KERO Kama Muhimbili wamebadili ratiba ya kuona wagonjwa waseme. Wanatupa usumbufu mkubwa tunaotoka maeneo ya mbali

KERO Kama Muhimbili wamebadili ratiba ya kuona wagonjwa waseme. Wanatupa usumbufu mkubwa tunaotoka maeneo ya mbali

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Habarini JamiiForums,

Nawaailisha kero yangu kwenu iwafikie Hospitali ya Muhimbili, wanachotufanyia tunaokuja kuona wagonjwa si uungwana.

Juzi July 10, 2024 nilikwenda kuona mgonjwa nikiwa nimeambatana na baadhi ya ndugu, kufika pale tukakatiliwa kuona wagonjwa tukiambiwa ndugu waliokwenda kuona wagonjwa wametosha, hii ni sawa?

Ndugu wanaingia wanne eti mnaambiwa hii imetosha wengine mje siku nyingine na walinzi wanawakataza kuingia, na hapo siyo kwamba muda umeisha!

Mtu umetoka mbali umepoteza nauli na muda wako kuja kuzuiliwa kumuona mgonjwa wako hii siyo sawa. Kama muda umebadilika watuambie, itatusaidia sisi kujipanga hata kwa kujiwekea zamu, lakini siyo unafika na unajua upo ndani ya muda unazuiliwa kwenda kumuona mgonjwa wako.

Sijapenda kabisa nilichofanyiwa juzi.
 
Sasa mwanangu, watu wanne kumuona mgonjwa mmoja, kumbuka wodi ina vitanda vingapi, na kila watu wanne wamezunguka kitanda kimoja, hao wagonjwa watapata hewa kweli?

Mngejipanga muingie wodini kwa zamu.

Wodi nyingine ni mtu mmoja tu anaruhusiwa kuingia wengine mnakaa nje.

Tuliouguza wazazi na wenza tunalijua hilo.

Na mkienda mkasikia ndugu wa fulani njooni ofisini jua ndo hivyo tena.

Pole kwa kuuguliwa.
 
Kwanza hiyo ya kurundikana wodini eti kumuona mgonjwa ni ujinga unakuta mko 30 wote mnataka kumuona mgonjwa mmoja kwann msiteue mtu mmoja akaenda kumuona mgonjwa Kisha akaja kuwapa feedback?
 
Nadhani wangeweka muda maalum wa kumwona mgonjwa! Kila baada ya dk.10 wanaingia watu 4 kwenda kumwona mgonjwa harafu wanatoka! dk.10 nyingine wanaingia wengine mpaka masaa ya kumwona mgonjwa yatakapoisha! Kwa kufanya hivyo ndugu wengi wanaweza kumwona mgonjwa. Vinginevyo nikuongeza msongamano wa watu wodini.
 
Nadhani wangeweka muda maalum wa kumwona mgonjwa! Kila baada ya dk.10 wanaingia watu 4 kwenda kumwona mgonjwa harafu wanatoka! dk.10 nyingine wanaingia wengine mpaka masaa ya kumwona mgonjwa yatakapoisha! Kwa kufanya hivyo ndugu wengi wanaweza kumwona mgonjwa. Vinginevyo nikuongeza msongamano wa watu wodini.
wewe ndo umenena utaratibu wao n mgumu sana yaan hao ndugu wa4 watakaoingia ndo hao hao mpka lisaa liishe sasa ni utaratbh gani ilitakiwa kama akitoka mmoja anaingia mmoja
 
Habarini JamiiForums,

Nawaailisha kero yangu kwenu iwafikie Hospitali ya Muhimbili, wanachotufanyia tunaokuja kuona wagonjwa si uungwana.

Juzi July 10, 2024 nilikwenda kuona mgonjwa nikiwa nimeambatana na baadhi ya ndugu, kufika pale tukakatiliwa kuona wagonjwa tukiambiwa ndugu waliokwenda kuona wagonjwa wametosha, hii ni sawa?

Ndugu wanaingia wanne eti mnaambiwa hii imetosha wengine mje siku nyingine na walinzi wanawakataza kuingia, na hapo siyo kwamba muda umeisha!

Mtu umetoka mbali umepoteza nauli na muda wako kuja kuzuiliwa kumuona mgonjwa wako hii siyo sawa. Kama muda umebadilika watuambie, itatusaidia sisi kujipanga hata kwa kujiwekea zamu, lakini siyo unafika na unajua upo ndani ya muda unazuiliwa kwenda kumuona mgonjwa wako.

Sijapenda kabisa nilichofanyiwa juzi.
Nilichosikia ni kuwa wanaruhusu watu 2 kwa siku. Naona sio sawa, wangeruhusu watu 2 kwa dakika kadhaa, wakitoka wanaingia wengine 2 ingependeza.
 
Nilichosikia ni kuwa wanaruhusu watu 2 kwa siku. Naona sio sawa, wangeruhusu watu 2 kwa dakika kadhaa, wakitoka wanaingia wengine 2 ingependeza.
Mgonjwa anaitaji matibabu.
 
Back
Top Bottom