Kama TBC haioneshi Mechi ya Timu ya Taifa (Taifa Stars V J.Afrika ya Kati)..ni lipi lioneshe?

Kama TBC haioneshi Mechi ya Timu ya Taifa (Taifa Stars V J.Afrika ya Kati)..ni lipi lioneshe?

matunge

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2010
Posts
442
Reaction score
426
Inasikitisha kuona shirika la habari la Taifa (TBC) linashindwa kuonesha mechi muhimu ya Timu yetu ya Taifa. Na kutegemea shirika binafsi kuonesha.Duniani kote Shirika la umma ndilo linapaswa kuwa la kwanza kutumia njia yoyote ile ili kuonesha tukio la kitaifa.Hivi TBC na TFF mnafikiria nini katika hili? ni lazima mjue Taifa Stars ni timu ya watanzania wote na si wakazi wa Dar es Salaam tu.Mnapaswa kuhakikisha mnafikia makubaliano na kuwapa raha watanzania.Leo mmenisikitisha sana kutokuonesha mechi hii muhimu.Hivi mnafikiri ni kwa nini watu wanapenda sana ligi ya ulaya..hasa uingereza...moja ya sababu (pamoja na kuwa ni bora) ni kutangazwa sana. Sasa nyie mnafikiri sisi wa vijijini tutaipenda vipi Taifa Stars bila ya kuiona ikicheza???
 
KBC wanaonyesha game kati ya Angola na Harambee....TBC ni chombo cha wasanii tu.....................................
 
KBC wanaonyesha game kati ya Angola na Harambee....TBC ni chombo cha wasanii tu.....................................
inasikitisha sana..japokuwa tunafurahia ushindi
 
Hilo liko busy na ze komedi na propaganda wa watu wa ccm!! Hata wakionyesha siyo ajabu kukata matangazo ili kurusha hotuba zao au bunge. La muhimu ni kuwaomba vituo binafsi vijieneze nchi nzima.
 
...nafikiri ruzuku imepunguzwa sana sasa jeuri yote kwisha kazi!!!! wapo pale kisiasa zaidi na si kisasa zaidi!!
 
Back
Top Bottom