Kamera za CCTV kifaa muhimu kinosaidia kupata ushahidi. Watanzania wajizoeshe kukusanya ushahidi na kuuhifadhi kwa kutumia simu ya mkononi

Kamera za CCTV kifaa muhimu kinosaidia kupata ushahidi. Watanzania wajizoeshe kukusanya ushahidi na kuuhifadhi kwa kutumia simu ya mkononi

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Moja kwa moja kwenye mada na leo nazungumzia umuhimu wa kamera za CCTV.

CCTV (closed- circuit television) ambayo pia yajulikana kama video ya uchunguzi au Video Surveillance ni kifaa muhimu sana cha ulinzi kwenye dunia ya leo.

CCTV hutumika katika maeneo ya umma kwa minajili ya kubaini na kuzuia uhalifu (detection and prevention of crime) na huongozwa na sheria na kanuni za matumizi yake.

Kutokana na matukio mengi ya uhalifu katika sehemu mbalimbali duniani kupita bila kupata ushahidi wa kutoka kiasi cha kuweza kumtia hatiani mtuhumiwa wa uhalifu, sehemu nyingi zimewekwa kamera za CCTV.

Ukiwa Marekani na Ulaya na sasa sehemu nyingi duniani huwezi kukosa kuona kamera za CCTV katika majumba, nyumba za makazi, maofisi, mabarabarani, katika vyombo vya usafiri kama reli mabasi magari ya kukodi (taxis) na ndege vyote hivi vimefungwa kamera za CCTV.

Ukija kwa maeneo kama jeshi la polisi na idara kama za zimamoto wao nao hutumia kamera za kurekodi shughuli zao popote wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao. Polisi (wa doria na wale wabeba silaha au armed police) na hata walinzi wa maduka (security guard) nao pia huvaa BodyCam ambazo ni kwa ajili ya kurekodi matuko yoyote na pia kwa ajili ya usalama wa mhusika.

Polisi wa nchi hizi ziloendelea wakienda kutekeleza kazi yao iwe ni kukamata muuza madawa ya kulevya, au mhalifu yoyote ni lazima wavae kamera za kurekodi matukio. Ni lazima waiwashe kamera hiyo ili kurekodi tukio wanolifanya na baadae kuzima.

Baadae kinofanyika ni kuinywila kamera hiyo/hizo na kufanya analysis na utambuzi wa tukio/matukio na baadae kuchukua hatua kulingana na maamuzi ya mwendesha mashtaka au jaji.

Lakini pamoja na hayo yote wananchi wa nchi hizi nao siku hizi wamekuwa makini na shughuli zozote na mapolisi na uhalifu kwa ujumla. Mtu huweza kuchukua tukio lolote kwa kutumia simu ya mkononi au kamera ya kwenye gari (dashcam) ambazo baadae polis huweza kuweka laini maalum ambayo wananchi wataweza kujaza video hizo.

Pia polisi wakianza uchunguzi ni lazima watataka kuona video zinozunguka eneo tukio lilipotokea na pia kuuliza raia kuhusu kamera zao za majumbani au milango mbele ya nyumba zao.

Kutokana na utendaji kazi zao polisi wa nchi hizi kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa wananchi na endapo tukio limetokea, kitu cha kwanza polisi watakifanya ni kuitisha "press conference" ili kueleza tatizo na kisha kuomba wananchi watoe ushirikiano.

Sasa tukiangalia tukio na kutekwa kwa mzee Mohamed Ally Kibao, kitu cha kwanza kabisa ni kulichukua basi alokuwa akisafiria na kulihifadhi kwa uchunguzi wa forensic na pia kuwasiliana na abiria wote walokuwamo kwenye basi.

Abiria hao wataweza kutoa ushirikiano wa kueleza namna tukio lilivyotokea na namna mzee huyo alivyofuatwa kwenye basi na kisha kuteremshwa. Litakuwa ni jambo la kushangaza endapo hakutakuwa na raia yoyote ambae amerekodi tukio hilo isipokuwa kama raia hao walitishiwa maisha yao na kuambiwa wasifanye kitu chochote.

