Kamati tendaji Yanga mtuambie, ni nini chanzo cha ukata unaoikumba Yanga?

JFK wabongo

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2015
Posts
3,887
Reaction score
3,197
Swali hilo hapo juu. Majibu yenu tunataka. Tena mtuambie Yanga itatokaje kwenye hali hiyo? Kama hamna majibu, kwa nini bado mko ofisini?
 
Mashabiki wanagoma kwenda uwanjani sasa, mnataka muwe mnatazama mechi wenyewe bila mashabiki?
 
Timu ina udhamini, kila mechi inapata mgao wa Gate collection ina pesa ya mashindano ya CAF halafu bado mnatuambia timu ina ukata! Hizo pesa mnalishia kenge?
 
Mashabiki wa yanga wa Dar mnashindwaje kuwahoji viongozi kuhusu hili suala? Kazi yenu kudalali nafasi za uongozi yanga. Yaani ndo kusema hamna msaada wowote kwenye timu nyakati hizi za dhiki?
 
Wapige hesabu inapokea tsh ngapi za udhamini na gate collection inatumia kiasi gani kulipa wachezaji pamoja na benchi la ufundi, inalipa kiasi gani kwaajiri ya kambi pamoja na watendaji wa timu.

hesabu zipigwe kisha waangalie kimepungua kiasi na namna gani ya kukiongeza.

Kama kuna jini(deni) linakunywa pesa za Yanga muwaweke wazi washabiki na wanachama wa Club sio kuficha ficha Vyura nyie.
 
hizi timu zetu kila zinapofika kwenye hatua nzuri za mashindano ya kimataifa basi matatizo ndani ya timu yanaongezeka..bado najiuliza ni nani aliye turoga????? kama yupo tumtafute jamani na kama kafa tuonyeshwe kaburi lake !!!!!
 
Tatizo la Yanga ni uongozi. Viongozi wa Yanga siyo wasomi na wanachama wasomi wa Yanga wanaogopa kuiongoza. Majungu na ugomvi mwingi. Makundi ya kukaa getini (maninja) ndiyo yanayoamua nani awe kiongozi.
Bayern Munich wana Board of Directors yenye watu tisa.
Kuna mtu wa Adidas, Audi, Allianz na wanachama wana watu wao sita.
Yanga wauze angalau 30% stake ya club ili kuvutia investment na utaalam wa uongozi.
 
Yanga kuna chumaulete pale haiwezekani pesa zote za udhamini+michango ziishe ndani ya Muda mfupi tu.
 
wapi Akilimali? maana alisema Yanga hawamuhitaji Manji!!

kwa kweli hizi klabu zenu za bongo ni kama magenge ya wachawi tu.
 
Swali hilo hapo juu. Majibu yenu tunataka. Tena mtuambie Yanga itatokaje kwenye hali hiyo? Kama hamna majibu, kwa nini bado mko ofisini?
Chanzo ni bilioni 11 anazodai Mhindi. Namna ya kutoka hapo ni kumlipa tu, wachezaji na makocha watalipwa baadaye
 
Tatizo la Yanga na bei ya mbaazi kushuka ni sawa na pande mbili za shilingi mchawi ni mmoja tu...wala si uongozi
 
Swali hilo hapo juu. Majibu yenu tunataka. Tena mtuambie Yanga itatokaje kwenye hali hiyo? Kama hamna majibu, kwa nini bado mko ofisini?


Yanga ni timu ya jalalani tu, pesa mpaka wafadhali....Yanga kama timu haina hela na haina tofauti na timu zingine za ligi yetu isipokuwa baba yao Azam tu.
 
Duuu! Watu wamekula buyu umeamua kuchangia mwenyewe uzi wako
Unajua wabongo tunatabia ya kuridhika na majibu mepesi. Hakuna anayehoji mapato na matumizi ya timu. Ndiyo maana hata uzi unaona watu wana shy away kuchangia maana hawana ujasiri wa kuhoji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…