Kama ni kweli haya tunayoyasikia katika mchakato huu wa uchaguzi, kuenguliwa kwa idadi kubwa ya wapinzani kwa kile kinachoitwa kukosa sifa. Je, wahusika hawaoni kuwa hii hali inaweza kupelekea vurugu zisizokuwa za lazima?
Hivi inakuwaje hiyo kukosa sifa kunatokea upande wa wapinzani tu? Je, ni sifa gani hizo ambazo wapinzani wamazikosa kwa idadi kibwa namna hiyo na hakuna hata mgombea mmoja wa CCM aliyekosa hizo sifa?
Je, Nec, Vyombo vyetu vya Ulinzi, Viongozi wa Dini na wazee wetu wastaafu, mnakubaliana na mwenendo huu? Siombei itokee lakini najiuliza tu ikiwa upizani utakosa uvumilivu katika hili na kama ambavyo tumesikia matamko yao mbali mbali, Je mtajiweka katika nafasi gani?
Kwa miaka mingi nchi yetu imejizolea sifa kuwa kisiwa cha Amani, na wengine tuliobahatika kufika nchi za watu tulekuwa tukitamba kuwa tunatoka kwenye kisiwa cha Amani.
Sasa ni vema tukaendelea kuidumisha hiyo sifa kwa kuzuia viashiria vyote vinavyoweza kuharibu amani yetu.
Binafsi natamani kuona Nec wanarekebisha hii hali mapema iwezekenavyo. Na kama kuna ulazima wa kumuengua mtu basi iwe ni kwa sababu zenye mashiko, (1) kama kutokuwa raia wa tanzania kwa kukosa vigezo vyote vya uraia sio kusingizia.(2) kuwa na mashitaka ya kutenda jinai.(3) kukosa maadili tena kwz ushahidi usiokuwa na shaka.
Katika hili haki itendeke, haileti picha nzuri kwamba wanaokosa sifa ni upande wa upinzani tu. Tuipende nchi yetu na tuilinde kwa kuanzia na kupendana sisi kwa sisi bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kidini, maumbile yetu, makabila yetu, rangi zetu, au eneo tunalotoka na tuamini kwamba yeyote anayechaguliwa anaenda kufanya kazi ya kuiletea maendeleo Tanzania yetu.
Tuwaache wagombea watoe sera zao na Watanzania wapiga kura wawe ndio waamuzi wa mwisho. Sisi sote ni Watanzania tutendeane kama Watanzania.
Hivi inakuwaje hiyo kukosa sifa kunatokea upande wa wapinzani tu? Je, ni sifa gani hizo ambazo wapinzani wamazikosa kwa idadi kibwa namna hiyo na hakuna hata mgombea mmoja wa CCM aliyekosa hizo sifa?
Je, Nec, Vyombo vyetu vya Ulinzi, Viongozi wa Dini na wazee wetu wastaafu, mnakubaliana na mwenendo huu? Siombei itokee lakini najiuliza tu ikiwa upizani utakosa uvumilivu katika hili na kama ambavyo tumesikia matamko yao mbali mbali, Je mtajiweka katika nafasi gani?
Kwa miaka mingi nchi yetu imejizolea sifa kuwa kisiwa cha Amani, na wengine tuliobahatika kufika nchi za watu tulekuwa tukitamba kuwa tunatoka kwenye kisiwa cha Amani.
Sasa ni vema tukaendelea kuidumisha hiyo sifa kwa kuzuia viashiria vyote vinavyoweza kuharibu amani yetu.
Binafsi natamani kuona Nec wanarekebisha hii hali mapema iwezekenavyo. Na kama kuna ulazima wa kumuengua mtu basi iwe ni kwa sababu zenye mashiko, (1) kama kutokuwa raia wa tanzania kwa kukosa vigezo vyote vya uraia sio kusingizia.(2) kuwa na mashitaka ya kutenda jinai.(3) kukosa maadili tena kwz ushahidi usiokuwa na shaka.
Katika hili haki itendeke, haileti picha nzuri kwamba wanaokosa sifa ni upande wa upinzani tu. Tuipende nchi yetu na tuilinde kwa kuanzia na kupendana sisi kwa sisi bila kujali itikadi zetu za kisiasa, kidini, maumbile yetu, makabila yetu, rangi zetu, au eneo tunalotoka na tuamini kwamba yeyote anayechaguliwa anaenda kufanya kazi ya kuiletea maendeleo Tanzania yetu.
Tuwaache wagombea watoe sera zao na Watanzania wapiga kura wawe ndio waamuzi wa mwisho. Sisi sote ni Watanzania tutendeane kama Watanzania.