Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

Kama unatafuta nyumba ya kupanga DSM, kuna vitu vya kuzingatia usivichukulie poa!

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Edit:

9. Uchumi ukiruhusu tafuta chumba chenye choo ndani.

Kama uchumia na mazingira yanaruhusu, epuka nyumba zenye vyoo vya kushare. Kuna watu ustaarabu mdogo sana .

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
 
as
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
asantee ndugu. umenipa madini muhimu
 
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
Jenga ya kwako hata Chumba kimoja hii itakuweka huru
 
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
Hapa ni kujenga tu captain dodoma kuna nyumba nilikaa huyo mwenye nyumba ghafla akaanza kufunga geti saa mbili😀 sasa ndio mambo gani hayo weekend kama hii mtu urudi saa moja huo umeme wake sasa sio poa
Kwanza anauza maji kuna mota pale na matenki ikiwashwa tu mmeisha hapo hapo ana zahanati nayo inashea umeme huo huo🙌🏻🙌🏻 Uzuri kwenye nyumba ile maji hayakua shida baaasi

Jamaa ni mchungaji anakaa na mashemasi wake hapo hapo wapo wa kutosha nyumba kama kariakoo hapo bado watoto wa st john hawajaweka amapiano hadi saa nane usiku
 
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
Kodi yako ya mwaka uku kwetu nanjilinji unajenga.
 
Nilikua kwenye nyumba ya kupanga, nzuri tu. Tatizo mwenye nyumba akapandisha bei kwa asilimia zaidi ya 25, bila taarifa mapema.

Nikaona sio shida, nikahama mkataba ulivyoisha. Sasa katika harakati za kutafuta nyumba, kuna vitu nimejifunza na vingine nimeshachelewa nimejikuta najuta tayari niko ndani.

Baadhi yake:

1. Usikae na mwenye nyumba.

Nilipokua zamani nilikua sikai na mwenye nyumba. Anakuja mara chache sana. Ila sahivi nimeyatimba.

Hafu mwenye nyumba ana shughuli kila siku, mazingira yapo ovyo wala sio masafi kwasababu yeye tu ana ndugu zaidi ya 8 na watoto, ukijumlisha mnashare uwanja, aisee.

2. Jitahidi msiwe mna-share bili/matumizi ya maji au umeme.

Iwe na wapangaji wenzako au mwenye nyumba, jitahidi sana ulipie bili mwenyewe.

Ikitokea umebanwa sana bdsi angalau muwe wawili mwisho. Sub-meater hazitasaidia kitu. Mtatoa kila mtu 20,000/= ya umeme kwa mwezi wewe unashinda kazini ukirudi unawasha feni tu, kuna sista duu anachemsha maharage kwa presha cooker.

Lazima mtagombana tu.

3. Hakikisha nyumba imekamilika ujenzi, asikudanganye lipia tu namalizia wiki ili kuweka madirisha sijui.

Unavyoenda kukagua eti nyumba haijakamilika choo au dirisha, akasema lipia namalizia mtego huo.

Ukishalipia tu imeisha. Utakuta jikoni hakuna sink, feni ya sebuleni haweki, na ata maji unaweza kuta akachelewa kuyaingiza.

Jitahidi uende nyumba iliokamilika kila kitu.


4. Kama una gari, angalia upatikanaji wa funguo za geti.

Otherwise utajikuta unawahi kurudi kuogopa kufungiwa geti kama mtoto. Zamani nilikua ata saa 8 usiku naweza kutoka sahivi nawahi home saa 4 wasije funga geti. Nishalalamika ila ndio ivo, kila siku ahadi hewa.

5. Zingatia idadi ya wapangaji wenzako.
Kama unaweza, jitahidi wapangaji muwe wachache. Mkiwa kikosi kuna faida na challenge zake. Faida moja wapo unaweza pata mke hapo hapo. Ila hasara unakuta challenge hadi kwenye kamba za kuanika mfano weekend mkifua wengi kwa pamoja, makelele kila mtu akiweka singeli nk.


6. Uliza kuhusu utaratibu wa bili za maji taka, takataka/usafi na ulinzi shirikishi.

Hii michango haiwagi mikubwa ila nayo ni kero.
Kuna hii ya maji taka kuyatoa kwasababu shimo limejaa, michango ya wale wazoa takataka na ulinxi shirikishi.

7. Zingatia msimu wa mvua kunapitika? Mafuriko na nyumba kuvuja?

Kuna nyumba msimu wa mvua hazifikiki sio kwa gari wala kutembea, pia kuna uwezekano mvua ikinyesha nyumba ikawa inavuja.

8. Kelele/mishemishe za majirani.

Unaweza ukawa umeenda kucheki nyumba ukakuta pako cool, kumbe jioni kuna bar uchwara inapiga music usiku kucha.

Au ukakuta weekend au jioni ni nyumba za ibada wanatumia maspika ww unasema unapumzika wao wakakiwasha.

Kwa sasa nimeyatimba, ila kutaka kuforce kukaa Makongo Juu kumeniponza. Nikimaliza Kodi yangu naamsha.
9. Usiishi na mwenye nyumba wa kike mjane halafu mstaafu.
10. Hakikisha kama utaishi na mwenye nyumba basi awe na watoto wa kike wazuri
 
Kabla sijahamia hapa ninapoishi kwa sasa kuna sehemu nilikaa.

Wake wa wapangaji wenzangu wanakuja kupiga soga kibarazani kwangu.

Maji yalikatwa, wapangaji wakagoma kulipa hela yarudishwe.

Barabara kufika home changamoto kweli.

NIlipohamia kwa sasa mambo hayo hayapo. Shida ni mijusi ndio inanipa kero.
 
Hapa ni kujenga tu captain dodoma kuna nyumba nilikaa huyo mwenye nyumba ghafla akaanza kufunga geti saa mbili😀 sasa ndio mambo gani hayo weekend kama hii mtu urudi saa moja huo umeme wake sasa sio poa
Kwanza anauza maji kuna mota pale na matenki ikiwashwa tu mmeisha hapo hapo ana zahanati nayo inashea umeme huo huo🙌🏻🙌🏻 Uzuri kwenye nyumba ile maji hayakua shida baaasi
Hahahaha as if unakaa bure. Kuna muda nahisi kama namsumbua mwenye nyumba wakati ni biashara yake.
 
Hahahaha as if unakaa bure. Kuna muda nahisi kama namsumbua mwenye nyumba wakati ni biashara yake.
Kama hataki usumbufu arudishe kodi tuhame

Kuna hio nyumba nilikaa haina ridhiki kabisa nilivohamia tu mambo yakaanza kwenda resi hata baadhi ya mali nikauza kwaajili ya madeni basi nikajikusanya na kumwambia bibie hapa tuhame kupunguza burden maana things are worse..
Akaridhia wakati natafuta dalali mara mtoto akaumwa akalazwa wiki mbili pesa zote chali nilisota sana katika ile nyumba
 
Back
Top Bottom