Kama ningepata bahati ya kumshauri Rais Dkt. Mwinyi ningemshauri haya

Kama ningepata bahati ya kumshauri Rais Dkt. Mwinyi ningemshauri haya

KAUCHEZEA

Member
Joined
Mar 4, 2013
Posts
29
Reaction score
15
Ushauri wangu kwako Rais wangu Dkt. Mwinyi.

1. Kupitia kampuni zote za tour operator na mikataba ya wafanyakazi wa ndani Bara na Visiwani.

2. Kulipwa fidia kwa wafanyakazi waliotimuliwa kazi bila utaratibu wa kisheria wkt wakiwa ndani ya mikataba.

3. Kutokupewa vibali kwa wafanyakazi wageni waliokuwa wakijiona Zanzibar ni ya kwao mfano General managers.

4. Kurudishwa makwao managers waliokuwa wanaishi Znz kiujanja janja na kuwaona wafanyakazi wa Tanzinia sio watu. Mfano ubaguzi wa rangi na ubaguzi wa kimaslahi.

5. Timua wageni wote wasiofata taratibu za nchi mfn Sheria za kazi na ajira na ukwepaji wa Kodi.

6. Mwanzoni mwa ugonjwa wa Corona,manyanyaso mengi kwa wafanyakazi wa ndani Bara na Visiwani yalifanyika pasipo watu kulipwa stahiki zao.

Tunaomba Rais wetu ufanyike uchunguzi kwa tour operators na mahotelini ili watu wapate haki zao na waliofanya hivyo wachukuliwe hatua.

Mh Rais Dkt. Mwinyi wananchi wako wengi wanamaumivu moyoni na kupoteza mwelekeo wa maisha baada ya kuachishwa kazi ghafla pasipo kupewa haki zao.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki Viongozi wetu.

Amina
 
Tatizo linaanza kuwa serekali yenyewe haijali wananchi wake, Hivyo vitimbi vya wamiliki na viongozi wa mahoteli vinaendelea kufanyika kwa sababu serekali inaridhia hayo. Maafisa wa serekali wanachojali wao ni rushwa tu hakuna jengine, hawashuhuliki kabisa na wafanyakazi.
hivi ile mifuko yao ZSSF imefanya nini kuwasaidia wale wafanya kazi waliopoteza ajira? Hata hela zao wamegoma kuwapa.
As long hii nchi inaendelea kuongozwa na CCM mwananchi wa kawaida ataendelea kudhalilika na kuteseka tu.
 
Back
Top Bottom