Kamati ya usajili ya Simba Sports Club rekebisheni haya kabla ya Agosti 31

Ni kweli, hatuna kiungo mkabaji wa maana. Bora wamuuze Kanuti watafute mtu wa kazi ampe changamoto Mkude. Mkude kwa game zenye washambuliaji na viungo wenye kasi anawapa mzigo mabeki.

Ila seems kocha anafikiria kumtumia Inonga au beki wetu mpya kucheza kama CDM hivyo anatafuta partnership nzuri ya Onyango then mwingine acheze kama CDM.
 
Mkude ni tatizo tusiogope kusema ukweli, kila akipatikana CDM anapigwa misumari

hii imesababisha simba kutokua na watu wa maana kwenye eneo hilo kwa muda mrefu.
 
Ndio maana ya box to box, mgunda alilazimika ampeleke kitenge kwenye no 6 kwenye UKABAJI.

Akpan ni Box to box.
 
Msimu uliopita Simba SC haikuwa na tatizo kwa Kikosi chake kama Watu wengi wanavyodhani, ila tatizo Kubwa lilikuwepo katika Administration na Management hasa.
Fafanua vizuri mkuuu
 
Jamaa ameongea kitaalam sana...
Binafsi huwa naona kabisa kuna shida kwenye kuongo wa chini....tunahitaji kiungo mwenye kucheza kwa akili lakini pia yuko fast..
Pamoja kuwa umemsifia THADo LWANGA ndio alikuwa solid lakini slow.
Kwa timu ipinzani iliyocheza kwa pressure uliona ktk CL timu ikikaa nyuma sana.

Kama INONGA angeweza kuimudu hiyo nafasi ni mtu yuko fast.
Mkude tunampenda , ni kweli anakaba lakini sio mkimbiaji .

Tusubiri tuone falsafa ya ZAKI..
 
Nakazia. Simba ilikuwa na tatizo kubwa sana la viungo wabunifu ambao wanacheza kwa kujiamini mbele ya namba 6 aliyekamilika ambaye pia hatukuwa naye
 
Eneo la goal kipa naona simba wanajisahau kakolanya na ali salum wale sio wa kuwategemea manula kashaumia national team wale makipa wengine wanawekwa tu lakini hawaaminiki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…