Kamishna Mkuu TRA: Mwaka wa fedha 2024/2025, TRA ilivuka malengo yake kwa kukusanya Shilingi Trilioni 16.528

Kamishna Mkuu TRA: Mwaka wa fedha 2024/2025, TRA ilivuka malengo yake kwa kukusanya Shilingi Trilioni 16.528

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Yusuph Juma Mwenda, amesema Siku ya Mlipakodi ni tukio maalum linalolenga kutambua na kuwashukuru walipakodi wa kada zote kwa mchango wao katika maendeleo ya taifa.

Akizungumza Januari 23, 2025, jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho hayo, Bw. Mwenda ameeleza kuwa utoaji wa tuzo unakusudia kutambua walipakodi waliotoa mchango mkubwa katika sekta mbalimbali, zikiwemo sekta ya madini, taasisi za umma, taasisi za fedha, uzalishaji na viwanda, pamoja na sekta ya utalii.

Bw. Mwenda amebainisha kuwa baadhi ya walipakodi walifanikisha makusanyo makubwa ya kodi katika nusu ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/2025, ambapo TRA ilivuka malengo yake kwa kukusanya Shilingi Trilioni 16.528. Washindi hao pia wametunukiwa tuzo maalum kwa mchango wao.
 
kati ya hizo, Trillion 12 tunawapelekea world bank na IMF. Mwanaume mwenye gololi mbili aje apinge. Nipo hapa.

 
Baada ya hapo zinachotwa na wenyewe mamlaka ni mwendo wa kufungua petrol stations na malls kila sehemu
🗣🎼🎵Hili linaniliza saaaaana hili linalizaaaa sanaa 🎶🎼
 
Kumbe kulipa kodi ni fadhila na sio wajibu?
 
Narudia tena, trillion 12 kati ya hizo zinaenda World bank na IMF, halafu tunarudishiwa tena zote kama mkopo wenye riba ya kibiashara.., yaani pesa zetu halafu tunakopeshwa kwa riba.., aje mtu apinge, hatu Mwigulu aje hapa kupinga, si yupo humu?

 
Back
Top Bottom