Morning_star
JF-Expert Member
- Apr 21, 2018
- 6,042
- 17,320
Leo nilikuwa na issue zangu zilizonipelekea kuamka asubuhi sana kwenda kati ya viunga vya Dar kukutana na jamaa yangu. Sasa niliwahi maeneo ya kukutana nikaona wakati namsubiri ebu nikapate vyombo kidogo bar ya karibu.
Nikafika bar fulani mandhari inavutia ila nikakuta wamekusanya viti upande mmoja upande wa pili wanadeki. Nikaagiza kinywaji cha aghali sana nikachukua kiti pembeni nikaanza kugonga. Sasa upande ule waliokuwa wanadeki walipomaliza wakanihamishia hapo ili waendelee kudeki sehemu niliokuwa nimekaa.
Nikawekewa kiti na meza nikatulia zangu naendelea kunyonya kinywaji changu. Sasa eeeh Bwaana!!! Yule mdada sijui kaona nini maeneo karibu na meza niliyokuwa nimekaa kapita katingisha meza na kumwaga kinywaji changu!
Iseee! Ilibidi nimuite mwenye Bar/manager inakuwaje? Wakaanza kumlaumu huyu mfanya usafi lakini hayo yote hayawezi kurudisha kinywaji changu! Niliwaangalia nikaondoka!
Nikafika bar fulani mandhari inavutia ila nikakuta wamekusanya viti upande mmoja upande wa pili wanadeki. Nikaagiza kinywaji cha aghali sana nikachukua kiti pembeni nikaanza kugonga. Sasa upande ule waliokuwa wanadeki walipomaliza wakanihamishia hapo ili waendelee kudeki sehemu niliokuwa nimekaa.
Nikawekewa kiti na meza nikatulia zangu naendelea kunyonya kinywaji changu. Sasa eeeh Bwaana!!! Yule mdada sijui kaona nini maeneo karibu na meza niliyokuwa nimekaa kapita katingisha meza na kumwaga kinywaji changu!
Iseee! Ilibidi nimuite mwenye Bar/manager inakuwaje? Wakaanza kumlaumu huyu mfanya usafi lakini hayo yote hayawezi kurudisha kinywaji changu! Niliwaangalia nikaondoka!