Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 590
- 1,648
Katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na chanel ya ITV tarehe 16 May, 2022, Kamisaa wa Sensa Anna Makinda alihojiwa kuhusu zoezi la sensa, na moja ya kitu alichoelezea ni bajeti ya Sensa, ambapo alisema bajeti ya Sensa kwa mwaka 2022 ni Tsh bilioni 629.
Cha kushangaza jana tarehe 1 September, 2022 Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kuhusu maendeleo ya Sensa ya Watu na Makazi, Sensa ya Majengo na Sensa ya Anwani za Makazi hadi kufikia August 31, 2022, alisema kuwa bajeti ya Sensa ya Watu na Makazi na Sensa ya Majengo ambayo iliidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ni kiasi cha Tsh. billion 400.
Kwa mkanganyiko huu kati ya Kamisaa wa Sensa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali unaleta picha gani, kwamba hakuna mawasiliano kati yao au kuna harufu ya upigaji kwenye zoezi hili?
Hii imekaaje wadau?
Cha kushangaza jana tarehe 1 September, 2022 Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kuhusu maendeleo ya Sensa ya Watu na Makazi, Sensa ya Majengo na Sensa ya Anwani za Makazi hadi kufikia August 31, 2022, alisema kuwa bajeti ya Sensa ya Watu na Makazi na Sensa ya Majengo ambayo iliidhinishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ni kiasi cha Tsh. billion 400.
Kwa mkanganyiko huu kati ya Kamisaa wa Sensa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali unaleta picha gani, kwamba hakuna mawasiliano kati yao au kuna harufu ya upigaji kwenye zoezi hili?
Hii imekaaje wadau?