Melubo Letema
JF-Expert Member
- Apr 1, 2020
- 416
- 414
Kwa mara ya kwanza kambi ya Riadha iliwekwa West Kilimanjaro, ilipomaliza Mafunzo ya huko, ikaamishiwa Olmotonyi Arusha, baada ya Serikali kushindwa kulipa pango , timu ikahamia Chuo Cha Habari Maalum Jijini Arusha, huku Nako wakatimuliwa baada ya kushindwa kulipa bili Mbalimbali, ikiwemo vyumba na Chakula.
Ndipo Wanariadha wakafukuzwa kwenye Chuo hicho, Kila mtu akaondoka na kwenda kwake wakati Wengine wamepewa hifadhi Kwa wasamaria Wema.
Mjumbe wa kamati ya riadha akaandika hivi:
"Lakini kuna changamoto zimejitokeza zinazosababishwa na utaratibu wa Malipo ya serikali na hivyo tumelazimika kuwapa wachezaji mapumziko ya siku mbili.
Viongozi wa Wizara, BMT na RT wanazishughulikia. Baada ya hizo siku mbili wachezaji watarudi kambini.
Si jambo la kufurahisha kwa wanariadha wetu na shirikisho kwa ujumla, lakini ndio hali halisi." Aliandika hivyo.
Waziri wa wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Anahitajika Ajitafakari , Kwa kuwa Juzi akizindua Marathon Moja alisikika akisema Kambi zote zipo na zimejitosheleza na Pesa zimetolewa.
Ndipo Wanariadha wakafukuzwa kwenye Chuo hicho, Kila mtu akaondoka na kwenda kwake wakati Wengine wamepewa hifadhi Kwa wasamaria Wema.
Mjumbe wa kamati ya riadha akaandika hivi:
"Lakini kuna changamoto zimejitokeza zinazosababishwa na utaratibu wa Malipo ya serikali na hivyo tumelazimika kuwapa wachezaji mapumziko ya siku mbili.
Viongozi wa Wizara, BMT na RT wanazishughulikia. Baada ya hizo siku mbili wachezaji watarudi kambini.
Si jambo la kufurahisha kwa wanariadha wetu na shirikisho kwa ujumla, lakini ndio hali halisi." Aliandika hivyo.
Waziri wa wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Anahitajika Ajitafakari , Kwa kuwa Juzi akizindua Marathon Moja alisikika akisema Kambi zote zipo na zimejitosheleza na Pesa zimetolewa.