Kamati ya Amani ipo wapi wakati huu Polisi wakivamia makanisa na kuvuruga ibada?

Kamati ya Amani ipo wapi wakati huu Polisi wakivamia makanisa na kuvuruga ibada?

Tulimumu

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2013
Posts
14,409
Reaction score
13,262
Nauliza viongozi wote wa dini pamoja na ile inayojiita kamati ya amani iliyojitokeza kupiga marufuku matumizi ya neno mwendazake wako wapi muda huu ambapo polisi wameanza kuvamia makanisa na kukamata watu kwa kisingizio kuwa wamevaa nguo za CHADEMA.

Toka lini ikawa ni utaratibu kwa polisi kupangia waumini nguo za kuvaa wanapoenda ibadani? Mbona tumeona askari wa aina zote wakiingia makanisani na wengine kufunga ndoa wakiwa wamevaa sare za jeshi na hawajawahi kukamatwa au kutolewa kanisani?

Ni ukweli ulio wazi kuwa amani ya nchi huharibiwa na watawala kwa kutumia vyombo vyao vya mabavu kama polisi. Hakuna mahali popote wapinzani au waumini walianzisha vurugu mpaka pale polisi walipofika na kuanza kuvurumisha mabomu yao, kupiga na kukamata watu.
 
Kamati ya amani ni mimi na wewe mkuu. Kukataa ufedhuli unaofanywa na yeyote yule awe mtawala au mwanaharakati.

Kwa hili la kuvamia nyumba za ibada halina afya . Serikali na jeshi la polisi wanakosea sana. Ni kupanda chuki kwa wananchi na imani zao. Wajitafakari
 
Uzi mtamu huu sijawahi ona muda huu kamati umelala itaamka wakisikia lisu kaliamsha dude.
 
Hawajatengewa fungu bado..likiwepo utawaona tuu.. Kipindi cha mwanakwenda walifaidi sana
 
Kamati ya amani ni mimi na wewe mkuu. Kukataa ufedhuli unaofanywa na yeyote yule awe mtawala au mwanaharakati.

Kwa hili la kuvamia nyumba za ibada halina afya . Serikali na jeshi la polisi wanakosea sana. Ni kupanda chuki kwa wananchi na imani zao. Wajitafakari
Watavuna wanachopanda
 
Ngoja CCM iwavuruge hata huko Makanisani/Miskitini Kwa maana Viongozi wa dini Wanapokuwa hawajaguswa wanaona Mambo yako sawa. Hapo sasa ndio Hakiri ziwaingie na wajue CCM na serikali yake hawanaga rafiki na adui wa kudumu.

Viongozi wa Dini Wakeup mmelala sana Kuanzia Uongozi wa JPM. Mnapoona Wapizani Wanaburutwa Kichwa chini Miguu Juu Mnajifanya hamwoni Udhalimu huo sasa ni Zamu yenu, tulieni mnyolewe..
 
majambazi na maharamia husari kajisani na misikitini pia.

tuacheni akili zetu ziwe huru kufikiri,na si mahaba ya kisiasa wakati wote.
 
Ngoja CCM iwavuruge hata huko Makanisani/Miskitini Kwa maana Viongozi wa dini Wanapokuwa hawajaguswa wanaona Mambo yako sawa. Hapo sasa ndio Hakiri ziwaingie na wajue CCM na serikali yake hawanaga rafiki na adui wa kudumu. Viongozi wa Dini Wakeup mmelala sana Kuanzia Uongozi wa JPM. Mnapoona Wapizani Wanaburutwa Kichwa chini Miguu Juu Mnajifanya hamwoni Udhalimu huo sasa ni Zamu yenu, tulieni mnyolewe..
Wao wenyewe wameambiwa hakuna usajili wa kudumu
 
Back
Top Bottom