Kamati ya Bunge Yahimiza Maslahi ya Watumishi Wapya Yazingatiwe

Kamati ya Bunge Yahimiza Maslahi ya Watumishi Wapya Yazingatiwe

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI imeiomba serikali kuendelea kuboresha maslahi ya watumishi na kuwalipa stahiki zao, hususan kwa watumishi wapya, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Gl60mZ9XEAAOl7d.jpg
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Justin Lazaro Nyamoga ametoa kauli hiyo wakati wa ziara ya kukagua mradi wa Hospitali Mpya ya Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza ambayo ni miongoni mwa hospitali mpya 129 zilizojengwa na serikali kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI.

"Suala la watumishi katika baadhi ya mikoa, ikiwemo Kigoma, ni changamoto. Kamati inasisitiza mambo mawili: kuongeza watumishi hasa pale fursa zinapojitokeza, na kuhakikisha malipo stahiki yanatolewa kwa watumishi wapya na wanaohama ili kuwapa moyo wa kufanya kazi kwa bidii," amesema Mhe. Nyamoga.

Aidha,Kamati hiyo imetoa maelekezo kwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuhakikisha jenereta kubwa linapelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Uvinza, kwani lililopo sasa halina uwezo wa kusambaza umeme kwa hospitali nzima.

Gl60mZ8XwAAPbWn.jpg
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Zainab Katimba, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Mhe. Mohamed Mchengerwa, ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo ya kamati huku akiwataka watumishi wa umma kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Gl60oE2WkAAuCfV.jpg
Gl60oE6WAAAJBs9.jpg
Gl60oE1WcAA9CV4.jpg
 

Attachments

  • Gl60mZ8XkAAF6Td.jpg
    Gl60mZ8XkAAF6Td.jpg
    255.4 KB · Views: 1
  • Gl60mZ8WsAA_r8w.jpg
    Gl60mZ8WsAA_r8w.jpg
    199 KB · Views: 1
  • Gl60oFJW4AAV9UL.jpg
    Gl60oFJW4AAV9UL.jpg
    280 KB · Views: 1
Back
Top Bottom