Kamisheni ya Mitandao ya kifedha M-PESA na HALOPESA

huko kwenu vipi

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2015
Posts
1,520
Reaction score
1,462
Habarini za asubuhi wanajamvi....

Mimi ni mfanyabiashara wa biashara ya mitandao ya kifedha kama vile M-pesa,halopesa,tigo pesa na Airtel money..

Lakini nizungumzie kidogo kwenye mitandao ya kifedha ya M-pesa na Halopesa....


Baada ya kulipwa Kamisheni(M-pesa) kuanzia tarehe 1 hadi kwenye tareh 17 hivi Kamisheni inakuwa inapanda kwa kasi baada ya tarehe hizo hadi tarehe 31 yaan kiasi kinachoongezeka kwenye Kamisheni ni kidogo sana miamala ni ile ile kwanini?

Au ni kwangu tu

Je Kama ni kwangu tu nakwama wap?

Kamisheni yangu tarehe inakuwa nzuri kweli kweli lakin kadiri navyoelekea mwisho wa mwezi mambo yanabadilika,

Wafanyabiashara wenzangu na ninyi huwa mnaona hili?

Mtandao wa halopesa ni kabisa sionagi kitu najikuta kwa mwezi napokea 20,000 kushuka chini na nimefanya utafiti hata mjini wanapokea kamisheni ndogo sana,

Tunakwama WAP kwa mtandao huu wa Halopesa?
 
kwanza kabisa kamisheni ya kutuma hua ni ndogo kuliko kutoa,hivyo kama unafanya miamala mingi ya kuweka lazima upate kamisheni ndogo
2. kama unafanya miamala mingi ya kutuma pesa nje ya mkoa wako kwa mpesa mwisho wa mwezi kuna makato unakatwa.
3. kama unafanya miamala mingi lakini ya pesa kidogo hauwezi kupata mgao mkubwa kama yule anaefanya miamala ya hela nyingi cha msingi tu piga hesabu kwa siku unaingiza shngap zidisha mara 30
 


Ooooooh katika vitu ambaavyo sivijui ni hivi...

Kumbe ukituma hela kwenda mikoa mengine kuna makato mwisho wa mwezi?

Duh
 
Reactions: apk
Ooooooh katika vitu ambaavyo sivijui ni hivi...

Kumbe ukituma hela kwenda mikoa mengine kuna makato mwisho wa mwezi?

Duh
Hapa walichemka inaonekana kama vile kila mkoa una mwekezaji wake ambao mawakala wa mkoa husika wapo chini yake.
Hivyo basi swali langu ni hivi inakuwaje kama laini ya uwakala ilisajiliwa Mbeya then ikauzwa Dar itakuwa inatambulika ipo Mbeya au Dar?
Asante
 
Wakikujibu unitag
 
Kimsingi tu kwa sasa biashara ya miamala ya simu commision zake ni ndogo mnooo.M pesa sio kama zamani mtu unakunja hata 600k mwisho wa mwezi.
 
Hawakuchemka manake ni namna ya kuongeza faida kwa upande wao manake unapo mwekea mteja wa karibu yako atume kuna hela inakatwa ile ndio wanaitaka ya kuongeza mtaji kwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…