Kama una uwezo kifedha na haujui ufanye nini kuwekeza,au unataka kuongeza uwekezaji soma apa

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304
Vijana wengi wana idea nyingi za biashara lakini kutokana na kukosa fedha wamezikalia hizo idea,hivyo kama uko na uwezo kifedha andaa mashindano kupitia mitandao ya kijamii kama Facebook,Twitter,JF etc.

Ilo shindano lenyewe ni kushindanisha watu kukuandikia wazo bora la biashara kwenye ukurasa wako wa mtandao wa kijamii,na shindano ilo lipeleke ata kwa miezi 3 na utangaze mshindi anapata laki moja.

Utapata mawazo mengi sana ya biashara na mazuri sana sababu yatakuwa yametoka kwa vichwa mbalimbali na hao waliokupa mawazo watakuwa waliumiza sana kichwa hivyo utapata wazo sahihi.

Matajiri wengi wanatumia njia hii japo nyie hamuwezi kujua lakini wengine tunajua.Watu wengi wenye uwezo wamefanikiwa kuwekeza sehemu tofauti lakin bado wanataka mawazo mapya ili kuongeza uwekezaji.Pia njia hii haina gharama kubwa kama kuajiri mshauri wa biashara ambaye utalazimika umlipe pesa nyingi na bado hautoweza kupata mawazo mbalimbali.

kwa wale wote wenye uwezo tumieni njia hii,mtapata mawazo mapya hadi mtashangaa
 
Nadhani upo sahihi sana na nitalifanyia kazi wazo lako hapahapa JF soon! Thanks.
 
Itakuwa vyema zaidi kama huyo utakae chagua wazo lake mbali na kumpa hiyo laki moja ukashirikiana naye pia kutekeleza hilo wazo. Founder wa idea anaweza akawa na mbinu nyingi za kukamilisha idea yake, kwahiyo ukiwa naye kama partneship/Joint venture inaweza kusaidia kukamilisha hiyo idea mapema kuliko kama utaisimamia mwenyewe as if wewe ndiyo originator wa hiyo idea.
 
Mawazo ni mtaji mkubwa sana kuliko fedha. Nionavyo mimi hapa kwetu Biashara nyingi watu wanafanya kwa kuiga na wala sio wazo halisi, matokeo yake biashara/ huduma nyingi ni za kiwango cha chini sana.
 
Mawazo ni mtaji mkubwa sana kuliko fedha. Nionavyo mimi hapa kwetu Biashara nyingi watu wanafanya kwa kuiga na wala sio wazo halisi, matokeo yake biashara/ huduma nyingi ni za kiwango cha chini sana.

Hiyo ni kweli kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…