Kama unataka mali utaipata wapi? Soma

Tutor B

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2011
Posts
9,025
Reaction score
6,598
Wenzangu na mie mlosoma miaka ya 80 mnakumbuka ubeti huu....
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili,
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali,
Wakataka na kauli, iwafae maishani.

Kauli ya baba ilikuwa hii....
"KAMA UNATAKA MALI, UTAIPATA SHAMBANI"

Badala yake kilimo kimekuwa kama laana, huwezi kumsikia mzazi akimhasa mwanae awe mkulima, utasikia maneno kama haya
Wewe ndo daktari wa kesho,
Wewe ndo waziri wa kesho,
Wewe ndo Diamond wa kesho,

Tufanye nini kuienzi kauli ya baba huyu iliyokuwa ikiimiza kilimo?
 
Akatamka mgonjwa,ninaumwa kwelikweli
Hata kama nikichanjwa,haitoki homa kali,
Roho naona yazima,(sikumbuki nini na nini)
Kama mnataka mali,mtayapata shambani.
 
KILIMO BADO NI SEHEMU YA KUTOKEA MKUU,KIKUBWA KUJIPANGA TU.BINAFSI NIPO KWENYE BIASHARA ILI NIPATE MTAJI MKUBWA THEN NIJIKITE KWENYE KILIMO HASA MAZAO KAMA UFUTA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…