Kama una roho ndogo ukiisoma hii barua ya dogo Aslay lazima chozi lidondoke

Mleta MADA TAFADHALI NAKUOMBA....

kama unafahamiana au una ukaribu na dogo aslay mwambie hii barua naihitaji kupitia wimbo atakao utoa..

tena mwambie yeye hatokuwa wa kwanza kuandika au kutunga wimbo wa kuzungumza na mtu au roho iliyoko upande wa pili wa waisha ya mwanadamu...

mwambie kama anaweza apitie mitandaoni atafute wimboau album za mwanzo za mwanamuziki DMX alishawahi kuandika wimbo akimlalamikia na kumlilia MUNGU...

kiufupi mwambie aweke hisia katika kuisoma hiyo barua na nyuma yake kuwe na milio ya vinanda au violini vyenye melody ya huzuni sana...

hakika ATATEKA NYOYO ZA MASHABIKI WAKE NA MAJIBU YATAKUWA MAKUBWA KULIKO ALIVYOTARAJIA....

pia mwambie asihofie kuwa wimbo au hiyo barua itakuwa ndefu sana kwamba haitochezwa redioni...hapana...itachezwa mpaka na video yake itachezwa asiogope.

Kama hatoelewa concept nzima ya huo wimbo basi mwambie ajiunge jf anifuate pm nitajitolea kumwelwkeza jinsi ya kuufanya huo wimbo.

SHUKRANI ZA DHATI KWAKO NA KWAKE DOGO ASLAY.
 
Mwambie aslay asikilize wimbo wa DMX feat Faith evans MISS YOU...pia asikilize nyimbo ya dmx inaitwa prayers...atajifunza kuelezea story au hisia zake kwenye muziki na sio lazima uwe na vyombo hata akapela inatosha na akauza na kupata views za mamilioni youtube.
 
anataka akamate mashabiki kwa depression exotic,,only watu kama joyce kiria atawakamata,,
 
Kuweka hisia zako mitandaoni ni udhaifu
Ni udhaifu Kwa wale wasioelewa, lkn kwa mwelewa anayetambua njia mbalimbali Za relief hawezi sema ni udhaifu.

Tena hapo atapata ahueni kwa kile anachokumbana nacho. It's better kuongea public kuliko kukaa kimya.
 
Pole, mama amekufa lakini Mungu hafi, yupo na atakuwepo. Ukishafikia umri wa balekhe kila kitu sababu itakuwa ni wewe sio mzazi tena. Ondoa kile kipande cha nyuma kilichooza usichokipenda kwenye kazi zako na utengengeze upya kilichobaki kwa kiwango na matakwa yako.

Kuwa na mpango wa kazi zako, ongeza taaluma/ujuzi wako kwenye hicho unachokifanya na ongeza mtandao wako uwe mpana. Kuuliza si ujinga, waulize waliokutangulia kwenye mafanikio kupitia music ndipo uchanganye na akili zako. Hata hivyo, usimlaumu sana aliyekufikisha hapo japo hukufaidika kifedha lakini kitaaluma umefaidika saaana, watu walikufahamu kupitia huko.
 
Nachojua wafu wanahitaji msaada toka kwetu sisi tunaoishi,tuwaombee dua na toba kwa Mwenyezi Mungu sasa hii ya mtu hai kumuandikia barua marehem ilihal huyo marehemu mwenyewe hujui yuko wapi na anapitia kipindi kipi sidhani kama ni poa.
 
Mkuu milion 8.1 views kwa hapa bongo ni sawa kiasi gani tafadhali
 
Punguza mawazo! Yote ni mapenzi ya Mungu! Najua ni pengo lisiloweza kuzibika, kidonda kisichoweza kutibiwa, lakini hali inayoweza kuzoeleka. Najua ungetamani ale matunda ya kazi yako lakini atayaoata kwa kumuombea thawabu kwa Mungu
 
Akina diwani si ndo promota wako? Natumaj majibu ya hiyo barua wanayo wao. Yule mwingine anayeshitakiwa kwa kudurufu kazi ya maalimu bila ruhusa nae aliwatosa wenzie kama wewe na kumkumbatia kaka yako mkubwa.
 
Hizi hisia zake angemwambia Mungu wa mbingu na nchi zingeleta tija kwake kuliko kutueleza binadamu.

Mungu angempatia mipango mizuri kuliko sisi ambao tutaishia kumsikitikia na kumsonya pia.

Asante mtoa mada.
 
Castr hii comment yako imenikumbusha yule jamaa wa Linkin Park,Cheater beddington aliyejiua juzi kati!! yule jamaa alikuwa anatandika ma chorus hatariii sana kama ile ngoma bleed it out,In the end n.k.aysee mule jamaa ameimba kwa hisia sanaaaaaaa,sisi mashabiki tunafurahia burudani kumbe jamaa ana reveal na ku express what he real faces in real life!! he had dough,fast lane houses,cars,family but deep down inside ana depression balaa mpaka kuja kujiua badae,doooh!! Fame has a price too!!
 
Punguza mawazo! Yote ni mapenzi ya Mungu! Najua ni pengo lisiloweza kuzibika, kidonda kisichoweza kutibiwa, lakini hali inayoweza kuzoeleka. Najua ungetamani ale matunda ya kazi yako lakini atayaoata kwa kumuombea thawabu kwa Mungu
Kwakuwa hayupo, lakini hata angekuwepo asingebadilisha kitu kwako. Wako watu wanao wazazi wao wote lakini hawana cha maana kinachoonekana. Kaza buti, kuzaliwa ni mchakato tu unaoishia wakati wa umri wa kujitegemea, baada ya hapo wazazi wanabakia kama watu muhimu tu kwako wanaokutegemea, grieving and mooning has to have an end.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…