Kama ni ndoto, mbona haiishi?

Haya mambo ya kutoana machozi asubuhi si mazuri mkuu.

Pole sana mungu akupe nguvu
 
Kaka!
ndivyo inavyotokea pale tunapowapoteza wapendwa wetu,mawazo yetu yan ndani huwa hayataki kuamini na huwa tunatamani iwe tofauti na ilivyo,inauma sana.

Ila Mungu ni muweza wa yote weka kila kitu kwake naye atakupa nguvu na imani kuweza kuyakubali hayo yaliyotokea na kuendelea na maisha,kwa nguvu zetu wenyewe mengi hayawezekani ila kwa nguvu zake Manani yote yanawezekana,amini sote tutakutana nae tena Sayuni kwenye siku ilee ya mwisho.

Pole kaka.
 
Mungu amlaze mahalipema peponi Amin. naakupe afuwan inshaalaah. kisahiki kimeniliza sana nahizi uchungu mpaka sasa. pole sana mkuu mungu kampenda zaidi


 
nimejikuta nikipata majonzi kama mimi ndio mhusika wa hili jambo. pole sana ndugu yangu!
 
Ndugu yangu, naomba kukutia nguvu, ni ngumu na haisahauliki ila mgeukie MUNGU WA MBINGUNI yeye anauwezo wa kuziba majonzi moyoni mwako kwa upendo wake.jitaidi kuwa msomajiwa Biblia na vitabu mbalimbali, kutazama sinema na kukaa na marafiki isikae mwenyewe ili kupunguza mawazo.nataka uwe na moyo mkuu na ujasiri.tunakuombea kwa MUNGU WETU atakutia nguvu.
 
".....I ain't got no time to pretend that I'm not missin' You
Oh no no no no
I know You're in good hands the same hands that hold my heart
And I'll cherish every moment that we've spent
As a gift from God above for He takes care of all fragile hearts.."

Kipande toka Fragile hearts wa Yolanda Adams ukipata muda usikilize..,
Pole sana Mkuu
 
story yako imenitia uchungu na simanzi moyoni,mungu akutie nguvu na ujasiri pole sana mpendwa
 
Mestod pole sana, kazi ya mungu haina makosa. Mshukuru mungu kwa kila jambo.
 
Duh, nimelia aje? hii ni mipango ya mungu MESTOD yani wengine tunalia vitu vidogo vya masahibu ya mapenzi mwenzetu una zigo kubwa la matatizo na mawazo, mungu akutie nguvu sana mpendwa, haya yote ni mapito ya dunia lazima tuyapitie. muombee mungu marehemu huku ukijipa moyo na kuendelea na maisha, binadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni fupi sana nazo zimejaa misukosuko ya hapa na pale walipoandika haya hawakukosea.POLE SANA
 
Dedication mwimbo mpya wa lina, najuaaa kama umelala, na huwez amkaaaa, wewee. ila kufumba kwako macho..............
 

Ahsante Gaga. Lakini unajua tatizo ni tatizo tu. Huwezi kuwa na maumivu ya kichwa halafu mwenzio kakatwa mkono ukasema afadhali mimi kichwa kuliko yule kakatwa mkono. Maumivu yataumiza tu, haijalishi ukubwa wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…