Kama unafanya haya, tafakari upya

Kama unafanya haya, tafakari upya

ndayilagije

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2016
Posts
7,491
Reaction score
8,304
Kama uko mjini,unaparty kila weekend na washkaji huko bush bimkubwa anatumia choo cha shimo tafakari upya.

Kama unamiliki nyumba zaidi ya moja mjini na unawapangaji,hali dada/kakaako anapanga room moja uswahilini tafakari upya.

Kama unamiliki magari zaidi ya moja mjini na mamiyo anatumia kibatari mafuta ya taa anapima vibaba! mmmh tafakari upya.

Kama unawatoto na unashindwa kuwapeleka kwenu likizo kwa sababu yoyote ile...tafakari sana.

Kama unadiriki kumnunulia gari demu wako hali baba yako hana hata baiskeli, kibanda kinavuja kama mpapai na kimekaa upande kama ngadu!! Kwa kweli hapo chukua hatua kabisa.

Nimekukumbusha tu .
 
Kama hujachangia uz huu basi tafakari
 
Kama una tabia ya kufatilia maisha ya watu tafakari mara mbili yake.
 
Back
Top Bottom