Kamati ya Kudumu ya Bunge yazipiga pini Halmashauri kujipangia Ada ya Shule za English Medium zinazomilikiwa na Serikali

Kamati ya Kudumu ya Bunge yazipiga pini Halmashauri kujipangia Ada ya Shule za English Medium zinazomilikiwa na Serikali

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imezitaka Halmashauri zote nchini kutotumia Shule za "English Medium" za Serikali kama vyanzo vya mapato.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ya kudumu ya bunge inayoshughulikia Elimu, Utamaduni na Michezo Bi. Husna Sekiboko ametoa kauli hiyo leo Septemba 10, 2024 Jijini Dar es Salaam, Wakati wa Ziara ya kamati hiyo, iliyolenga kukagua mradi wa shule ya awali na msingi ya Richard Mgana iliyopo Kinondoni.

Sekiboko amesema kumekuwa na Mjadala mkali watu wakihoji kwanini walimu wa "English medium" wamekuwa wakilipwa na Watanzania wakati gharama za Shule hizo zikiwa juu.
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo imezitaka Halmashauri zote nchini kutotumia Shule za "English Medium" za Serikali kama vyanzo vya mapato.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ya kudumu ya bunge inayoshughulikia Elimu, Utamaduni na Michezo Bi. Husna Sekiboko ametoa kauli hiyo leo Septemba 10, 2024 Jijini Dar es Salaam, Wakati wa Ziara ya kamati hiyo, iliyolenga kukagua mradi wa shule ya awali na msingi ya Richard Mgana iliyopo Kinondoni.

Sekiboko amesema kumekuwa na Mjadala mkali watu wakihoji kwanini walimu wa "English medium" wamekuwa wakilipwa na Watanzania wakati gharama za Shule hizo zikiwa juu.
Hiyo shule ipo kinondoni maeneo gani?
 
Jambo jema kabisa hizi shule za serikali zinazofundisha kwa lugha ya kiingereza zinawalipisha ada kubwa wazazi wakati kilichobadilika ni lugha tu. Kisutu, olimpio, mugabr na nyingjnezo zina mtindo huo.
 
English medium sijui media ni ujinga tu. mimi nilishawatoa watoto wangu. na kuwarudisha shule za kayumba
 
English medium sijui media ni ujinga tu. mimi nilishawatoa watoto wangu. na kuwarudisha shule za kayumba
Hukupata tu shule nzuri ila hizi english medium ni msingi mzuri sana kwa mtoto na sekondari unaweza mpeleka kata na akatoboa kwani yale ya sekondari ndio ya shule msingi ni lugha tu imebadilika
 
Jambo jema kabisa hizi shule za serikali zinazofundisha kwa lugha ya kiingereza zinawalipisha ada kubwa wazazi wakati kilichobadilika ni lugha tu. Kisutu, olimpio, mugabr na nyingjnezo zina mtindo huo.
Serikali iache ujinga kubagua watoto wanaosoma shule za serikali ibadili shule zote za serikali kuwa English medium sio kufanya tu baadhi ya shule zake
 
Wakiondoa ada apo basi mtoto kuingia shule hizo itakuwa ni mtihani mzito, watu watahonga mpaka laki 5 kumuingiza mtoto English Medium, wakati laki 5 hiyo hiyo ndo ada.

English Medium za serikali ni nzuri, wanajitahidi kwa kweli, mimi ningependa ziongezwe zaidi.
 
English medium sijui media ni ujinga tu. mimi nilishawatoa watoto wangu. na kuwarudisha shule za kayumba
Wewe unasema ujinga wakati serikali yenyewe sasa hivi kila mkoa ina shule zake za serikali za English Medium.wewe kaa na uswahili wako
 
Wakiondoa ada apo basi mtoto kuingia shule hizo itakuwa ni mtihani mzito, watu watahonga mpaka laki 5 kumuingiza mtoto English Medium, wakati laki 5 hiyo hiyo ndo ada.

English Medium za serikali ni nzuri, wanajitahidi kwa kweli, mimi ningependa ziongezwe zaidi.
Hadi sasa bila laki 4 uiingii unaambiwa nafasi zimejaa
 
Hadi sasa bila laki 4 uiingii unaambiwa nafasi zimejaa
Ila kwa shule za Ilala mfano Bunge, Kisutu, Olympio, Diamond na Zanaki nafikiri nafasi bado zipo za kutosha.

Zamani English medium ilikuwa Olympio na Diamond tu.
 
Back
Top Bottom