Kamala Harris ampigia simu Rais Trump kumpongeza na kukubali matokeo ya uchaguzi

Kamala Harris ampigia simu Rais Trump kumpongeza na kukubali matokeo ya uchaguzi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Makamu wa Rais wa Marekani ambaye alikuwa Mgombea Urais wa Marekani 2024 aliyeshindwa dhidi ya Rais Mteule Donald Trump, amempigia simu Trump na kumpongeza kwa ushindi kitendo kinachoashiria amekubaliana na matokeo hayo ya uchaguzi.

Pia, Soma:

Yanayojiri katika Uchaguzi Mkuu Marekani 2024: Nani kuibuka kidedea?
Donald Trump ashinda Urais wa Marekani kwa 51.05% dhidi ya Harris Kamala aliyepata 47.46%
IMG_0577.jpeg

Kamala amempigia Trump kumpongeza na wameongea pia kuhusu mchakato wa kukabidhi madaraka kwa amani na umuhimu wa Trump kuwa Rais wa Wamarekani wote bila kujali tofauti ya Vyama au Itikadi.

Kambi ya kampeni ya Trump imepongeza alichokifanya Kamala wakisema ni ukomavu wa kisiasa.

Kamala ametoa hotuba ya kukubali kushindwa na mstakabali wa Serikali katika Chuo Kikuu cha Howard.

 
Kamala Ameonyesha kukomaa kisiasa na uelewa wa demokrasia.

Moja ya misingi mikuu ya demokrasia ni pamoja na kukubali kushindwa na kuwa tayari kukabidhi madaraka kwa kiongozi mpya aliechaguliwa kihalali na wapiga kura wanojitambua.
 
Pongezi kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwezesha uchaguzi huo
 
Marekani ni mfano wa kuigwa.
Katiba mpya ndo soln kwa nchi nyingi za kiafrica
 
Makamu wa Rais wa Marekani ambaye alikuwa Mgombea Urais wa Marekani 2024 aliyeshindwa dhidi ya Rais Mteule Donald Trump, amempigia simu Trump na kumpongeza kwa ushindi kitendo kinachoashiria amekubaliana na matokeo hayo ya uchaguzi.

Pia, Soma:

Yanayojiri katika Uchaguzi Mkuu Marekani 2024: Nani kuibuka kidedea?
Donald Trump ashinda Urais wa Marekani kwa 51.05% dhidi ya Harris Kamala aliyepata 47.46%
View attachment 3145605
Kamala amempigia Trump kumpongeza na wameongea pia kuhusu mchakato wa kukabidhi madaraka kwa amani na umuhimu wa Trump kuwa Rais wa Wamarekani wote bila kujali tofauti ya Vyama au Itikadi.
View attachment 3145630
Kambi ya kampeni ya Trump imepongeza alichokifanya Kamala wakisema ni ukomavu wa kisiasa.

Kamala ametoa hotuba ya kukubali kushindwa na mstakabali wa Serikali katika Chuo Kikuu cha Howard.
View attachment 3145630
View attachment 3145629
Nafkiri Samia akishindwa atampigia simu mbowe ama Tundu lissu kumpongeza, huyu ni mwanamke mwenzake amekubali matokeo bila ya hila zozote, anaumia lakini amejikaza huwezi ona tofauti
 
"And we will engage in Peaceful transfer of Power..." KAMALA HARRIS
👏👏👏👏🫡
 
Back
Top Bottom