Nini kifanyike.

1. Wananchi watanzania wenzangu wajifunze kutumia simu zao kurekodi matukio yoyote ambayo yaweza kutumiwa kama ushahidi. Hilo liende sambamba na kuanza kununua DashCams za kufunga katika magari ili kujilinda na matukio kama wizi, kutekwa na ajali za barabarani.

2. Vyombo za usafiri kama mabasi ya abiria umefika wakati sasa wa kuhakikisha mabasi ya kisasa yote kamera zake zafanya kazi. Ni lazima mabasi yote ya kisasa kwa sasa yamefungwa kamera toka kiwandani tayari kwa kazi ya kurekodi hivyo kinohitajika ni kuhakikisha kamera hizo zafanya kazi na matukio hayo yamekodiwa na kuhifadhiwa kwenye Kanzidata ya Cloud ambayo ni vigumu kuiingilia.

Cloud storage si ghali na wenye mabasi waweza kuilipia kwa dola chache sana kila mwezi kulingana na ujazo wa data.

3. Wananchi kuwa macho na makini na maisha yao kwani hakuna imani kuwa usalama wao walindwa masaa yote na jeshi la polisi.

Mwisho, matukio ya kutekwa, kuteswa na kuuawa kwa watanzania ni jambo baya na linotia doa serikali na jeshi la polisi. Serikali iamke na ijitokeze kwa kuunda tume huru itayochunguza madhila haya yanotendwa na kundi la watu makatili.

Yawezekana lengo ni kuwatia hofu raia lakini bado misingi ya katiba ya JMT yatoa haki ya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni, hayo yote yakiwa ni sehemu ya demokrasia tunoipigia debe kila mara. Je, kwanini raia watiwe hofu kwa kuua au kuteka na kutesa?

Ubalozi wa Marekani umetoa tamko na pengine balozi zingine zitatoa tamko kulingana na kasi ya uwajibikaji wa tukio lolotokea hivi majuzi.
 
Mfano tukio la viongozi wa CDM kupigwa na polisi. Unajiuliza hivi wanashindwa hata kutembea na camera za siri zinazoweza kuwa na muundo wa miwani au peni na kurekodi matukio na kuyatumia kama ushahidi mahakamani na hata kuziachia wazi mtandaoni umma uuone ukweli.
 
Moja kwa moja kwenye mada na leo nazungumzia umuhimu wa kamera za CCTV.

CCTV (closed- circuit television) ambayo pia yajulikana kama video ya uchunguzi au Video Surveillance ni kifaa muhimu sana cha ulinzi kwenye dunia ya leo.

CCTV hutumika katika maeneo ya umma kwa minajili ya kubaini na kuzuia uhalifu (detection and prevention of crime) na huongozwa na sheria na kanuni za matumizi yake.

Kutokana na matukio mengi ya uhalifu katika sehemu mbalimbali duniani kupita bila kupata ushahidi wa kutoka kiasi cha kuweza kumtia hatiani mtuhumiwa wa uhalifu, sehemu nyingi zimewekwa kamera za CCTV.

Ukiwa Marekani na Ulaya na sasa sehemu nyingi duniani huwezi kukosa kuona kamera za CCTV katika majumba, nyumba za makazi, maofisi, mabarabarani, katika vyombo vya usafiri kama reli mabasi magari ya kukodi (taxis) na ndege vyote hivi vimefungwa kamera za CCTV.

Ukija kwa maeneo kama jeshi la polisi na idara kama za zimamoto wao nao hutumia kamera za kurekodi shughuli zao popote wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao. Polisi (wa doria na wale wabeba silaha au armed police) na hata walinzi wa maduka (security guard) nao pia huvaa BodyCam ambazo ni kwa ajili ya kurekodi matuko yoyote na pia kwa ajili ya usalama wa mhusika.

Polisi wa nchi hizi ziloendelea wakienda kutekeleza kazi yao iwe ni kukamata muuza madawa ya kulevya, au mhalifu yoyote ni lazima wavae kamera za kurekodi matukio. Ni lazima waiwashe kamera hiyo ili kurekodi tukio wanolifanya na baadae kuzima.

