“Kama tunatoa ripoti na kuna ubadhirifu na hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu wa Bunge." Sehemu ya nukuu ya Professor Assad

“Kama tunatoa ripoti na kuna ubadhirifu na hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu wa Bunge." Sehemu ya nukuu ya Professor Assad

Lucas Julson

Member
Joined
Sep 8, 2014
Posts
12
Reaction score
4
“Kama tunatoa ripoti na kuna ubadhirifu na hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu wa Bunge. Bunge linatakiwa lisimamie na kuhakikisha kwamba pale penye matatizo, linahakikisha kuwa hatua zinachukuliwa. Sasa, sisi kazi yetu ni kutoa ripoti tu,” Professor Assad aliyekuwa kuwa CAG

Wakati tukiendelea kufuatilia mjadala wa suala la Mh. Mpina kuna haja ya Bunge na Serikali kutupatia majibu ya baadhi ya maswali mfano;
1. Mh. Mpina ni mbunge wa muda mrefu kidogo hivyo anajua Kanuni na taratibu zinazoliongoza Bunge, Kwa nini aliamua kutoa ushahindi sehemu mbili kwa Mh. Tulia na kwenye vyombo vya habari??
Kuna nini nyuma ya maamuzi haya

2. Ushahidi wake ni wa kweli? Kama jibu ni ndiyo kwa nini Mh. Bashe hakuhojiwa kama Mh. Mpina?

3. Kama ushahidi ni WA Uongo kwa nini Bunge na Serikali wamekaa kimya wakijua kabisa Ushahidi huo unazua Taharuki kwa wananchi?

4. Wanatupa tafsiri gani wananchi kwamba Mh. Mpina ni msaliti au wao ndiyo wasaliti?
 
Back
Top Bottom