wa baadhi ya viongozi.
Hiko ni kibarua sio kazi, probably hata mkataba hutopewa
 
Ni kweli ni mshahara mdogo sana huo
Ila kulingana na maisha yenyewe ndio sababu
Hela haina thamani ili iwe na thamani lazima muuze vitu vingi nje kuliko vinavyoingia la sivyo mtakuwa mnashindia mihogo tu
Serikali ndio ya kuilaumu kwa haya
Ukiritimba mwingi
 
Leo nimesikitika sana baada ya kusoma uzi wa jamaa anayetaka wahudumu wa mgahawani kwa mshahara wa Tsh 2000/= kwa siku kwa hoja kwamba watakula bure mgahawani. Watu wengi kwenye ule uzi wamempinga vikali mleta mada. Mimi pia niliandika comments za kupinga huo ujinga.

Ninawasihi waajiri binafsi watoe ujira ambao mtu anaweza hata kulipa nauli ya daladala na kubakiwa hata na Tsh 2000/= kila siku badala ya huu utumwa wanaoutangaza. Kama biashara yako haina mzunguko mzuri ni bora ukakomaa kivyako na familia yako hadi pale utakapoweza kuajiri mtu mwingine. Au akijitokeza mtu wa kujitolea ndo umlipe hizo posho kuliko kusema eti ni nafasi za kazi wakati ni utumwa mtupu.

Hata wafanyabiashara wakubwa wenye viwanda wanatuhumiwa kulipa mishahara ya chini ya Tsh 5000/= huku watu wakipigika hatari. Utetezi wao ni kwamba wakipandisha mishahara watashindwa kuendesha viwanda. Huu ni uongo mtupu. Hao matajiri ni wabinafsi wasio na utu. Kama kwenye net profit kwa mwaka tajiri anaweza kujinunulia V8 la anasa au kujijengea hekalu anawezaje kusema gharama za ku-run ni kubwa? Pia kusema kodi ni tatizo ninapinga. TRA wanachukua kodi baada ya kuangalia gharama zako za uendeshaji. Ina maana kiasi kidogo utachoongeza kama posho kwa wafanyakazi kitajumuishwa kwenye matumizi ya kampuni na kupelekwa TRA.

Watanzania tupendane na tuache kukandamizana. Kama sisi wa chini tunakandamizana kamwe hatuwezi kuwa kitu kimoja na kukataa ukandamizaji wa baadhi ya viongozi.
Mkuu kuna watu hawana huruma au alitaka aonekane ametoa ajira, ujue hata mm nimefikiria sana, kwa mshahara wa 2,000.00/day mtoto wa mtu apande daladala kutoka anakoishi mpaka kibaruani kwake na kurudi kwao, anunue sabuni ya kufulia nguo zake maana jamaa kasema awe msafi, kweli?????.

Bado muda wa kazi anaanza saa 1:00 asubuhi mpaka saa 4 usiku hii inamaanisha awe anaamka saa kumi alfajiri na kulala saa sita usiku, kama anakoishi ni mbali na foleni za DSM hii sijui itakuwaje

Vinginevyo utakuta anawalaza watoto wa watu stoo ya vyakula. Zaidi sana hawa mabinti itabudi wajiuze kwa wateja wao chakula ili waweze kumudu maisha.

Ninatambua tunateswa na ufukara na wahitaji wa kazi hii ni wengi, lakini jaribuni kuwaonea watoto wa watu huruma. Alienda mbali akasema kuwa atawahudumia chakula. ukweli ni kwamba hawa watu mara nyingi huwalisha wafanyakazi wao
''UKOKO au MABAKI ya chakula pamoja na michuzi.'' mfanyakazi akitaka ale vizuri inabidi akubali akatwe hela kwenye malipo yake.

Sawa hali ni ngumu lakini tuoneane huruma. Pia asilinganishe kazi ya mgahawa na kazi za ndani.
 
Back
Top Bottom