Baadae kinofanyika ni kuinywila kamera hiyo/hizo na kufanya analysis na utambuzi wa tukio/matukio na baadae kuchukua hatua kulingana na maamuzi ya mwendesha mashtaka au jaji.

Lakini pamoja na hayo yote wananchi wa nchi hizi nao siku hizi wamekuwa makini na shughuli zozote na mapolisi na uhalifu kwa ujumla. Mtu huweza kuchukua tukio lolote kwa kutumia simu ya mkononi au kamera ya kwenye gari (dashcam) ambazo baadae polis huweza kuweka laini maalum ambayo wananchi wataweza kujaza video hizo.

Pia polisi wakianza uchunguzi ni lazima watataka kuona video zinozunguka eneo tukio lilipotokea na pia kuuliza raia kuhusu kamera zao za majumbani au milango mbele ya nyumba zao.

Kutokana na utendaji kazi zao polisi wa nchi hizi kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa wananchi na endapo tukio limetokea, kitu cha kwanza polisi watakifanya ni kuitisha "press conference" ili kueleza tatizo na kisha kuomba wananchi watoe ushirikiano.

Sasa tukiangalia tukio na kutekwa kwa mzee Mohamed Ally Kibao, kitu cha kwanza kabisa ni kulichukua basi alokuwa akisafiria na kulihifadhi kwa uchunguzi wa forensic na pia kuwasiliana na abiria wote walokuwamo kwenye basi.

Abiria hao wataweza kutoa ushirikiano wa kueleza namna tukio lilivyotokea na namna mzee huyo alivyofuatwa kwenye basi na kisha kuteremshwa. Litakuwa ni jambo la kushangaza endapo hakutakuwa na raia yoyote ambae amerekodi tukio hilo isipokuwa kama raia hao walitishiwa maisha yao na kuambiwa wasifanye kitu chochote.

Nini kifanyike.

1. Wananchi watanzania wenzangu wajifunze kutumia simu zao kurekodi matukio yoyote ambayo yaweza kutumiwa kama ushahidi. Hilo liende sambamba na kuanza kununua DashCams za kufunga katika magari ili kujilinda na matukio kama wizi, kutekwa na ajali za barabarani.

2. Vyombo za usafiri kama mabasi ya abiria umefika wakati sasa wa kuhakikisha mabasi ya kisasa yote kamera zake zafanya kazi. Ni lazima mabasi yote ya kisasa kwa sasa yamefungwa kamera toka kiwandani tayari kwa kazi ya kurekodi hivyo kinohitajika ni kuhakikisha kamera hizo zafanya kazi na matukio hayo yamekodiwa na kuhifadhiwa kwenye Kanzidata ya Cloud ambayo ni vigumu kuiingilia.

Cloud storage si ghali na wenye mabasi waweza kuilipia kwa dola chache sana kila mwezi kulingana na ujazo wa data.

3. Wananchi kuwa macho na makini na maisha yao kwani hakuna imani kuwa usalama wao walindwa masaa yote na jeshi la polisi.

Mwisho, matukio ya kutekwa, kuteswa na kuuawa kwa watanzania ni jambo baya na linotia doa serikali na jeshi la polisi. Serikali iamke na ijitokeze kwa kuunda tume huru itayochunguza madhila haya yanotendwa na kundi la watu makatili.

Yawezekana lengo ni kuwatia hofu raia lakini bado misingi ya katiba ya JMT yatoa haki ya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni, hayo yote yakiwa ni sehemu ya demokrasia tunoipigia debe kila mara. Je, kwanini raia watiwe hofu kwa kuua au kuteka na kutesa?

Ubalozi wa Marekani umetoa tamko na pengine balozi zingine zitatoa tamko kulingana na kasi ya uwajibikaji wa tukio lolotokea hivi majuzi.
Kama ile iliyomfuata Mo kutoka Ostabei ikamkimbiza mpaka Mwenge wakapotezana! Mhe. Lazaro karibu huku tena.
 
