Unajua najiuliza sana. Zamani, enzi za Nyerere na Mwinyi ambapo uchumi ulikuwa mdogo sana, bado tulikuwa na mashirika makubwa ya ndege ya kimataifa yakija na ndege zao hapa Dar es Salaam. Ninavyoelewa, kiashiria kimojawapo kwamba uchumi wa nchi uko vizuri ni kuwa na mashirika ya ndege mengi ya kimataifa yakifanya safari kuja nchini kwenu.
Sasa iweje kama uchumi unakua ndipo tunapoteza hayo mashirika?