Kama si mzee Aboud Jumbe kusingekuwapo na CCM

Mkuu JokaKuu,

Hapo umenena, sioni sababu ya mjadala kuhamia kwenye mashambulizi dhidi ya Nyerere, litakuwa jambo jema kama watu watafahamishwa kuhusu makuu aloyatenda Mzee Jumbe. Yaliyomkuta Mzee Jumbe hayakusababishwa na Nyerere pekee, sidhani kama alikuwa na uwezo huo, bali watu kama kina Seif na kiu yao ya kuongozi visiwa hivyo, ni wazi walitumia mwanya ulojitokeza kummaliza Mzee Jumbe wakitambuia udhaifu wa Mwalimu linapokuja suala la Muungano.

Bado narudia kila kiongozi anapita katika wakati wake, huongoza kulingana na mazingira ya wakati huo, hivyo uongozi wake huwa na matokeo hasi na chanya, hauwezi asilani ukawa na mazuri matupu. Hata Amini pamoja na kuonekana kuwa kiongozi dhalimu bado kwa Waganda yapo mazuri alowafanyia na wanamkumbuka kwa hayo pia.

Mzee Jumbe kafanya mengi kwenye ujenzi wa demokrasia visiwani humo, hilo halina ubishi na anayepinga ana lake jambo.
 
Mkuu kumbuka hata kina jumbe walimtosa field marshal tito okero.kuna mabo mengi sana yanayouhusu hizi nchi mbili yamefichwa sio hilo la istoria ya aboud jumbe tu
Hamna Okello ni victim mwengine katika mikono ya Mwalimu, ni yeye Mwalimu aliyefitinisha mpaka akafukuzwa kisingizio Okello alipanga na wanajeshi waasi kuipindua serikali yake, akamuagiza Karume amfukuze na kumrejesha kwao, na akina Jaha Ubwa walimchukuwa kwa ndege mapka Kenya wakati huo Mwalimu alishazungumza na Kenyatta asimpokee Okello na alipokwenda kwao Uganda Mwalimu alimwambia Obote "hatari" ya mtu kama Okello naye akamfukuza, akakimbilia Msumbuji kujiunga na FRELIMO bila kutaka.
ZAIDI REJEA:" ZANZIBAR REVOLUTION" by John Okello. kw maneno yake mwenyewe.
 
suala la kuamini na kutoamini hilo ni la mtu binafsi, hivyo ndivyo waandishi wa historia wa u.n walivyoandika. Haya ya salmani usiyalete yanagusa imani za watu, na moto wake hauzimiki plz

EEhenhe!! "Imani za watu"!! wewe uliongelea suala la uenye heri wa Nyerere, hiyo nayo ni imani ya watu!!wacha ubinafsi.
 

"Aliemfitinisha" hii ndiyo lugha yenu ya kuwatambulisha, huwa mnaitumia sana tu, lakini tunaowajua malengo yenu hatutaacha kuwaambia muache tabia hiyo ya kugeuza ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli..... ni tabia ya Kishetani.
 
Ni ile habari ya kuchafuka hali ya kisiasa Visiwani wakati ule!

Wakati huo sisi tulikuwa bado vijana: waliokuwepo ule wakati wanaweza kutuhabarisha yaliyomfika Jumbe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…