Mfano tukio la viongozi wa CDM kupigwa na polisi. Unajiuliza hivi wanashindwa hata kutembea na camera za siri zinazoweza kuwa na muundo wa miwani au peni na kurekodi matukio na kuyatumia kama ushahidi mahakamani na hata kuziachia wazi mtandaoni umma uuone ukweli.
Hiyohiyo simu yako ya mkononi waweza kuitumia kukusanya data khasa video footage na kuipeleka moja kwa moja kwenye server mara simu inapokuwa connected na internet.

Zipo apps kadhaa zinoweza kusaidia kazi hiyo.
 
Mfano tukio la viongozi wa CDM kupigwa na polisi. Unajiuliza hivi wanashindwa hata kutembea na camera za siri zinazoweza kuwa na muundo wa miwani au peni na kurekodi matukio na kuyatumia kama ushahidi mahakamani na hata kuziachia wazi mtandaoni umma uuone ukweli.
Mahakama zipi??
 
Pale alikoshambuliwa Mh Lisu hapakuwa na hizo camera?? Nini kimefanyika hadi leo?? Tatizo la nchi yetu liko pale JUU kupitia Katiba tuliyonayo.
 
Hiyohiyo simu yako ya mkononi waweza kuitumia kukusanya data khasa video footage na kuipeleka moja kwa moja kwenye server mara simu inapokuwa connected na internet.

Zipo apps kadhaa zinoweza kusaidia kazi hiyo.
Hilo linajulikana. Mfano tukio la kutekwa mzee Kibao inasemwa kuwa watekaji waliwatishia abira wasipige picha huoni tatizo hapo sio watu kutojua kutumia simu zao bali ni hofu ya kuonekana ndio maana umeona hapo kumetajwa camera za siri ambazo ni ngumu kujulikana wakati inafanya kazi.
 
Nyumbani kwangu technician alinifungia old android phones kama cctv. Mwaka wa 3 huu na zinafanya vyema. Mpaka toilet ipo moja
 
Hizo hizo za ccm.
Mkuu umesahau ule Mhimili uliojichimbia chini zaidi Kiongozi wake alisema " vijana wanatengeneza vi drama" kujiteka??? After few days anakuja kutoa Masikitiko yake juu ya matendo yale maovu. Nani analeta vidrama hapo?? Tatizo liko hapo?? Kimemo kikishaenda tu pale kwenye Mihimili mingine ikiwepo Mshakama ushahidi wako wote unatupwa gizani.

Katiba Mpya Katiba Mpya Katiba Mpya Mihimili mingine iweze kuwa Huru.
 
Moja kwa moja kwenye mada na leo nazungumzia umuhimu wa kamera za CCTV.

CCTV (closed- circuit television) ambayo pia yajulikana kama video ya uchunguzi au Video Surveillance ni kifaa muhimu sana cha ulinzi kwenye dunia ya leo.

CCTV hutumika katika maeneo ya umma kwa minajili ya kubaini na kuzuia uhalifu (detection and prevention of crime) na huongozwa na sheria na kanuni za matumizi yake.

Kutokana na matukio mengi ya uhalifu katika sehemu mbalimbali duniani kupita bila kupata ushahidi wa kutoka kiasi cha kuweza kumtia hatiani mtuhumiwa wa uhalifu, sehemu nyingi zimewekwa kamera za CCTV.

Ukiwa Marekani na Ulaya na sasa sehemu nyingi duniani huwezi kukosa kuona kamera za CCTV katika majumba, nyumba za makazi, maofisi, mabarabarani, katika vyombo vya usafiri kama reli mabasi magari ya kukodi (taxis) na ndege vyote hivi vimefungwa kamera za CCTV.

Ukija kwa maeneo kama jeshi la polisi na idara kama za zimamoto wao nao hutumia kamera za kurekodi shughuli zao popote wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao. Polisi (wa doria na wale wabeba silaha au armed police) na hata walinzi wa maduka (security guard) nao pia huvaa BodyCam ambazo ni kwa ajili ya kurekodi matuko yoyote na pia kwa ajili ya usalama wa mhusika.

