Kama umewahi kupata mkopo toka nje ya nchi pitia hii

Ngatu

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2018
Posts
263
Reaction score
185
Habari zenu wakuu .....naomba niende moja kwa moja kwenye mada ...juzi juzi nilikuwa nasoma investments habari nikabahatika kuona kumbe unaweza kukopa nikaclick then nikapewa contact pamoja na email nikawasiliana nao na nikajisajili badae tukaja mpaka kwenye kutuma accont number ndayopokelea mkopo. wakanambia mkopo wako umeshakuwa approved sasa natakiwa kutuma insurance fee kupitia wasternunion ili pesa yangu iwe safe na iweze kunifikia na wamenipa namba za mashuda waliowahi kukopa toka nchi mbali mbali nimewauliza wananambia ivo ivo ivo.Je ni kweli kwamba hiyo insurance fee unalipa mkopaji au kampuni ndio inagharamia
 
Mkuu jiongeze wewe, Hamna kitu cha namna hiyo...unatapeliwa! ushawahi kuona wapi unatoa Pesa ili Upate pesa za mkopo...
 
Mkuu jiongeze wewe, Hamna kitu cha namna hiyo...unatapeliwa! ushawahi kuona wapi unatoa Pesa ili Upate pesa za mkopo...
mkuu upo sawa na mimi nilimuuliza how comes ninashida ya pesa halafu nikatoa pesa akanambia bila hiyo insurance fee siwezi pata mkopo ...
 
Waambie hiyo insurance wakate hapo hapo kwenye huo mkopo ambao upo approved
niliwambia hivo lakini wakasema hizo sio terms and condition za compuni yao nikamwambia bhasi anikopeshe yeye ili mkpo wangu ukifika nimlipe maana siamini huu mkopo akasema inatakiwa kutuma pesa
 
Sorry kwa kuingilia uzi. Ila napenda kuuliza eti inachukua siku ngapi kutumiwa message ya online payment verification code kwa card ya CRDB??
Maana leo ni siku ya tatu na sijapokea huo ujumbe kwa simu yangu.
 
Mkuu jiongeze wewe, Hamna kitu cha namna hiyo...unatapeliwa! ushawahi kuona wapi unatoa Pesa ili Upate pesa za mkopo...
Insurance unalipa kwanza kabla ya mkopo kuingia hata hapa kwetu bongo.
Sema huko ni utapeli tu hakuna jingine.
 
Sorry kwa kuingilia uzi. Ila napenda kuuliza eti inachukua siku ngapi kutumiwa message ya online payment verification code kwa card ya CRDB??
Maana leo ni siku ya tatu na sijapokea huo ujumbe kwa simu yangu.
Ni ukimaliza kujisajili unapata sms za crdb kama ukiunganishwa na namba yako wakupa password za kuanzia utaenda atm utachange no ya siri
 
Mara nyingi matapeli na kampuni zao au majina yao cia huwa wana list zao
Kila unapopata taarifa za hivyo au unataka kujiridhisha ni lazima uangalie je ni genuine au utapeli?

Unaweza kupata mkopo kutoka nje labda uwe una acc huko na una hela zako huko

Tuwe makini kuna fake news kila kona siku hizi
 
wakuu hizi ni baadhi ya docoments nilizotumiwa leo
 

Attachments

  • IMG-ed8ef83a57d2f21a80474db3272e3d7c-V.jpg
    55.6 KB · Views: 25
  • IMG-5041f7fa1a17bd11ab671f4f4652cede-V.jpg
    24.1 KB · Views: 24
Insurance unalipa kwanza kabla ya mkopo kuingia hata hapa kwetu bongo.
Sema huko ni utapeli tu hakuna jingine.
Wanaitumia kama loophole kwa kutapela hii term ya mkopo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…