Me nakumbuka niliambiwa hivyo na binti xxxxx wa kirangi ila sasahivi hata kusalimiana ni issue na hataki hata kuniona yani kwa kifupi hakuna mtu mwenye upendo na mwenzake.Katika mapenzi yetu niliwahi kumuunganisha hadi humu JamiiForums na nilishangaa sana kwenye uzi ya 'Andika chochote kuhusu mpenzi wako wa zamani' aka-reply "AKAFIE MBELE".Dah of course ile ilikuwa inanihusu mimi na nikagonga "LIKE" nikachapa raba.
Nikikumbuka maneno yake nabaki nashangaa tu..
Je unakumbuka nini ukisikia sentensi hiyo "Sitakuacha maisha yangu yote"?
Hayo maneno wanayaongea mshobobo ukiwakolea Na wakikutana Na mwenye kisu kikali zaidi yako wanakutosa kimyakimya.
Dawa ya mapenzi ya kibongo, USIWEKEZE moyo wako, Wekeza KUCHA Na nywele hata vikikatika vitaota tena