Polisi wa nchi hizi ziloendelea wakienda kutekeleza kazi yao iwe ni kukamata muuza madawa ya kulevya, au mhalifu yoyote ni lazima wavae kamera za kurekodi matukio. Ni lazima waiwashe kamera hiyo ili kurekodi tukio wanolifanya na baadae kuzima.

Baadae kinofanyika ni kuinywila kamera hiyo/hizo na kufanya analysis na utambuzi wa tukio/matukio na baadae kuchukua hatua kulingana na maamuzi ya mwendesha mashtaka au jaji.

Lakini pamoja na hayo yote wananchi wa nchi hizi nao siku hizi wamekuwa makini na shughuli zozote na mapolisi na uhalifu kwa ujumla. Mtu huweza kuchukua tukio lolote kwa kutumia simu ya mkononi au kamera ya kwenye gari (dashcam) ambazo baadae polis huweza kuweka laini maalum ambayo wananchi wataweza kujaza video hizo.

Pia polisi wakianza uchunguzi ni lazima watataka kuona video zinozunguka eneo tukio lilipotokea na pia kuuliza raia kuhusu kamera zao za majumbani au milango mbele ya nyumba zao.

Kutokana na utendaji kazi zao polisi wa nchi hizi kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa wananchi na endapo tukio limetokea, kitu cha kwanza polisi watakifanya ni kuitisha "press conference" ili kueleza tatizo na kisha kuomba wananchi watoe ushirikiano.

Sasa tukiangalia tukio na kutekwa kwa mzee Mohamed Ally Kibao, kitu cha kwanza kabisa ni kulichukua basi alokuwa akisafiria na kulihifadhi kwa uchunguzi wa forensic na pia kuwasiliana na abiria wote walokuwamo kwenye basi.

Abiria hao wataweza kutoa ushirikiano wa kueleza namna tukio lilivyotokea na namna mzee huyo alivyofuatwa kwenye basi na kisha kuteremshwa. Litakuwa ni jambo la kushangaza endapo hakutakuwa na raia yoyote ambae amerekodi tukio hilo isipokuwa kama raia hao walitishiwa maisha yao na kuambiwa wasifanye kitu chochote.

Nini kifanyike.

1. Wananchi watanzania wenzangu wajifunze kutumia simu zao kurekodi matukio yoyote ambayo yaweza kutumiwa kama ushahidi. Hilo liende sambamba na kuanza kununua DashCams za kufunga katika magari ili kujilinda na matukio kama wizi, kutekwa na ajali za barabarani.

2. Vyombo za usafiri kama mabasi ya abiria umefika wakati sasa wa kuhakikisha mabasi ya kisasa yote kamera zake zafanya kazi. Ni lazima mabasi yote ya kisasa kwa sasa yamefungwa kamera toka kiwandani tayari kwa kazi ya kurekodi hivyo kinohitajika ni kuhakikisha kamera hizo zafanya kazi na matukio hayo yamekodiwa na kuhifadhiwa kwenye Kanzidata ya Cloud ambayo ni vigumu kuiingilia.

Cloud storage si ghali na wenye mabasi waweza kuilipia kwa dola chache sana kila mwezi kulingana na ujazo wa data.

3. Wananchi kuwa macho na makini na maisha yao kwani hakuna imani kuwa usalama wao walindwa masaa yote na jeshi la polisi.

Mwisho, matukio ya kutekwa, kuteswa na kuuawa kwa watanzania ni jambo baya na linotia doa serikali na jeshi la polisi. Serikali iamke na ijitokeze kwa kuunda tume huru itayochunguza madhila haya yanotendwa na kundi la watu makatili.

Yawezekana lengo ni kuwatia hofu raia lakini bado misingi ya katiba ya JMT yatoa haki ya uhuru wa kujieleza na kutoa maoni, hayo yote yakiwa ni sehemu ya demokrasia tunoipigia debe kila mara. Je, kwanini raia watiwe hofu kwa kuua au kuteka na kutesa?

Ubalozi wa Marekani umetoa tamko na pengine balozi zingine zitatoa tamko kulingana na kasi ya uwajibikaji wa tukio lolotokea hivi majuzi.
Huu ndo digital ulinzi
 
Back
Top Bottom